Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

TUIGE IMANI YAO | SARA

‘Wewe Ni Mwanamuke Mwenye Sura Nzuri’

‘Wewe Ni Mwanamuke Mwenye Sura Nzuri’

SARA anasimama katikati ya chumba kimoja cha nyumba yake na anaangalia pembeni yake. Fikiria katika akili yako mwanamuke wa Mashariki ya Kati mwenye kuwa na macho ya rangi ya mweusi na yenye kuonyesha namna anajisikia. Alama ya huzuni inaonekana katika sura hiyo? Kama ni hivyo, ni mwepesi kujua sababu gani. Nyumba hii ilikuwa na mambo mengi. Yeye pamoja na Abrahamu, bwana yake, walipitisha muda murefu wenye furaha katika nyumba hii. * Wote wawili walifanya nyumba hiyo ikuwe kwao kabisa.

Waliishi katika Uru, muji wenye kuendelea na wenye kujaa watu wengi wenye kuwa na ufundi mbalimbali na wafanyabiashara. Bila shaka walikuwa na mali mingi. Lakini nyumba ya Sara haikuwa tu mahali pa kuwekea vitu vyake. Yeye na bwana yake walipitisha miaka mingi ya furaha na magumu katika nyumba hiyo. Walitoa sala mara nyingi katika nyumba hiyo kwa Yehova, Mungu wao mwenye walipenda. Sara alikuwa na sababu nzuri ya kupenda sana nyumba yao.

Lakini, Sara alikuwa tayari kuhama na kuacha mambo yote yenye alijua. Hata kama alikuwa na miaka 60 hivi, angeenda mahali penye hakujua na kuishi maisha yenye kujaa magumu, bila tumaini lolote la kurudia. Sababu gani alifanya mabadiliko hayo makubwa katika maisha yake? Imani yake inaweza kutufundisha nini leo?

‘TOKA KATIKA INCHI YAKO’

Inawezekana Sara alikomalia katika muji wa Uru. Leo, ni mabomoko tu ndiyo yanapatikana nafasi kwenye kulikuwa muji huo. Lakini katika siku za Sara, mashua ya wafanyabiashara yalifanya biashara juu ya Muto Efrati kwa kuleta katika muji huo wenye kuendelea vitu mbalimbali vya bei kutoka mbali. Watu walisongamana katika barabara ndogo-ndogo na zenye kujikunja-kunja za Uru, mashua yalijaa kwenye bandari, na biashara ilijaa katika masoko ya muji huo. Wazia Sara akikomalia katika muji huo wenye kujaa watu ambao wako na utendaji mbalimbali na amefikia kujua watu wengi kwa majina yao. Bila shaka, watu katika muji huo walimujua pia, kwa sababu alikuwa mwanamuke murembo sana. Alikuwa pia na jamaa kubwa katika muji huo.

Biblia inaonyesha kama Sara alikuwa na imani kubwa, lakini haikuwa imani katika mungu-mwezi mwenye aliabudiwa sana katika muji wa Uru. Munara wa mungu huyo ulionekana katika muji wote. Lakini, Sara aliabudu Yehova, Mungu wa kweli. Maandiko hayaonyeshe namna gani alifikia kupata imani hiyo. Wakati fulani, baba yake alikuwa muabudu-sanamu. Hata hivyo, aliolewa na Abrahamu, mwanaume mwenye kumupita miaka kumi. * (Mwanzo 17:17) Kisha, Abrahamu alifikia kujulikana kuwa “baba ya wale wote walio na imani.” (Waroma 4:11) Wote wawili walifanya ndoa yao ikuwe ya muzuri na yenye nguvu. Katika ndoa hiyo, waliheshimiana, walikuwa wanazungumuza pamoja, na walikuwa tayari kusaidiana wakati wa magumu. Zaidi ya yote, walimupenda Mungu wao.

Sara alipenda sana bwana yake, na wote wawili waliishi pamoja na watu wa jamaa yao katika muji wa Uru. Hata hivyo, bila kukawia, walipambana na tatizo moja. Biblia inasema kama Sara alikuwa ‘tasa; hakuwa na mutoto.’ (Mwanzo 11:30) Katika desturi ya wakati huo, hali ya Sara ilikuwa jaribu kabisa. Lakini Sara aliendelea kuwa mwaminifu kwa Mungu na kwa bwana yake. Loti, yatima na mutoto wa ndugu ya Abrahamu, alifikia kuwa kama mutoto wao. Maisha yaliendelea vile, mupaka siku yenye mambo yote yalibadilika.

Siku moja Abrahamu alikuja kwa Sara akiwa mwenye kuchangamuka sana. Haikuwa mwepesi kwake kuamini jambo lenye lilikuwa tu limetokea. Mungu mwenye walikuwa wanaabudu alimutokea na kuzungumuza naye, bila shaka kupitia malaika! Wazia Sara akiangalia bwana yake kwa upendo, na kumuuliza kwa furaha: “Alikuambia nini? Tafazali, uniambie!” Pengine Abrahamu alikaa kwanza ili kupanga mawazo yake muzuri; kisha akamuambia mambo yenye Yehova alisema: “Toka katika inchi yako na kutoka kwa watu wa jamaa yako na ukuje mupaka katika inchi ambayo nitakuonyesha.” (Matendo 7:2, 3) Kisha kutulia, sasa walianza kufikiria mugao wenye Yehova aliwapatia. Walipaswa kuacha maisha ya muzuri yenye walikuwa nayo na kuenda kuishi maisha ya kuhama-hama! Sara aliona namna gani mugao huo? Bila shaka Abrahamu alimutazama kwa uangalifu. Sara angekuwa tayari kumuunga mukono na kufanya mabadiliko makubwa kama hayo katika maisha yao?

Jambo lenye Sara alipaswa kuamua kufanya linaweza kutushangaza. Pengine unaweza kufikiri hivi: ‘Mungu hajaniomba ao kuomba bibi ao bwana yangu kufanya jambo kama hilo!’ Hata hivyo, wakati fulani hatuombwe kukamata uamuzi kama huo? Tunaishi katika ulimwengu wenye kututia moyo tutafute kwanza maisha ya muzuri, vitu vingi vya kimwili, ao usalama wetu. Lakini, Biblia inatuomba kukamata uamuzi mwengine: kutafuta kwanza mambo ya kiroho, ni kusema, kutia mapenzi ya Mungu pa nafasi ya kwanza. (Mathayo 6:33) Kadiri tunafikiri juu ya jambo lenye Sara alifanya, tujiulize hivi: ‘Ni uamuzi gani nitakamata katika maisha yangu?’

‘WAKATOKA KATIKA INCHI’

Wakati Sara alikuwa anapanga vitu vya kubeba, alijiuliza kama anaweza kubeba nini ao kuacha nini. Alipaswa kuacha kitu chenye punda na ngamia hawangeweza kubeba, ni kusema, kila kitu chenye hakikustahili kwa ajili ya maisha ya kuhama-hama. Bila shaka, walipaswa kuuzisha ao kupatia watu wengine vitu vingi kati ya vitu vyenye walikuwa navyo. Angeacha pia maisha ya muzuri yenye alikuwa nayo katika muji. Ilikuwa mwepesi kwake kuenda kwenye masoko ili kuuza mbegu, nyama, matunda, nguo, na vitu vingine vya lazima na mambo mengine ya muzuri.

Imani ya Sara ilimuchochea kuacha mambo mazuri yenye alikuwa nayo

Pengine ilikuwa nguvu sana kwa Sara kuacha nyumba yake. Ikiwa nyumba ya Sara ilikuwa kama nyumba zenye wachimbuaji walichimbua katika Uru, pengine alikumbuka maisha ya muzuri yenye aliacha. Nyumba fulani kati ya nyumba hizo zilikuwa na vyumba zaidi ya 12, na pia mabomba kwa ajili ya maji safi na mabomba mengine. Hata nyumba ya kawaida ilikuwa na paa na kuta zenye nguvu, na mulango wenye ungeweza kufungwa. Hema ingeweza kuwalinda na wezi kama nyumba hizo? Ao ingeweza kuwalinda na simba, chui, dubu, na mbwa-mwitu, wanyama hao wote ambao walikuwa wengi wakati huo katika maeneo yenye kuzungumuziwa katika Biblia?

Tuseme nini kuhusu jamaa yake? Ni nani Sara alipaswa kuacha? Inawezekana amri ya Mungu ya ‘kutoka katika inchi yako na kutoka kwa watu wa jamaa yako’ ilikuwa jaribu, zaidi sana kwa Sara. Pengine mwanamuke huyo muchangamufu na mwenye upendo alikuwa na ndugu na dada, wajomba na shangazi pamoja na watoto wao wenye alishikamana nao sana, na ambao hangeona tena. Lakini, Sara alionyesha ujasiri, na siku baada ya siku alijitayarisha kwa ajili ya safari.

Hata kama alikuwa katika hali hiyo, Sara alikuwa tayari kuenda wakati siku yenye ilipangwa ilifika. Tera, mukubwa wa jamaa, alienda pamoja na Abrahamu na Sara hata kama alikuwa na miaka 200 hivi. (Mwanzo 11:31) Bila shaka, Sara alikuwa na mengi ya kufanya ili kuhangaikia muzazi huyo mwenye kuzeeka. Loti alijiunga pia nao wakati walitii maneno yenye Yehova alisema na ‘kutoka katika inchi ya Wakaldayo.’​—Matendo 7:4.

Walifikia kwanza Harani, kilometre 960 hivi kaskazini-mangaribi, wakipitia pembeni-pembeni ya muto Efrati. Waliishi kwa muda fulani Harani. Inawezekana Tera alikuwa mugonjwa wakati walikuwa Harani, na hakuwa na uwezo wa kuendelea na safari. Familia ilibakia Harani mupaka wakati Tera alikufa akiwa na miaka 205. Wakati fulani Yehova alizungumuza tena na Abrahamu, na kumuambia tena atoke katika eneo hilo na kuenda katika inchi yenye Yehova angemuonyesha. Mara hiyo Mungu aliongeza ahadi nzuri sana: ‘Nitakufanya taifa kubwa.’ (Mwanzo 12:2-4) Lakini wakati walitoka Harani, Abrahamu alikuwa na miaka 75 na Sara 65, na hawakuwa na mutoto. Namna gani Abrahamu angeweza kutokeza taifa? Angekuwa na bibi mwengine? Wakati huo, ilikuwa jambo la kawaida mwanaume kuwa na wanawake wengi; kwa hiyo, inawezekana Sara aliwaza juu ya jambo hilo.

Hata hivyo, walitoka Harani na kuendelea na safari. Tuzungumuzie watu wenye walikuwa sasa pamoja nao. Habari ya Biblia inasema kama familia ya Abrahamu iliondoka pamoja na mali yenye walikuwa nayo na hata “nafsi [ao, watu] ambazo walikuwa wamejipatia katika Harani.” (Mwanzo 12:5) Watu hao walikuwa nani? Inawezekana walikuwa watumishi. Lakini, inawezekana Abrahamu na Sara walielezea watu hao wenye walikuwa tayari kuwasikiliza kuhusu imani yao. Mafasirio fulani ya Wayahudi kuhusu andiko hili yanasema kama watu hao walikuwa wageuzwa-imani, watu wenye walijiunga na Abrahamu na Sara ili kuabudu Yehova. Kama ni hivyo, imani yenye nguvu yenye Sara alikuwa nayo ilimufanya aseme na uhakika wote wakati alikuwa anazungumuza nao juu ya Mungu na tumaini lake. Ni muzuri kufikiria hilo, kwa sababu tunaishi wakati wenye imani na tumaini havipatikane sana. Kama unajifunza jambo fulani la muzuri katika Biblia, utaambia wengine jambo hilo?

‘WAKATEREMUKA KUELEKEA MISRI’

Kisha kuvuka muto Efrati, pengine tarehe 14 mwezi wa Nisani mwaka wa 1943 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, walienda kusini, katika inchi yenye Yehova aliwaahidi. (Kutoka 12:40, 41) Wazia namna Sara anaangalia huku na huku, akivutiwa na uzuri, hali ya hewa yenye kupendeza, na mambo mbalimbali ya inchi hiyo. Karibu na miti mikubwa ya More, karibu na Shekemu, Yehova anamutokea tena Abrahamu. Mara hiyo alimuambia hivi: ‘Nitaupa uzao wako inchi hii.’ Ah, neno “uzao,” lingekuwa na maana kubwa kwa Abrahamu! Bila shaka, hilo lilimukumbusha shamba la Edeni, kwenye Yehova alitabiri kama uzao ungeharibu Shetani. Tayari Yehova alikuwa amemuambia Abrahamu kwamba taifa lenye angetokeza lingefungulia watu wote wenye kuishi duniani njia ya kupata baraka.​—Mwanzo 3:15; 12:2, 3, 6, 7.

Hata hivyo, familia hiyo ilipatwa pia na magumu ya ulimwengu huu. Njaa kubwa ilitokea katika inchi ya Kanaani, na Abrahamu akaamua kupeleka familia yake kusini kuelekea Misri. Lakini, alitambua hatari yenye ingeweza kutokea katika eneo hilo. Kwa hiyo, alimuambia Sara hivi: ‘Tafazali, tazama! najua vema kuwa wewe ni mwanamuke mwenye sura nzuri. Basi itakuwa kwamba Wamisri watakapokuona watasema: Huyu ni muke wake. Nao wataniua, lakini wewe watakuhifazi hai [ao, hawatakuua]. Tafazali sema wewe ni dada yangu, ndipo ikuwe vema kwangu kwa sababu yako, na nafsi [ao, uzima] yangu itaishi kwa ajili yako.’ (Mwanzo 12:10-13) Sababu gani Abrahamu aliomba Sara afanye jambo hilo lenye halikuwa la kawaida?

Abrahamu hakuwa muongo wala mwoga, kama vile watu fulani wamesema. Kwa kweli, Sara alikuwa dada-nusu ya Abrahamu. Na Abrahamu alikuwa na sababu nzuri ya kuwa mwangalifu. Abrahamu na Sara walijua kwamba hakukuwa jambo lingine la maana kuliko kusudi la Mungu la kutokeza uzao wa pekee na taifa kupitia Abrahamu. Kwa hiyo, usalama wa Abrahamu ulikuwa jambo la maana sana. Zaidi ya hiyo, mambo yenye yamevumbuliwa yameshuhudia kwamba ilikuwa jambo la kawaida kwa watu wenye mamlaka katika Misri kunyanganya bibi ya mwanaume fulani na kuua mwanaume huyo. Kwa hiyo, Abrahamu alitenda kwa hekima, na Sara alikubali kwa unyenyekevu kumuunga mukono bwana yake.

Kisha muda kidogo tu, mambo yenye yalitokea yalionyesha kama Abrahamu alikuwa na sababu nzuri ya kuwa mwangalifu; watu fulani wenye kuwa na mamlaka katika utawala wa Farao walitambua kwamba Sara alikuwa murembo sana hata kama alikuwa mwenye kuzeeka. Walimuelezea Farao habari juu ya Sara, naye akasema waende kumukamata! Ni wazi kwamba Abrahamu alihangaika sana na Sara aliogopa. Hata hivyo, inaonekana kama Sara hakutendewa kama mateka, lakini kama mugeni mwenye kuheshimiwa. Pengine Farao alipanga kumutongoza na kumushangaza kwa kumuonyesha mali yake na kujaribu kuzungumuza na “ndugu” yake ili Sara akuwe bibi yake.​—Mwanzo 12:14-16.

Wazia Sara akiangalia eneo la Misri kupitia dirisha ao baraza la nyumba ya mufalme. Alijisikia namna gani kuwa tena ndani ya nyumba yenye kuwa na kuta, paa, na chakula cha muzuri mbele yake? Alivutiwa tena na maisha ya raha, pengine yenye kupita hata maisha yenye alikuwa nayo katika muji wa Uru? Wazia furaha yenye Shetani angekuwa nayo kama Sara angekubali kumuacha Abrahamu na kuwa bibi ya Farao! Lakini Sara hakufanya jambo lolote kama hilo. Alibakia mushikamanifu kwa bwana yake, kwa ndoa yake, na kwa Mungu wake. Kama tu kila mutu mwenye kuoa ao kuolewa katika ulimwengu huu mubaya angeonyesha ushikamanifu kama huo! Utafuata mufano wa ushikamanifu wa Sara katika uhusiano wako pamoja na wapendwa na marafiki wako?

Hata kama alipata majaribu katika nyumba ya Farao, Sara alibakia mushikamanifu kwa bwana yake

Yehova alitenda ili kulinda mwanamuke huyo mupendwa kwa kutuma mapigo juu ya Farao na nyumba yake. Wakati Farao alifikia kujua kwamba Sara alikuwa bibi ya Abrahamu, mara moja akamurudisha kwa bwana yake na kuomba familia yote ya Abrahamu itoke katika inchi ya Misri. (Mwanzo 12:17-20) Wazia namna Abrahamu alifurahi wakati walimurudishia bibi yake mupendwa! Usisahau kwamba alikuwa amemuambia hivi kwa upendo: ‘Najua vema kuwa wewe ni mwanamuke mwenye sura nzuri.’ Lakini alifurahia sana uzuri wa namna ingine wenye Sara alikuwa nao kuliko sura yake ya inje. Sara alikuwa na uzuri wa ndani kabisa, wenye Yehova anaona kuwa wa maana sana. (1 Petro 3:1-5) Huo ni uzuri wenye kila mumoja wetu anaweza kukomalisha. Kama tunatia mambo ya kiroho mbele ya mambo ya kimwili na kujikaza kutangazia wengine mambo yenye tunajua juu ya Mungu, na pia kama tunashikamana na kanuni za Mungu za mwenendo safi wakati tunapata majaribu, tutaonyesha kwamba tunaiga imani ya Sara.

^ fu. 3 Mwanzoni, majina yao yalikuwa Abramu na Sarai, lakini wanajulikana sana kwa majina yenye Yehova alifikia kuwapatia.​—Mwanzo 17:5, 15.

^ fu. 8 Sara alikuwa dada-nusu ya Abrahamu. Tera alikuwa baba yao wote wawili, lakini walikuwa na mama tofauti. (Mwanzo 20:12) Hata kama leo ni mubaya kufunga ndoa kama hiyo, ni jambo la maana kujua kwamba mambo yalikuwa tofauti wakati huo. Wanadamu walikuwa karibu na ukamilifu wenye Adamu na Eva walipoteza. Kwa watu hao wenye afya nzuri, ndoa kati ya watu wa jamaa ya karibu haikuwa na hatari yoyote juu ya watoto wenye walizaliwa. Lakini, miaka 400 kisha, urefu wa maisha ulikuwa kama wetu. Wakati huo sasa, Sheria ya Musa ilikataza ngono kati ya watu wa jamaa ya karibu sana.​—Mambo ya Walawi 18:6.