Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 5

Mungu Anapenda Dunia Ikuwe Namna Gani?

Mungu Anapenda Dunia Ikuwe Namna Gani?

1. Juu ya nini Mungu aliumba dunia?

Yehova alipatia wanadamu dunia. Dunia njo makao yetu. Adamu na Eva, mwanaume na mwanamuke wa kwanza, hawakuumbwa ili waishi mbinguni. Wakati Mungu aliwaumba, alikuwa ameumba malaika ili waishi mbinguni. (Yobu 38:4, 7) Mungu alimutia mutu wa kwanza mu paradiso yenye kupendeza yenye iliitwa bustani ao shamba la Edeni. (Mwanzo 2:15-17) Yehova alimupatia Adamu na watoto wenye angezaa, tumaini la kuishi milele ku dunia.​—Soma Zaburi 37:29; 115:16.

Ku mwanzo, bustani ya Edeni tu njo ilikuwa paradiso. Dunia ingepaswa kujaa watoto wa Adamu na Eva. Kisha wakati fulani, wangetawala dunia yote na kuifanya kuwa paradiso. (Mwanzo 1:28) Dunia haitaharibiwa hata siku moja. Itakuwa makao ya watu milele.​—Soma Zaburi 104:5.

Angalia video Sababu Gani Mungu Aliumba Dunia?

2. Juu ya nini dunia haiko paradiso leo?

Adamu na Eva hawakumutii ao kumusikia Mungu, kwa hiyo, Mungu aliwafukuza mu bustani ya Edeni. Paradiso ikapotea, na hakuna mutu mwenye ameweza kuirudisha. Biblia inasema hivi: “Dunia imetiwa katika mukono wa muovu.”​—Yobu 9:24.​—Soma Mwanzo 3:23, 24.

Je, Yehova amesahau kusudi lenye alikuwa nalo ku mwanzo juu ya watu? Hapana! Yeye ni mweza-yote. Hawezi kushindwa kutimiza kusudi lake. (Isaya 45:18) Atarudishia watu hali yenye alipenda wakuwe nayo tangu mwanzo.​—Soma Zaburi 37:11, 34.

3. Paradiso itarudishwa namna gani?

Paradiso itarudishwa ku dunia wakati wa utawala wa Yesu, Mufalme mwenye Mungu ameweka. Ku vita yenye kuitwa Armagedoni, Yesu ataongoza malaika wa Mungu ili kuharibu watu wote wenye wanamupinga Mungu. Kisha, Yesu atamufunga Shetani kwa miaka elfu moja (1 000). Watu wa Mungu wataokoka uharibifu huo kwa sababu Yesu atawaongoza na kuwalinda. Watapata uzima wa milele mu Paradiso ku dunia.​—Soma Ufunuo 20:1-3; 21:3, 4.

4. Mateso itaisha wakati gani?

Mungu atamaliza mateso ku dunia wakati gani? Yesu alitupatia “alama” yenye ingetuonyesha kama mwisho uko karibu. Hali zenye kuwa ku dunia leo zinatia maisha ya watu mu hatari na zinaonyesha kama tunaishi sasa wakati wa “umalizio wa mupangilio wa mambo.”​—Soma Matayo 24:3, 7-14, 21, 22.

Kwa miaka elfu moja, Yesu atatawala dunia na iko mbinguni. Wakati huo atamaliza mateso yote. (Isaya 9:6, 7; 11:9) Yesu hatakuwa Mufalme tu, atakuwa pia Kuhani Mukubwa, na ataondoa zambi za wale wenye kumupenda Mungu. Kwa hiyo, Mungu atamutumia Yesu ili kumaliza magonjwa, uzee, na kifo.​—Soma Isaya 25:8; 33:24.

5. Ni nani wataishi mu Paradiso yenye itakuja?

Ku Jumba la Ufalme, utakutana na watu wenye wanamupenda Mungu na wenye wanapenda kujua namna ya kumufurahisha

Watu wenye kumutii ao kumusikia Mungu njo wataishi mu Paradiso. (1 Yohana 2:17) Yesu alituma wanafunzi wake ili watafute watu wapole na wawafundishe mambo yenye wanapaswa kufanya ili Mungu awakubali. Leo, Yehova iko anatayarisha mamilioni ya watu ili waishi mu Paradiso ku dunia wakati wenye kuja. (Sefania 2:3) Ku Majumba ya Ufalme ya Mashahidi wa Yehova, watu wanajifunza namna ya kuwa bwana na bibi wazuri na pia namna ya kuwa wazazi wazuri. Watoto na wazazi wanamuabudu Yehova pamoja na wanajifunza namna habari njema inaweza kuwaletea faida.​—Soma Mika 4:1-4.