Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Jina Tattannu limeandikwa kwenye sehemu moja ya bamba hili la maandishi ya kikabari

Ushuhuda mwingine

Ushuhuda mwingine

Kuna ushuhuda wa vitu vya zamani vyenye kuchimbuliwa ambao unaunga mukono habari ya Biblia? Katika mwaka wa 2014 habari moja katika gazeti Biblical Archaeology Review ilikuwa na ulizo hili: “Ni watu ngapi katika Maandiko ya Kiebrania wameshuhudiwa na vitu vya zamani vyenye vilivumbuliwa?” Jibu lenye lilitolewa: “50 hivi!” Mwanaume mumoja mwenye hakuwa katika liste hiyo ni Tatenai. Alikuwa nani? Tuone namna Biblia inazungumuzia Tatenai kwa kifupi.

Muji wa Yerusalemu ulikuwa sehemu ya Utawala wa Waperse [ao, Waajemi]. Muji huo ulikuwa katika eneo lenye Waperse waliita Ngambo ya Muto, ni kusema, mangaribi mwa muto Efrati. Kisha kukamata muji wa Babiloni, Waperse waliacha huru Wayahudi wenye walikuwa wamekamatwa na kuwaruhusu kujenga tena hekalu la Yehova katika Yerusalemu. (Ezra 1:1-4) Lakini, maadui wa Wayahudi walipinga mupango huo, na walitumia jambo hilo ili kuchongea Wayahudi kwamba wanapinga utawala wa Waperse. (Ezra 4:4-16) Wakati wa utawala wa Dario wa Kwanza (522-486 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu), mukubwa mumoja wa utawala wa Waperse mwenye kuitwa Tatenai alichunguza jambo hilo. Biblia inamuita ‘gavana wa Ngambo ya Muto.’​—Ezra 5:3-7.

Inawezekana, mabamba ya maandishi ya kikabari yenye kuwa na jina la Tatenai ambayo yameokoka ni sehemu ya maandishi ya familia. Bamba lenye kupatanisha mutu mumoja wa familia hiyo na mutu mwenye kutajwa katika Biblia ni ahadi yenye kuandikwa ya kulipa deni. Bamba hilo ni la mwaka wa 20 wa utawala wa Dario wa Kwanza, ni kusema, 502 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu. Linaonyesha kwamba shahidi wa mapatano ya kibiashara ni mutumishi wa “Tattannu, gavana wa Ngambo ya Muto,” ni kusema, Tatenai mwenye kutajwa katika kitabu cha Biblia cha Ezra.

Mwanaume huyo alikuwa na daraka gani? Katika mwaka wa 535 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Koreshi Mukubwa alipanga maeneo yenye kuwa chini ya utawala wake katika majimbo, na moja katika ya majimbo hayo iliitwa Babiloni na Ngambo ya Muto. Kisha muda fulani, jimbo hilo liligawanywa katika sehemu mbili, na sehemu moja ikaitwa Ngambo ya Muto. Sehemu hiyo ya Ngambo ya Muto ilitia ndani Coele-Siria, Foinike, Samaria, na Yuda, na inawezekana iliongozwa kutoka Damasko. Tatenai aliongoza eneo hilo kuanzia 520 mupaka 502 hivi, mbele ya kuzaliwa kwa Yesu.

Kisha kuenda Yerusalemu ili kuchunguza kama Wayahudi walikuwa wanapinga Waperse, Tatenai alimuambia Dario kama walisema kwamba ni Koreshi ndiye aliwapatia ruhusa ya kujenga upya hekalu la Yehova. Uchunguzi katika maandishi ya kifalme ulihakikisha jambo hilo. (Ezra 5:6, 7, 11-13; 6:1-3) Kwa hiyo, Tatenai aliambiwa asipinge jambo hilo, na alitii.​—Ezra 6:6, 7, 13.

Kusema kweli, “Tatenai gavana wa Ngambo ya Muto’ hakutimiza jambo la maana kabisa katika historia. Lakini, Maandiko yanamutaja bila kukosea kwa jina lake la cheo. Hilo linatupatia ushuhuda mwingine kwamba vitu vya zamani vyenye kuchimbuliwa vinaendelea kuhakikisha kama habari yenye Biblia inazungumuzia kuhusu historia ni ya kweli.