Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | NDOA

Namna ya Kuonyesha Heshima

Namna ya Kuonyesha Heshima

MAGUMU

Bwana anasema hivi: “Wakati tulioana, mimi na bibi yangu tulikuwa na mawazo tofauti juu ya maana ya kuonyesha heshima. Mawazo yetu yalikuwa tu tofauti; hakukuwa ya muzuri na ya mubaya. Mara nyingi niliona kama bibi yangu alipaswa kuonyesha heshima zaidi wakati alikuwa anazungumuza na mimi.”

Bibi anasema hivi: “Mahali nilikomalia watu walizoea kusema kwa sauti ya juu, kutumia ishara nyingi za uso, na kukatiza wengine wakati wanazungumuza. Hatukuona kama kufanya vile ni kukosa heshima. Lakini bwana yangu alikomalia katika mahali tofauti kabisa.”

Heshima katika ndoa haiko jambo lenye unaweza kuonyesha wakati fulani; ni jambo la lazima. Namna gani unaweza kuonyesha kama unaheshimia bibi ao bwana yako?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Wanaume wako na lazima ya pekee ya kuheshimiwa. Biblia inaambia hivi wanaume wenye kuoa: ‘Kila mutu mumoja-mumoja kati yenu na amupende hivyo muke [ao, bibi] wake kama vile anajipenda mwenyewe.’ Lakini inaongezea hivi: ‘Muke anapaswa kumuheshimu sana mume [ao, bwana] wake.’ (Waefeso 5:33) Hata kama bibi na bwana wote wako na lazima ya kujisikia kwamba wanapendwa na kuheshimiwa, mara nyingi bwana wanataka kuheshimiwa sana. Bwana mumoja mwenye kuitwa Carlos, * anasema hivi: “Wanaume wanapenda kujisikia kwamba wako na uwezo wa kushugulikia hali mbalimbali, wa kumaliza matatizo, na wa kuhangaikia familia yao.” Wakati bibi anaheshimia uwezo wa bwana yake katika mambo kama hayo, wote wawili wanapata faida. Bibi mumoja mwenye kuitwa Corrine, anasema hivi: “Bwana yangu ananionyesha upendo zaidi wakati ninamuheshimia.”

Bibi pia wako na lazima ya kuheshimiwa. Hiyo ni kweli kwa sababu bwana hawezi kupenda kabisa bibi mwenye haheshimie. Daniel anasema hivi: “Ninapaswa kuheshimia mawazo ya bibi yangu. Ninapaswa pia kuheshimia namna anajisikia. Hata kama sielewe sababu gani anajisikia vile, hilo halimaanishe kwamba siwezi kuhangaikia namna anajisikia.”

Kila mutu iko na mawazo yake juu ya heshima. Tatizo haiko kuwaza kama unaonyesha heshima, lakini ni ikiwa bibi ao bwana yako anaona kama unamuheshimia. Bibi mwenye tumetaja katika mwanzo wa habari hii chini ya kichwa “Magumu,” alijifunza jambo hilo. Anasema hivi: “Hata ikiwa sikuona kama nilikuwa ninakosa heshima, lakini ikiwa bwana yangu aliona kama ninakosa heshima, ni mimi nilipaswa kubadilika.”

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

  • Andika mambo tatu yenye unafurahia juu ya bibi ao bwana yako. Mambo hayo yenye unafurahia ndiyo yanaweza kukuchochea kuonyesha heshima.

  • Kwa juma moja, chunguza mwenendo wako (hapana wa bibi ao bwana yako) katika mambo yenye kufuata.

Maneno yako. Kulingana na uchunguzi moja wenye ulifanywa juu ya ndoa nyingi, “wakati walizungumuzia matatizo yao, bibi na bwana katika ndoa zenye furaha na zenye kuwa nguvu walisema maneno tano ya kujenga kwa ajili ya kila neno moja la kuumiza. Lakini, bibi na bwana wenye ndoa zao zilikaribia kuvunjika walisema chini ya neno moja (0.8) la kujenga kwa ajili ya kila neno moja la kuumiza.” *​—Kanuni ya Biblia: Methali 12:18.

Ujiulize hivi: ‘Ninazungumuza kwa heshima na bibi ao bwana yangu? Ni mara ngapi ninamuhukumu nikilinganisha na mara yenye ninamupongeza? Ninatumia sauti ya namna gani wakati ninazungumuza juu ya jambo fulani lenye niliona ao lenye halinifurahishe?’ Bibi ao bwana yako atakubali kama majibu yako ni ya kweli?​—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:13.

Jaribu kufanya hivi: Ujiwekee muradi wa kupongeza bibi ao bwana yako hata mara moja kwa siku. Pendekezo: Angalia tena mambo yenye kukufurahisha yenye uliandika juu yake. Uzoee kuambia bibi ao bwana yako mambo yenye unafurahia kwake.​—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 8:1.

Matendo yako. Bibi mwenye kuitwa Alicia, anasema hivi: “Ninatumia wakati mwingi ili kufanya kazi za nyumbani, na wakati bwana yangu anaheshimia kazi yenye nilifanya kwa kuweka muzuri vitu vyake, na kwa kusafisha masahani, ninajisikia kama sikufanya kazi ya bure, na ninajisikia kuwa wa maana katika ndoa yetu.”

Ujiulize hivi: ‘Namna ninatendea bibi ao bwana yangu inaonyesha wazi kama ninamuheshimia? Ninajikaza kumuhangaikia na kupitisha wakati pamoja naye?’ Bibi ao bwana yako atakubali kama majibu yako ni ya kweli?

Jaribu kufanya hivi: Andika namna tatu zenye ungependa bibi ao bwana yako akuonyeshe heshima. Ambia bibi ao bwana yako afanye hivyo pia. Kisha, kila mumoja wenu apatie mwenzake liste yenye ameandika ili kila mumoja ajikaze kuonyesha heshima katika mambo yenye mwenzake ameandika. Kila mumoja akazie namna yeye mwenyewe anaweza kuonyesha heshima. Wakati mumoja anakuwa wa kwanza kufanya hivyo, mwengine anaweza kumuiga.

^ fu. 8 Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.

^ fu. 14 Kutoka katika kitabu Ten Lessons to Transform Your Marriage.