Kwa Waefeso 4:1-32

  • Umoja katika mwili wa Kristo (1-16)

    • Zawadi katika wanadamu (8)

  • Utu wa zamani na utu mpya (17-32)

4  Kwa hiyo, mimi mfungwa+ katika Bwana, ninawasihi mtembee kwa kustahili+ mwito mliopokea,  kwa unyenyekevu*+ wote na upole, kwa subira,+ mkivumiliana kwa upendo,+  mkijitahidi sana kudumisha roho ya umoja katika kifungo cha muungano cha amani.+  Kuna mwili mmoja,+ na roho moja,+ kama mlivyoitwa kwenye tumaini moja;+  Bwana mmoja,+ imani moja, ubatizo mmoja;  Mungu mmoja ambaye ni Baba wa wote, aliye juu ya wote, na kupitia wote na katika wote.  Basi kila mmoja wetu alionyeshwa fadhili zisizostahiliwa kulingana na jinsi Kristo alivyopima zawadi hiyo ya bure.+  Kwa maana inasema: “Alipopanda juu alichukua mateka; alitoa wanaume kuwa zawadi.”+  Basi neno “alipopanda,” linamaanisha nini? Linamaanisha kwamba pia alishuka chini, yaani, duniani. 10  Yule aliyeshuka ndiye pia aliyepanda+ juu zaidi ya mbingu zote,+ ili atimize mambo yote. 11  Naye alitoa wengine wawe mitume,+ wengine manabii,+ wengine waeneza injili,*+ wengine wachungaji na walimu,+ 12  ili kuwarekebisha* watakatifu, kwa ajili ya kutimiza huduma, na kuujenga mwili wa Kristo,+ 13  mpaka sote tuwe na umoja* katika imani na tuwe na ujuzi sahihi kumhusu Mwana wa Mungu, na kuwa mtu aliyekomaa kabisa,+ na kufikia kiwango cha kimo kamili cha Kristo. 14  Basi tusiwe tena watoto, tukirushwa huku na huku kama kwa mawimbi na kupeperushwa na kila upepo wa fundisho+ kwa udanganyifu wa watu, kupitia ujanja na njia za hila. 15  Lakini tukisema ukweli, kupitia upendo na tuendelee kukua katika mambo yote ndani ya Kristo, ambaye ni kichwa.+ 16  Kupitia kwake mwili wote+ unaunganishwa na kushirikiana kila kiungo kinapofanya kazi yake. Na kila kiungo kinapofanya kazi vizuri, hilo linafanya mwili ukue na kujijenga katika upendo.+ 17  Basi ninasema na kushuhudia katika Bwana, kwamba msiishi tena kama watu wa mataifa wanavyoishi,+ katika ubatili wa akili zao.+ 18  Wako gizani kiakili na wametenganishwa na uzima ambao ni wa Mungu, kwa sababu ya ujinga ulio ndani yao na kwa sababu ya ugumu wa* mioyo yao. 19  Kwa kuwa wamepotoka kabisa kimaadili, wamejiingiza katika mwenendo mpotovu*+ na kufanya mambo machafu ya kila namna kwa pupa. 20  Lakini ninyi hamkujifunza kwamba Kristo yuko hivyo, 21  ikiwa kwa kweli mlimsikia na kufundishwa kupitia kwake, kama vile kweli ilivyo katika Yesu. 22  Mlifundishwa kuvua utu wa zamani+ unaopatana na mwenendo wenu wa zamani na ambao unaharibiwa na tamaa zake za udanganyifu.+ 23  Na mnapaswa kuendelea kufanywa upya katika nguvu zinazoongoza akili zenu,*+ 24  na mnapaswa kuvaa utu mpya+ ulioumbwa kupatana na mapenzi ya Mungu katika uadilifu wa kweli na ushikamanifu. 25  Kwa hiyo, kwa sababu mmeacha udanganyifu, semeni ukweli kila mmoja na mwenzake,+ kwa sababu sisi ni viungo vya mwili mmoja.+ 26  Iweni na hasira, lakini msitende dhambi;+ jua lisitue mkiwa bado mmekasirika;+ 27  msimpe Ibilisi nafasi.+ 28  Mwizi asiibe tena; badala yake afanye kazi kwa bidii, akifanya kazi njema kwa mikono yake,+ ili awe na kitu cha kumgawia mtu mwenye uhitaji.+ 29  Neno lililooza lisitoke kinywani mwenu,+ bali neno jema kwa ajili ya kujenga kulingana na uhitaji, ili liwanufaishe wale wanaolisikia.+ 30  Pia, msiwe mkiihuzunisha roho takatifu ya Mungu,+ ambayo kupitia hiyo mmetiwa muhuri+ kwa ajili ya siku ambayo mtawekwa huru kupitia fidia.+ 31  Acheni kabisa kila aina ya chuki yenye uhasama,+ hasira, ghadhabu, kufoka, matusi,+ na mambo yote yanayodhuru.+ 32  Bali mtendeane kwa fadhili, huruma nyororo,+ mkisameheana kwa hiari kama vile Mungu alivyowasamehe ninyi kwa hiari kupitia Kristo.+

Maelezo ya Chini

Au “unyenyekevu wa akili.”
Au “wahubiri wa habari njema.”
Au “kuwazoeza.”
Au “muungano.”
Tnn., “kukosa hisia katika.”
Au “ufidhuli; matendo ya kuchukiza yanayofanywa bila aibu.” Kigiriki, a·selʹgei·a. Angalia Kamusi.
Au “nguvu zinazotawala akili zenu.” Tnn., “roho ya akili yenu.”