Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 7

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

Ufalme wa Mungu Ni Nini?

1. Ufalme wa Mungu ni nini?

Juu ya nini Yesu njo Mufalme mwenye anastahili kabisa?​—MARKO 1:40-42.

Ufalme wa Mungu ni serikali ao guvernema yenye kuwa mbinguni. Serikali hiyo itatosha serikali zote zenye kuwa ku dunia na itafanya mapenzi ya Mungu ifanyike mbinguni na ku dunia. Ile ni habari njema kabisa. Watu wako na lazima ya kuongozwa na serikali ya muzuri; hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utawatimizia jambo hilo. Utafanya watu wote waishi katika umoja ku dunia.​—Soma Danieli 2:44; Matayo 6:9, 10; 24:14.

Kila ufalme unapaswa kuwa na Mufalme. Yehova alimuchagua Mwana wake, Yesu Kristo, ili akuwe Mufalme wa Ufalme wake.​—Soma Ufunuo 11:15.

Angalia video Ufalme wa Mungu Ni Nini?

2. Juu ya nini Yesu njo Mufalme mwenye anastahili kabisa?

Yesu njo Mufalme mwenye anastahili juu iko mwema na anapenda sana mambo yenye kuwa sawa. (Matayo 11:28-30) Tena, iko na nguvu kabisa ya kusaidia watu kwa sababu atatawala dunia na iko mbinguni. Kisha kufufuliwa, Yesu alipanda mbinguni, akakaa kwenye mukono wa kuume wa Mungu ili kungojea apewe Ufalme. (Waebrania 10:12, 13) Mwishowe, Mungu alimupatia mamlaka na akaanza kutawala.​—Soma Danieli 7:13, 14.

3. Ni nani watatawala pamoja na Yesu?

Kikundi cha watu wenye kuitwa “watakatifu” watatawala pamoja na Yesu mbinguni. (Danieli 7:27) Mitume waaminifu wa Yesu njo walikuwa watakatifu wa kwanza wenye walichaguliwa. Yehova ameendelea kuchagua watakatifu wengine mupaka leo, wanaume na wanamuke waaminifu. Kama Yesu, watakatifu hao wanafufuliwa katika mwili wa roho.​—Soma Yohana 14:1-3; 1 Wakorinto 15:42-44.

Ni watu ngapi wataenda mbinguni? Yesu aliwaita “kundi ndogo.” (Luka 12:32) Wote watafikia kuwa watu 144 000. Watatawala dunia pamoja na Yesu.​—Soma Ufunuo 14:1.

4. Kulitokea nini wakati Yesu alianza kutawala?

Ufalme wa Mungu ulianza kutawala mu mwaka wa 1914. * Jambo la kwanza lenye Yesu alifanya kisha tu kufanywa kuwa Mufalme ni hili: alimutupa Shetani na pepo wake wachafu ku dunia. Shetani alikasirika sana na akaanza kuleta mateso mu dunia yote. (Ufunuo 12:7-10, 12) Kuanzia wakati huo, mateso ya watu imeongezeka sana. Vita, njaa, magonjwa ya kuambukiza, matetemeko ya inchi; ile mambo yote ni sehemu ya “alama” yenye kuonyesha kama hivi karibuni Ufalme wa Mungu utatawala dunia.​—Soma Luka 21:7, 10, 11, 31.

5. Ufalme wa Mungu uko unafanya mambo gani leo?

Kupitia kazi ya kuhubiri yenye inafanywa mu dunia yote, Ufalme wa Mungu unaunganisha watu wengi sana kutoka mu mataifa yote. Mamilioni ya watu wapole wanaendelea kuwa raia wa Ufalme wa Mungu wenye kutawaliwa na Yesu. Ufalme wa Mungu utalinda watu hao wakati utaharibu ulimwengu huu mubaya. Kwa hiyo, kila mutu mwenye anataka kupata faida zenye Ufalme wa Mungu utaleta, anapaswa kujifunza kuwa raia wa Yesu na kumutii.​—Soma Ufunuo 7:9, 14, 16, 17.

Kwa kipindi cha miaka elfu moja, Ufalme wa Mungu utatimiza kusudi lenye Mungu alikuwa nalo ku mwanzo juu ya wanadamu. Dunia yote itakuwa paradiso. Ku mwisho wa ile miaka elfu moja, Yesu atamurudishia Baba yake Ufalme. (1 Wakorinto 15:24-26) Kuko mutu fulani mwenye ungependa kuelezea juu ya Ufalme wa Mungu?​—Soma Zaburi 37:10, 11, 29.

 

^ fu. 6 Ili kupata habari zaidi juu ya unabii wa Biblia wenye kuonyesha kama Yesu alianza kutawala mu mwaka wa 1914, ona ukurasa wa 217-220 wa kitabu Biblia Inatufundisha Nini?