Ona video zinazopatikana

Biblia Inasema Nini Kuhusu Noeli?

Biblia Inasema Nini Kuhusu Noeli?

Jibu la Biblia

 Biblia haitoe tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu, na haiseme kwamba tunapaswa kukumbuka siku yake ya kuzaliwa. Kitabu kimoja kilichoandikwa na McClintock na Strong kinasema hivi: “Mungu hatuagize tufanye Noeli, wala AJ [Agano Jipya] halituambie hivyo.”

 Tofauti na hilo, historia ya Noeli inaonyesha kwamba sikukuu hiyo inatokana na desturi za dini za kipagani. Biblia inaonyesha kwamba tunamuchukiza Mungu tunapomuabudu katika njia ambayo hakubali.​—Kutoka 32:5-7.

Historia ya desturi za Noeli

  1.   Kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa Yesu: “Wakristo wa kwanza​-kwanza hawakukumbuka siku ya kuzaliwa kwa Yesu kwa sababu waliona kukumbuka siku ya kuzaliwa kwa mutu yeyote kuwa desturi ya wapagani.”​—The World Book Encyclopedia.

  2.   Tarehe 25 Mwezi wa 12: Hakuna jambo lolote linaloonyesha kwamba Yesu alizaliwa tarehe hiyo. Inaonekana kwamba viongozi wa dini walichagua tarehe hiyo ili ipatane na sikukuu za kipagani zilizofanywa wakati wa ao karibu na majira ya baridi kali.

  3.   Kupatiana zawadi, karamu: Kitabu kimoja kinasema hivi: “Desturi nyingi za kujifurahisha zinazofuatwa wakati wa Noeli zinatokana na Saturnalia, ambayo ilikuwa sikukuu ya Waroma iliyofanywa katikati ya Mwezi wa 12. Kwa mufano, karamu zenye madoido mengi, kupatiana zawadi, na kuwasha mishumaa zilitokana na sikukuu hiyo.” (The Encyclopedia Americana) Kitabu kingine kinasema kwamba “hakuna kazi wala biashara iliyofanywa” wakati wa Saturnalia. (Encyclopædia Britannica)

  4.   Taa za Noeli: Kulingana na kitabu kimoja, Wazungu walipamba nyumba zao kwa “taa na majani​-mabichi ya kila aina” ili kusherehekea majira ya baridi na kuwazuia roho waovu. (The Encyclopedia of Religion)

  5.   Mimea inayoitwa mulimbo na muholi: Kwa kawaida watu wanatumia mimea hiyo kuwa mapambo wakati wa Noeli. “Wadruidi (mapadri wa Waselti) walisema kwamba mulimbo ulikuwa na nguvu za kimuujiza. Mumea wa muholi ambao haukauke uliabudiwa kama ahadi ya kurudi kwa jua.”​—The Encyclopedia Americana.

  6.   Muti wa Noeli: “Wapagani wa Ulaya walizoea kuabudu miti na waliendelea na desturi hiyo kisha kuwa Wakristo.” Moja ya desturi iliyobaki ya ibada hiyo ya miti ni desturi ya “kuweka muti wa Noeli kwenye mwingilio ao ndani ya nyumba wakati wa sikukuu zinazofanywa katikati ya majira ya baridi kali.”​—Encyclopædia Britannica.