Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

SEHEMU YA 4

Jinsi ya Kupanga Matumizi ya Pesa

Jinsi ya Kupanga Matumizi ya Pesa

“Kwa shauri mipango yenyewe hufanywa imara.”​—Methali 20:18

Sisi sote tunahitaji pesa ili kuandalia familia zetu mahitaji yao. (Methali 30:8) Ni kweli kwamba “pesa ni ulinzi.” (Mhubiri 7:12) Mkiwa wenzi wa ndoa, huenda ikawa vigumu kwenu kuzungumzia mambo ya pesa, lakini msiruhusu pesa zivuruge ndoa yenu. (Waefeso 4:32) Mume na mke wanapaswa kuaminiana na kushirikiana wanapopanga matumizi ya pesa.

1 PANGENI KWA MAKINI

BIBLIA INASEMA HIVI: “Ni nani kati yenu anayetaka kujenga mnara ambaye haketi kwanza na kuhesabu gharama, ili aone kama ana kiasi cha kutosha kuukamilisha?” (Luka 14:28) Ni muhimu kwenu kupanga pamoja jinsi ya kutumia pesa zenu. (Amosi 3:3) Amueni vitu mnavyohitaji na kiasi mnachoweza kutumia. (Methali 31:16) Kama mna pesa za kununua kitu fulani, hilo halimaanishi kwamba lazima mkinunue. Jitahidini kuepuka madeni. Tumieni tu pesa mlizo nazo.​—Methali 21:5; 22:7.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Kama pesa fulani zinabaki mwisho wa mwezi, amueni mtakavyozitumia

  • Kama kuna upungufu, fanyeni mipango ya kupunguza matumizi. Kwa mfano, mnaweza kula nyumbani badala ya kula mikahawani

2 ZUNGUMZIENI MAMBO HUSUSA WAZIWAZI

BIBLIA INASEMA HIVI: “Tunafanya mpango wa unyoofu, si machoni pa Yehova tu, bali pia machoni pa wanadamu.” (2 Wakorintho 8:21) Uwe mnyoofu unapomwambia mwenzi wako kuhusu pesa unazopata na kiasi unachotumia.

Sikuzote shauriana na mwenzi wako unapofanya maamuzi makubwa kuhusu pesa. (Methali 13:10) Kuzungumza kuhusu pesa kutasaidia kudumisha amani katika ndoa yenu. Ona mapato yako, si kama pesa zako, bali kama pesa za familia.​—1 Timotheo 5:8.

UNACHOWEZA KUFANYA:

  • Kubalianeni kuhusu kiasi ambacho kila mmoja anaweza kutumia bila kumjulisha mwenzake

  • Msingoje mpaka tatizo litokee ili mzungumze kuhusu pesa