Methali 21:1-31

  • Yehova huuelekeza moyo wa mfalme (1)

  • Haki ni bora kuliko dhabihu (3)

  • Bidii huleta mafanikio (5)

  • Asiyemsikiliza mtu wa hali ya chini hatasikilizwa (13)

  • Hakuna hekima katika kumpinga Yehova (30)

21  Moyo wa mfalme ni kama vijito vya maji mkononi mwa Yehova.+ Yeye huuelekeza mahali popote anapopenda.+   Njia zote za mwanadamu huonekana kuwa sawa machoni pake,+Lakini Yehova huichunguza mioyo.*+   Kutenda mambo manyoofu na ya hakiHumpendeza Yehova zaidi kuliko dhabihu.+   Macho ya kiburi na moyo wenye majivuno—Taa inayowaongoza waovu ni dhambi.+   Mipango ya wenye bidii hakika huleta mafanikio,*+Lakini wote walio na haraka kwa hakika watakuwa maskini.+   Kupata hazina kwa ulimi unaosema uwongoNi kama ukungu unaotoweka, mtego unaoangamiza.*+   Ukatili wa waovu utawafagilia mbali,+Kwa maana wanakataa kutenda haki.   Njia ya mtu mwenye hatia imepinda,Lakini matendo ya mtu safi yamenyooka.+   Ni afadhali kuishi pembeni juu ya paaKuliko kuishi katika nyumba moja na mke mgomvi.*+ 10  Mtu mwovu hutamani maovu;+Hamtendei kwa fadhili jirani yake.+ 11  Mwenye dhihaka anapoadhibiwa, asiye na uzoefu hupata hekima zaidi,Na mtu mwenye hekima anapopata ufahamu, anapata ujuzi.*+ 12  Aliye Mwadilifu huichunguza nyumba ya mwovu;Huwapindua waovu na kuwaangamiza.+ 13  Yeyote anayeziba sikio lake asisikie kilio cha mtu wa hali ya chiniYeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+ 14  Zawadi ya siri hutuliza hasira,+Na rushwa iliyofichwa* hutuliza ghadhabu kali. 15  Mwadilifu hushangilia kutenda haki,+Lakini hilo ni jambo baya sana kwa watenda maovu. 16  Mtu anayetangatanga kutoka kwenye njia ya ufahamuAtapumzika katika kundi la wale waliokufa ambao hawana uwezo.+ 17  Anayependa raha* atakuwa maskini;+Anayependa divai na mafuta hatakuwa tajiri. 18  Mwovu ni fidia ya mwadilifu,Na mwenye hila atachukuliwa badala ya mnyoofu.+ 19  Ni afadhali kuishi nyikaniKuliko kuishi na mke mgomvi* anayekasirika haraka.+ 20  Hazina yenye thamani na mafuta hupatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+Lakini mtu mpumbavu atatumia vibaya* vitu alivyo navyo.+ 21  Yeyote anayefuatia uadilifu na upendo mshikamanifuAtapata uzima, uadilifu, na utukufu.+ 22  Mtu mwenye hekima anaweza kupanda katika* jiji la watu wenye nguvuNa kudhoofisha nguvu wanazotumaini.+ 23  Anayelinda kinywa chake na ulimi wakeAnajiepusha na taabu.+ 24  Mtu mwenye kimbelembele, anayejigamba kwa kiburi, hivyo ndivyo unavyomwitaMtu anayetenda kwa kimbelembele bila kujali.+ 25  Anachotamani mtu mvivu kitamuua,Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+ 26  Anatamani kwa pupa mchana kutwa,Lakini mwadilifu hutoa, hawanyimi wengine chochote.+ 27  Dhabihu ya mwovu inachukiza.+ Sembuse anapoitoa akiwa na nia ovu!* 28  Shahidi anayesema uwongo ataangamia,+Lakini mtu anayesikiliza atatoa ushahidi kwa mafanikio.* 29  Mtu mwovu huvaa uso wa ushupavu,+Lakini njia ya mtu mnyoofu ni hakika.*+ 30  Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.+ 31  Farasi hutayarishwa kwa ajili ya siku ya vita,+Lakini wokovu ni wa Yehova.+

Maelezo ya Chini

Au “huzichunguza nia.”
Au “manufaa.”
Au labda, “kwa wale wanaotafuta kifo.”
Au “msumbufu.”
Au “anajua la kufanya.”
Tnn., “iliyo kifuani.”
Au “anasa.”
Au “msumbufu.”
Tnn., “atavimeza.”
Au “kulishinda.”
Au “akiwa na mwenendo wa aibu!”
Tnn., “atazungumza milele.”
Au “mtu mnyoofu huifanya njia yake iwe hakika.”