Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Hekima Yenye Inaweza Kutuletea Furaha mu Familia

Hekima Yenye Inaweza Kutuletea Furaha mu Familia

Ndoa na watoto ni zawadi ya muzuri sana yenye Muumbaji wetu anatupatia. Anapenda tukuwe na furaha mu familia yetu. Kwa hiyo, kupitia kitabu moja ya zamani, yenye kuwa takatifu, anatupatia muongozo yenye inaweza kufanya familia yetu ikuwe na furaha zaidi. Fikiria hii mashauri ya hekima yenye anatutolea.

Bwana, Muwapende Bibi Zenu

“Bwana wanapaswa kupenda bibi zao kama miili yao wenyewe. Mwanaume mwenye anamupenda bibi yake anajipenda yeye mwenyewe, kwa maana hakuna mutu mwenye anachukia mwili wake, lakini anaukulisha na kuutunza kwa upendo.”​—WAEFESO 5:28, 29.

Bwana, njo kichwa ya familia. (Waefeso 5:23) Lakini bwana muzuri, hakuwake mukali na hakuwake mwenye kuwekea-wekea watu masheria. Anamuonaka bibi yake kuwa wa maana, anahangaikiaka mahitaji yake ya kimwili na anahangaikiaka pia namna bibi yake iko najisikia. Tena, anajikazaka sana juu amufurahishe, na hapendake bibi yake afanye tu mambo yenye yeye anapenda. (Wafilipi 2:4) Anamuambiaka bibi yake wazi-wazi mawazo yake, na namna iko najisikia. Na pia, anasikilizaka wakati bibi yake iko anasema. ‘Hamukasirikiake bibi yake kwa uchungu’ ao kumutendea mubaya kimwili. Hazungumuzake naye kwa ukali na hamusemake mubaya.​—Wakolosai 3:19.

Bibi, Muheshimie Bwana Zenu

“Bibi anapaswa kumuheshimia sana bwana yake.”​—WAEFESO 5:33.

Wakati bibi anamuheshimia bwana yake na anaunga mukono maamuzi yenye bwana yake anakamata, anasaidia mu familia mukuwe amani zaidi. Wakati bwana anakosea, bibi muzuri hatamuzarau bwana yake, lakini ataendelea kuwa mupole na kuendelea kumuheshimia. (1 Petro 3:4) Wakati bibi anataka kuongea na bwana yake juu ya jambo fulani, atatafuta wakati ya muzuri juu ya kufanya vile na atazungumuza naye kwa heshima.​—Muhubiri 3:7.

Ukuwe Muaminifu kwa Bibi ao Bwana Yako

“Mwanaume . . . atashikamana na bibi yake, nao watakuwa mwili mumoja.”​—MWANZO 2:24.

Wakati bibi na bwana wanaoana, wanakuwa na uhusiano wa karibu sana. Kwa hiyo, bibi na bwana wanapaswa kufanya yao yote juu ya kufanya ndoa yao ikuwe nguvu. Na watafanya vile, kama mu mazungumuzo yao, wanaambianaka mambo yote yenye iko mu moyo na ikiwa wanazoea kutendeana mambo ya kidogo-kidogo ya muzuri. Tena, kila mumoja anapaswa kuwa muaminifu kwa mwenzake kwa kuepuka kufanya ngono inje ya ndoa. Kama bibi ao bwana anakosa uaminifu, mwenzake ataumia sana. Anaweza kukosa kumuaminia, na ndoa inaweza hata kufikia kuvunjika.​—Waebrania 13:4.

Wazazi, Muzoeze Watoto Wenu

“Zoeza mutoto katika njia yenye anapaswa kufuata; hata wakati atazeeka hataiacha.”​—MEZALI 22:6, maelezo ya chini.

Mungu amepatia wazazi daraka ya kuzoeza watoto wao. Ni kusema, wazazi wanapaswa kuwafundisha namna ya kujiendesha, na wanapaswa kuwawekea mufano muzuri. (Kumbukumbu la Torati 6:6, 7) Wakati mutoto anajiendesha mubaya, wazazi wenye hekima hawatamutendea kwa ukali. Baba ao mama mwenye hekima, anakuwaka “mwepesi wa kusikiliza, hapana mwepesi wa kusema, hapana mwepesi wa kukasirika.” (Yakobo 1:19) Ikiwa muzazi anaona kama anapaswa kumupatia mutoto wake malipizi, anapaswa kufanya vile mu njia yenye kuonyesha mutoto wake kama anamupenda. Lakini, hapaswe kufanya vile wakati iko mwenye kukasirika.

Watoto, Mutii Wazazi Wenu

“Watoto, mutii wazazi wenu . . . ‘Heshimia baba yako na mama yako.’”​—WAEFESO 6:1, 2.

Watoto wanapaswa kutii wazazi wao na wanapaswa kuwaheshimia sana. Wakati watoto wanatii wazazi wao, mu nyumba munakuwa amani. Watoto wenye kukomala, wanaheshimia wazazi wao kwa kuwachunga muzuri. Ni kusema, wanapaswa kuhakikisha kama wazazi wao wako na nyumba ya muzuri na kama wako na kila kitu yenye wako nayo lazima ili kuishi.​—1 Timoteo 5:3, 4.