Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawafanyake Sikukuu Fulani?

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawafanyake Sikukuu Fulani?

 Nini njo inasaidiaka Mashahidi wa Yehova kuamua kama watasherehekea sikukuu fulani ao hapana?

 Mashahidi wa Yehova wanachunguzaka kwanza Biblia juu ya kujua kama watafanya sikukuu fulani ao hapana. Sikukuu fulani zinapingana kabisa na mambo yenye Biblia inafundisha. Mashahidi fulani hawafanyake sikukuu za vile. Lakini kuhusu sikukuu zingine, kila Shahidi wa Yehova anaamuaka ikiwa atazifanya ao hapana, na anajikazaka “kuendelea kuwa na zamiri safi mbele ya Mungu na wanadamu.”​—Matendo 24:16.

 Hii njo maulizo yenye Mashahidi wa Yehova wanajiulizaka juu wajue ikiwa watafanya sikukuu fulani ao hapana. a

  •   Hii sikukuu inatokana na fundisho yenye haipatane na maandiko?

     Kanuni ya Biblia: “‘Mutoke katikati yao na mujitenge,’ ni vile Yehova anasema, ‘na muache kugusa kitu kichafu.’”​—2 Wakorinto 6:15-​17.

     Juu ya kujitenga kabisa na mafundisho yenye haiko safi kiroho, ni kusema mafundisho yenye haipatane na Biblia, Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye kutokana na mambo yenye kufuata:

     Sikukuu zenye zinatokana na ibada ya miungu ingine. Yesu alisema: “Yehova Mungu wako ndiye unapaswa kuabudu, na yeye peke yake ndiye unapaswa kutolea utumishi mutakatifu.” (Matayo 4:10) Juu Mashahidi wa Yehova wanatii ile maneno, hawafanyake Noeli, Pasaka, ao May Day, juu zile sikukuu zinatokana na ibada ya miungu ingine, hapana ibada ya Yehova. Tena, hawafanyake sikukuu zenye kufuata:

    •  Kwanzaa. Jina Kwanzaa “inatokana na maneno ya Kiswahili matunda ya kwanza. Ile inatokana na sherehe za kwanza za mavuno mu historia ya Afrika.” (Encyclopedia of Black Studies) Hata kama watu wengi wanaonaka kuwa Kwanzaa haiko sikukuu ya kidini, Encyclopedia of African Religion inailinganisha na sherehe ya Afrika, yenye wakati ilikuwa inafanywa, matunda ya kwanza “ilikuwa inatolewa kwa mungu na kwa wazazi wa zamani, juu ya kuwashukuru.” Inaongezea hivi: “Ni ileile roho ya kuonyesha shukrani na kuonyesha kama wanafurahia uzima wenye wazazi wao wa zamani waliwapatia njo ilichochea Waamerika wenye walitoka Afrika waanzishe sikukuu ya Kwanzaa.”

      Kwanzaa

    •  Sikukuu ya Katikati ya Kipindi ya Mvua ya Kwanza. Ile “sikukuu inafanywa juu ya kutukuza mungu mwanamuke mwezi.” (Holidays, Festivals, and Celebrations of the World Dictionary) Wakati wa ile sikukuu “wanamuke wanainamaka mbele ya ule mungu mwanamuke. Mu Kichina ile desturi inaitwa a kowtow.”​—Religions of the World​—A Comprehensive Encyclopedia of Beliefs and Practices.

    •  Nauruz (Nowruz). “Ile sikukuu inatokana na dini ya Wazoroastre, na ni moya kati ya siku takatifu zaidi katika kalendari ya Wazoroastre. . . . Kulingana na desturi ya Wazoroastre, wakati wa sikukuu ya Nowruz, saa midi ilikuwa inafika, watu walikuwa wanafanya sherehe juu ya kusherehekea kurudia kwa Roho ya Midi, yenye inaitwa pia [Rapithwin]. Waliamini kama roho ya kipindi cha baridi ilikuwa inafungia roho ya midi chini ya udongo wakati wa miezi ya baridi.”​—United Nations Educational, Scientific and Cultural Organization.

    •  Shab-e Yalda. Ile sikukuu inafanywa mu Mwezi wa 12 wakati muchana ni mufupi kuliko usiku. Kitabu Sufism in the Secret History of Persia inaonyesha kama ile sikukuu inatokana na ibada ya Mithra, ni kusema, mungu wa mwangaza. Wengine wanawaza kama ile sikukuu inatokana na ibada ya mungu jua wa Waroma na wa Wagiriki. b

    •  Sikukuu ya Kutoa Shukrani. Kama vile sikukuu ya Kwanzaa, ile sikukuu inatokana na sherehe za zamani za mavuno zenye zilikuwa zinafanywa juu ya kutukuza miungu mbalimbali. Kisha wakati kupita, “viongozi wa kanisa ya Kikristo walikubali zile sherehe na watu wakaanza kuzifanya.”​—A Great and Godly Adventure​—The Pilgrims and the Myth of the First Thanksgiving.

     Sikukuu zenye zinatokana na ushirikina ao kuamini bahati. Biblia inasema kama wale wenye “kupanga meza kwa ajili ya mungu wa Bahati Njema” wako “kati ya wale wenye kumuacha Yehova.” (Isaya 65:11) Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye kufuata:

    •  Ivan Kupala. “Kitabu The A to Z of Belarus kinasema kama watu wengi wanaamini kama siku ya [Ivan Kupala,] ulimwengu unatoaka nguvu zake za uchawi, na kama uko na uhodari na uko na bahati, unaweza kupata sehemu ya ile nguvu.” Ku mwanzo, ile sikukuu ilikuwa ya kipagani, yenye ilikuwa inafanywa juu ya kusheherekea kipindi ya mwaka yenye muchana inakuwaka murefu sana kuliko usiku. Lakini sawa vile Encyclopedia of Contemporary Russian Culture inaonyesha, ile sikukuu ilichanganywa na sikukuu ya Kanisa [“sikukuu ya mutakatifu” Yohana Mubatizaji] kisha wapagani kukubali Ukristo.”

    •  Sikukuu ya Mwaka Mupya ya Wachina ao Sikukuu ya Mwaka Mupya ya Wakorea. “Mu ile kipindi ya mwaka, watu wa familia, marafiki na watu wa jamaa wanajitafutiaka baraka, wanatukuzaka miungu na roho, na kutakiana mambo ya muzuri kwa ajili ya mwaka mupya.” (Mooncakes and Hungry Ghosts​—Festivals of China) Vilevile, wakati wa sikukuu ya mwaka mupya ya Wakorea, watu wanafanyaka ibada ya wazazi wa zamani, wanafanyaka desturi mbalimbali juu ya kufukuza roho wabaya, na juu wapate baraka mu mwaka mupya. Na wanatafutaka alama za kuwasaidia kujua mambo yenye itatokea mu ile mwaka mupya.”​—Encyclopedia of New Year’s Holidays Worldwide.

      Sikukuu ya Mwaka Mupya ya Wachina

     Sikukuu zenye zinatokana na fundisho yenye kuonyesha kama nafsi haikufake. Biblia inaonyesha wazi kama nafsi inaweza kufa. (Ezekieli 18:4) Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye kufuata, zenye zinaunga mukono fundisho yenye kuonyesha kama nafsi haikufake:

    •  Sikukuu ya Wafu. Kitabu New Catholic Encyclopedia inaonyesha kama ile sikukuu inafanywa juu ya “kukumbuka waaminifu wote wenye walishakakufa.” Kuanzia mwaka wa 500 hivi, kisha kuzaliwa kwa Yesu, mupaka mwaka wa 1500 hivi, kisha kuzaliwa kwa Yesu, watu wengi waliamini kama roho zenye kuwa mu pirgatori zingeweza kujigeuza kuwa mizimu, wachawi, chura, na mambo ingine, na kutokea watu wenye walizitendeaka mubaya wakati zilikuwa zingali naishi.”

    •  Sikukuu ya Qingming (Ch’ing Ming) na Sikukuu ya Mizimu Yenye Kuwa na Njala. Zile sikukuu mbili zinafanywa juu ya kutukuza wazazi wa zamani. Kitabu Celebrating Life Customs Around the World​—From Baby Showers to Funerals inasema kama wakati wa Sikukuu ya Ch’ing Ming, watu wanalunguzaka “chakula, vinywaji, na makuta, juu wafu wasisikie njala ao kiu na wasikose makuta.” Ile kitabu inasema pia kama “Wakati wa Sikukuu ya Mizimu Yenye Kuwa na Njala, zaidi sana wakati wa usiku wenye mwezi uko wenye kuenea, watu wanaamini kama ule usiku kunakuwaka uhusiano mukubwa sana kati ya wafu na wazima kuliko usiku mwingine wowote. Njo maana ni jambo ya maana sana kutuliza wafu na kuonyesha wazazi wa zamani heshima.”

    •  Chuseok. Kitabu The Korean Tradition of Religion, Society, and Ethics, kinasema kama “wakati wa ile sikukuu watu wanatoleaka nafsi za wafu chakula na divai.” Wanafanyaka ile matoleo juu “wanaamini kama nafsi inaendeleaka kuishi kisha mwili kufa.”

     Sikukuu zenye kutokana na uchawi. Biblia inasema hivi: “Mutu yeyote mwenye kufanya uaguzi, mutu yeyote mwenye kufanya uchawi, mutu yeyote mwenye kutafuta alama za mambo yenye yatatokea, mulozi, mutu yeyote mwenye anafunga wengine kwa uchawi, mutu yeyote mwenye anatafuta shauri kwa mutu mwenye kupashana habari na pepo wachafu ao mutu mwenye kutabiri matukio, ao mutu yeyote mwenye kuuliza habari kwa wafu . . . ni chukizo kwa Yehova.” (Kumbukumbu la Torati 18:10-​12) Juu ya kuepuka aina yoyote ya uchawi, kama vile kutafuta alama za nyota, Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu ya Halloween ao sikukuu zenye kufuata:

    •  Mwaka Mupya wa Sinhala na Tamil. “Wakati wa zile sikukuu, watu wanafanyaka mambo mbalimbali ku saa fulani zenye zimechaguliwa, . . . zenye watu wenye kusoma alama za nyota wameonyesha kama zitaleta baraka.”​—Encyclopedia of Sri Lanka.

    •  Songkran. Jina ya Kiasia ya ile sikukuu “inatokana na neno ya Kisanskriti . . . yenye kumaanisha ‘mwendo’ ao ‘badiliko.’ Wanafanyaka ile [sikukuu] juu ya kusherehekea kupita kwa jua mu kikundi cha nyota cha zodiaki chenye kuitwa kondoo-dume.”​—Food, Feasts, and Faith​—An Encyclopedia of Food Culture in World Religions.

     Sikukuu zenye zinatokana na ibada yenye ilikuwa inafanywa wakati wa Sheria ya Musa, Sheria yenye ilifikia mwisho wakati Yesu alitoa zabihu yake. Biblia inasema hivi: “Kristo ndiye mwisho wa Sheria.” (Waroma 10:4) Wakristo wanapataka faida wakati wanatumikisha kanuni zenye zinatokana na Sheria ya Musa yenye Mungu alipatia Waisraeli wa zamani. Lakini hawafanyake sikukuu zenye ile Sheria iliomba Waisraeli wafanye, zaidi sana sikukuu zenye zilikuwa zinatayarisha watu kuya kwa Masiya juu Wakristo wanaamini kama Masiya alishakakuya. Biblia inasema hivi: “Mambo hayo ni kivuli cha mambo yenye yatakuja, lakini ukweli wa mambo ni wa Kristo.” (Wakolosai 2:17) Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake zile sikukuu, na tena juu watu wameingiza desturi zenye hazipatane na Maandiko mu sikukuu fulani, Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye kufuata:

    •  Hanukkah. Ni sikukuu ya kukumbuka wakati hekalu ya Wayahudi katika Yerusalemu ilitolewa tena kwa Mungu mara ya pili. Lakini Biblia inafundisha kama Yesu alifanywa kuwa Kuhani Mukubwa wa “hema [hekalu] kubwa na kamilifu zaidi yenye haikutengenezwa kwa mikono, ni kusema, hapana ya uumbaji huu.” (Waebrania 9:11) Wakristo wanaamini kama hekalu ya kiroho ilikamata nafasi ya hekalu ya Yerusalemu.

    •  Rosh Hashanah. Ni siku ya kwanza ya mwaka wa Wayahudi. Zamani, watu walikuwa natolea Mungu zawadi za pekee wakati wa ile sikukuu. (Hesabu 29:1-6) Lakini wakati Yesu Kristo alikuya na kuwa Masiya, alimaliza “mambo ya zabihu na toleo la zawadi,” na kwa hiyo Mungu hakuziona tena kuwa za maana.​—Danieli 9:26, 27.

  •   Ni sikukuu yenye inafanya watu wachangie imani?

     Kanuni ya Biblia: “Ao muamini iko na ushirika gani na mutu mwenye haiko muamini? Na hekalu la Mungu liko na makubaliano gani na sanamu?”​—2 Wakorinto 6:15-​17.

     Mashahidi wa Yehova wanajikazaka kuishi kwa amani na majirani wao, na wanaheshimia haki ya kila mutu ya kujichagulia dini. Lakini wanaepuka sikukuu zenye zinachochea watu wachangie imani mu njia zenye kufuata:

     Sikukuu zenye zinafanywa juu ya kuheshimia mutu fulani wa dini ao zenye zinachochea watu wa dini mbalimbali wafanye ibada pamoya. Zamani wakati Mungu aliingiza Waisraeli mu inchi ya mupya kwenye watu walikuwa mu dini zingine, aliwaambia hivi: “Haupaswe kufanya agano pamoja nao wala pamoja na miungu yao. . . . Kama unatumikia miungu yao, hakika jambo hilo litakuwa mutego kwako.” (Kutoka 23:32, 33) Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye kufuata:

    •  Loy Krathong. Ni sikukuu yenye inafanywa mu inchi ya Tailandi. Wakati wa ile sikukuu “watu wanatengenezaka mabakuli kwa kutumia majani, wanatiaka ndani mishumaa ao miti ya uvumba na kutia ile mabakuli juu ya maji. Wanaamini kama ile mabakuli inapelekaka mbali bahati mubaya. Lakini kusema kweli ile sikukuu ni ya kumutukuza Buda.”​—Encyclopedia of Buddhism.

    •  Sikukuu ya Kutubu. Gazeti The National ya Papousie Nouvelle Guinée inazungumuzia maneno ya mukubwa fulani wa serikali mwenye alisema kama wale wenye wanafanya ile sikukuu “wanakubaliana na mawazo ya musingi ya Kikristo. Alisema pia kama ile sikukuu inasaidia “kueneza kanuni za Kikristo mu inchi.”

    •  Vesak. “Njo siku takatifu zaidi ya Wabuda. Njo siku yenye wanakumbukaka kuzaliwa kwa Buda, namna alitoaka ufunuo mbalimbali, kifo yake ao namna alifika Nirvana.”​—Holidays, Festivals, and Celebrations of the World Dictionary.

      Vesak

     Sikukuu zenye zinategemea desturi za kidini zenye hazipatane na Maandiko. Yesu aliambia hivi viongozi wa dini: “Mumefanya neno la Mungu kuwa kitu cha bure kwa sababu ya desturi yenu.” Alisema pia kama ibada yao ilikuwa ya bure juu walifundisha “amri za wanadamu kuwa desturi.” (Matayo 15:6, 9) Mashahidi wa Yehova wanakamata kwa uzito ile maneno ya Yesu, njo maana kuko sikukuu za mingi za kidini zenye hawafanyake.

    •  Epiphanie (Sikukuu ya Wafalme Tatu, ao Timkat, ao Los Reyes Magos). Ni siku ya kukumbuka wakati yenye watu wenye elimu ya nyota waliendaka kutembelea Yesu, ao kukumbuka ubatizo wa Yesu. “Inafanya sherehe fulani za wapagani za kipindi cha mvua ya mwisho zionekane kuwa za Kikristo. Zile sherehe ziko na kusudi ya kutukuza miungu ya maji ya chemchemi, mito mikubwa, na mito ya kidogo-kidogo.” (The Christmas Encyclopedia) Timkat, sikukuu yenye kufanana na Epiphanie inatokana na desturi za zamani sana.​—Encyclopedia of Society and Culture in the Ancient World.

    •  Sikukuu ya kupanda kwa bikira Maria mbinguni. Watu wenye wanaifanyaka wanaamini kama Maria, mama ya Yesu, alipandaka mbinguni na mwili wake wa damu na nyama. Kitabu Religion and Society​—Encyclopedia of Fundamentalism, inasema kama “ile mawazo haikukuwa najulikana mu kanisa ya kwanza-kwanza na hakuna fasi kwenye Maandiko inaizungumuzia.”

    •  Sikukuu ya kutungwa mimba bila zambi. “Biblia haifundishe kama Maria hakukuwa na zambi tangu mama yake achukue mimba yake . . . [ile] ni fundisho yenye Kanisa ilianzisha.”​—New Catholic Encyclopedia.

    •  Kareme. Ni kipindi ya kutubu na kufanya mafungo. Kitabu New Catholic Encyclopedia inaonyesha kama ile sikukuu ilianzishwa “mu karne ya ine,” ni kusema zaidi ya miaka 200 kisha kazi ya kuandika Biblia kumalizika. Ileile kitabu inasema hivi kuhusu siku ya kwanza ya kareme: “Zoea ya kupakala waaminifu majivu kwenye siku ya tatu ya majivu ilianza kufanywa mu dunia yote tangu mukutano wa Benevento wenye ulifanywa mu mwaka wa 1091.”

    •  Meskel (ao, Maskal). Ni sikukuu yenye inafanywa Etiopia. Kitabu Encyclopedia of Society and Culture in the Medieval World (alama ya mabano ni ya muandikaji) kinasema kama “ile sikukuu ni ya kusherehekea kupatanikana kwa Musalaba wa Kwelikweli (musalaba wenye Yesu alisulubiwa ao alitundikwa juu yake). Watu wanafanyaka ile sikukuu kwa kuwasha moto na kucheza dansi kuzunguka ile moto.” Lakini, Mashahidi wa Yehova hawatumiake musalaba mu ibada yao.

  •   Ile sikukuu inatukuza mwanadamu, tengenezo fulani, ao alama ya taifa?

     Kanuni ya Biblia: “Yehova anasema hivi: ‘Amelaaniwa mutu mwenye anategemea wanadamu bure, mwenye anategemea nguvu za mwanadamu, na mwenye moyo wake unageuka na kumuacha Yehova.’”​—Yeremia 17:5.

     Mashahidi wa Yehova wanaheshimiaka wanadamu wenzao, na wanakuwaka hata wanasali kwa ajili yao. Lakini hawafanyake sikukuu zenye kufuata:

     Sikukuu ya kuheshimia mutawala fulani ao mutu mwingine mwenye kujulikana. Biblia inasema hivi: “Kwa ajili yenu wenyewe, muache kutumainia mwanadamu bure, mwenye ni pumuzi tu yenye kuwa katika matundu ya pua yake. Sababu gani afikiriwe?” (Isaya 2:22) Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu ya kuzaliwa kwa mutawala fulani.

     Sikukuu ya kutukuza bendera ya inchi. Mashahidi wa Yehova hawafanyake Sikukuu ya Kutukuza Bendera. Juu ya nini? Juu Biblia inasema hivi: “Watoto wadogo, mujiepushe na sanamu.” (1 Yohana 5:21) Watu fulani hawaamini kama bendera ni sanamu. Lakini mwanahistoria Carlton J. H. Hayes aliandika hivi: “Bendera njo alama yenye kuonyesha kama mutu anapenda sana inchi yake, na inaabudiwa na watu wengi.”

     Sikukuu zenye zinatukuza mutakatifu fulani. Mutume Petro alifanya nini wakati mwanaume fulani mwenye kumuogopa Mungu alimuinamia? Biblia inasema hivi: “Petro akamusimamisha, na kusema: “Simama; mimi pia ni mwanadamu tu.’” (Matendo 10:25, 26) Petro na mitume wengine hawakukubali watu wawapatie heshima ya pekee ao wawaabudu. Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye zinatukuza wale wenye watu fulani wanaona kuwa watakatifu. Sikukuu sawa vile:

    •  Siku ya Watakatifu Wote. “Ni sikukuu ya kutukuza watakatifu wote . . . Haijulikane kama ilianzaka namna gani.”​—New Catholic Encyclopedia.

    •  Sikukuu ya Mutakatifu Mwanamuke wa Guadalupe. Ile sikukuu inatukuza mutakatifu “mwanamuke wa Meksiko,” mwenye watu fulani wanaamini kuwa ni Maria, mama ya Yesu. Inasemekana kama alitokea kimuujiza mutu fulani wa ku mashamba, mu 1531.​—The Greenwood Encyclopedia of Latino Literature.

      Sikukuu ya Mutakatifu Mwanamuke wa Guadalupe

    •  Sikukuu ya Jina. Kitabu Celebrating Life Customs Around the World​—From Baby Showers to Funerals inasema kama “Sikukuu ya jina ni siku ya kukumbuka mutakatifu mwenye mutoto alipewa jina yake wakati wa ubatizo ao wakati wa kipaimara.” Ile kitabu inaongeza kama “ile siku iko na uhusiano mukubwa sana na mambo ya dini.”

     Sikukuu za mambo ya politike ao za kiraia. Biblia inasema hivi: “Ni muzuri kumukimbilia Yehova kuliko kutegemea wanadamu.” (Zaburi 118:8, 9) Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu za kisiasa ao za kiraia, sawa vile Sikukuu ya Vijana ao Sikukuu ya Wanamuke, juu kufanya vile kunaweza kuonyesha kama wanatumainia kuwa wanadamu wanaweza kumaliza magumu yenye kuwa mu dunia. Na ni ileile sababu njo inawachochea wasifanye Sikukuu ya Kumalizika kwa Utumwa na sikukuu zingine zenye kufanana na ile. Mashahidi wa Yehova wanaamini kama Ufalme wa Mungu tu njo utamaliza ubaguzi na ukosefu wa haki.​—Waroma 2:11; 8:21.

  •   Ile sikukuu inafanya kabila ao taifa fulani ionekane kuwa ya maana kuliko zingine?

     Kanuni ya Biblia: “Mungu hana ubaguzi, lakini katika kila taifa mutu mwenye anamuogopa na kufanya mambo yenye kuwa sawa anakubaliwa naye.”​—Matendo 10:34, 35.

     Mashahidi wengi wanapendaka inchi yao, lakini hawafanyake sikukuu zenye zinafanya taifa fulani ao kabila fulani ionekane kuwa ya maana kuliko ingine. Sikukuu sawa vile:

     Sikukuu za kutukuza jeshi. Yesu hakuambia wanafunzi wake wafanye vita. Lakini aliwaambia hivi: “Muendelee kupenda maadui wenu na kusali kwa ajili ya wale wenye kuwatesa ninyi.” (Matayo 5:44) Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu zenye zinatukuza maaskari, sawa vile sikukuu zenye kufuata:

    •  Siku ya Anzac. “Anzac ni kifupi ya Australian and New Zealand Army Corps,” ni kusema, Majeshi ya Australia na Nouvelle-Zélande. “Anzac ilifikia kuwa sikukuu ya kukumbuka maaskari wenye walikufiaka ku vita.”​—Historical Dictionary of Australia.

    •  Siku ya Maaskari wa Zamani (Siku ya Ukumbusho, Siku ya Kumbukumbu, Siku ya Yenga ya Ukumbusho). Zile sikukuu zinafanywa juu ya kuonyesha heshima “maaskari wa zamani na wale wenye waliuawa katika vita za kupigania inchi.”​—Encyclopædia Britannica.

     Sikukuu za kukumbuka historia ao uhuru wa inchi. Yesu alisema hivi kuhusu wanafunzi wake: “Wao hawako sehemu ya ulimwengu, kama vile mimi siko sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:16) Mashahidi wa Yehova wanafurahiaka kujifunza historia ya inchi yao, lakini hawafanyake sikukuu zenye kufuata:

    •  Siku ya Australia. Kitabu Worldmark Encyclopedia of Cultures and Daily Life inaonyesha kama ile sikukuu ni ya kukumbuka “siku yenye majeshi ya Uingereza ilishimika bendera yake ku udongo wa Australia na kutangaza kama Australia inakuwa chini ya utawala wake mu 1788.”

    •  Siku ya Guy Fawkes. Ni “sikukuu ya taifa ya kukumbuka namna Guy Fawkes na Wakatolika wenye walikuwa wanamuunga mukono walishindwa kuangusha mufalme James wa Kwanza na Bunge [ya Uingereza] mu mwaka wa 1605.”​—A Dictionary of English Folklore.

    •  Siku ya Uhuru. Mu inchi za mingi, ni “siku yenye watu wanakumbukaka tarehe yenye inchi yao ilipataka uhuru.”​—Merriam-Webster’s Unabridged Dictionary.

  •   Wakati wa ile sikukuu, watu wanakosa kujizuia na wanajiendesha mubaya?

     Kanuni ya Biblia: “Kwa maana wakati wenye ulipita uliwatosha ninyi kufanya mapenzi ya mataifa wakati mulifanya matendo ya mwenendo mupotovu wa bila haya, tamaa kali yenye haiwezi kuzuiwa, kunywa kupita kiasi, karamu za kupitisha mipaka, mashindano ya kunywa, na ibada za sanamu zenye kuchukiza.”​—1 Petro 4:3.

     Mashahidi wa Yehova wanatii ile kanuni. Njo maana hawafanyake sikukuu zenye wakati zinafanywa, watu wanakunywa sana na kushindwa kujizuia. Mashahidi wa Yehova wanafurahiaka kupitisha wakati pamoya na marafiki na wanaweza kuamua kunywa pombe, lakini kwa kiasi. Wanajikazaka kufuata hii shauri ya Biblia: “Ikuwe munakula ao munakunywa ao munafanya jambo lingine lolote, mufanye mambo yote kwa utukufu wa Mungu.”​—1 Wakorinto 10:31.

     Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake carnaval na sherehe zingine zenye zinachochea watu kufanya mambo yenye Biblia inakataza. Njo maana Mashahidi wa Yehova hawafanyake sherehe ya Wayahudi, yenye kuitwa Purimu. Hata kama kwa miaka mingi Purimu inajulikana kuwa sikukuu ya kukumbuka namna Wayahudi walikombolewaka mu karne ya tano mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, kitabu Essential Judaism inasema kama leo “tunaweza kusema kuwa ile sikukuu njo Carnaval.” Wakati wa ile sikukuu, mara mingi “wanaume wanavalaka nguo za wanamuke, watu wanashindwaka kujizuia, wanakunywaka sana, na kufanya fujo ya mingi.”

 Juu Mashahidi wa Yehova hawafanyake sikukuu fulani, ile inaonyesha kama hawapendake familia zao?

 Biblia inatuambia tupende na tuheshimie watu wa familia yetu, hata wakuwe wa dini gani. (1 Petro 3:1, 2, 7) Kusema kweli, wakati Shahidi wa Yehova anaacha kufanya sikukuu fulani, watu wa familia yake wanaweza kukasirika, kuumia mu moyo, ao kujisikia mubaya sana. Njo maana Mashahidi wa Yehova wanajikazaka kuhakikishia watu wa familia zao kama wanawapenda, kuwafasiria juu ya nini hawafanye tena sikukuu fulani, na kuwatembelea wakati ingine.

 Mashahidi wa Yehova wanaambiaka watu wengine wasifanye sikukuu fulani?

 Hapana, wanajua kama kila mutu anapaswa kujiamulia. (Yoshua 24:15) Mashahidi wa Yehova ‘wanaheshimia watu wa namna zote,’ hata wakuwe wa dini gani.​—1 Petro 2:17.

a Hii habari haizungumuzie sikukuu zote zenye Mashahidi wa Yehova hawafanyake, ao kanuni zote zenye inaomba kufikiria.

b Mithra, Mithraism, Christmas Day & Yalda, by K. E. Eduljee, ukurasa wa 31-33.