Ona video zinazopatikana

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumiake Musalaba mu Ibada?

Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawatumiake Musalaba mu Ibada?

 Watu wengi wanaonaka musalaba kuwa alama ya Ukristo. Na siye Mashahidi wa Yehova tuko Wakristo, lakini hatutumiake musalaba mu ibada. Juu ya nini?

 Sababu moja ni hii: Biblia inaonyesha kama Yesu hakukufiaka ku musalaba, lakini alikufiaka ku muti. Tena, Biblia inaonya kabisa Wakristo ‘wakimbie ibada ya sanamu,’ ni kusema hawapaswe kutumia musalaba mu ibada.​—1 Wakorinto 10:14; 1 Yohana 5:21.

 Ona pia vile Yesu alisema: “Kwa jambo hili wote watajua kama ninyi ni wanafunzi wangu​—kama muko na upendo kati yenu.” (Yohana 13:34, 35) Wakati Yesu alisema vile, alionyesha kama upendo njo alama yenye ingetambulisha Wakristo wa kweli, hapana musalaba ao sanamu fulani.