Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ninafurahia kupitisha wakati pamoja na vijana wa kutaniko

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Nilipenda Besiboli Kuliko Kitu Kingine!

Nilipenda Besiboli Kuliko Kitu Kingine!
  • ALIZALIWA MWAKA WA: 1928

  • INCHI: KOSTA RIKA

  • ALIKUWA: MWENYE KUPENDA SANA MICHEZO YA KULIPWA NA MICHEZO YA FEZA

MAISHA YANGU YA ZAMANI

Nilikomalia Puerto Limón, muji wenye kuwa na bandari (port), mashariki mwa Kosta Rika. Wazazi wetu walikuwa na watoto munane, na mimi nilikuwa wa saba. Baba alikufa wakati nilikuwa na miaka munane. Kisha jambo hilo kutokea, mama alitukomalisha peke yake.

Besiboli ilikuwa sehemu ya maisha yangu sikuzote. Nilipenda muchezo huo wakati nilikuwa mutoto. Wakati nilikaribia miaka 20, nilijiunga na kikundi cha watu wenye kucheza besiboli ili kujifurahisha tu. Wakati nilikuwa ninacheza katika kikundi hicho nikiwa sasa na miaka 20 na kitu, mwanaume mumoja aliniomba nijiunge na kikundi cha wachezaji wenye kulipwa katika inchi ya Nikaragua. Lakini, kwa sababu afya ya mama yangu haikuwa muzuri wakati huo na ni mimi ndiye nilikuwa ninamuchunga, sikupenda kuishi Nikaragua. Kwa hiyo nilikataa. Kisha, mwanaume mwengine aliniomba nicheze katika timu la taifa la besiboli la Kosta Rika, lenye lilifanyizwa na wachezaji wenye walichaguliwa katika kikundi cha wachezaji wa kujifurahisha tu. Mara hiyo niliitika. Nilicheza katika timu hilo la taifa kuanzia mwaka wa 1949 mupaka 1952, na nilicheza pamoja na timu hilo katika Kuba, Meksiko, na Nikaragua. Nilikuwa muchezaji muzuri wa besiboli, ningecheza sehemu 17 bila kufanya hata kosa moja. Nilifurahi kusikia watu wakiimba kwa kutaja jina langu!

Jambo la huzuni ni kwamba, nilikuwa pia na mwenendo mubaya. Hata kama nilikuwa na rafiki mwanamuke mumoja, nilikuwa ninatoka na wanawake wengine kila mara. Tena, nilikuwa mulevi sana. Siku moja nililewa sana hivi kwamba wakati niliamuka kesho yake, sikukumbuka namna nilifika nyumbani! Nilifanya pia michezo ya feza ya domino na kucheza tombola.

Wakati huo, mama yangu alifikia kuwa Shahidi wa Yehova. Alijaribu kunisaidia ili nipendezwe na imani yake, lakini alishindwa mwanzoni, kwa sababu nilizama kabisa katika michezo. Kama nilikuwa ninafanya mazoezi wakati wa kula, singeweza hata kusikia njaa! Nilifikiria tu michezo. Nilipenda besiboli kuliko kitu kingine!

Lakini siku moja wakati nilikuwa ninacheza, nikiwa na miaka 29, niliumia sana wakati nilijaribu kukamata kabumbu. Kisha kujisikia muzuri, niliacha muchezo huo wa kulipwa. Hata hivyo, niliendelea kuzoeza wachezaji katika timu la wachezaji wenye walipenda kucheza tu ili kujifurahisha karibu na kwangu.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

Katika mwaka wa 1957, nilikubali mualiko wa kuenda kwenye mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova wenye ulifanywa ndani ya kiwanja ambamo nilikuwa ninachezea besiboli. Wakati nilikaa pamoja na wasikilizaji wengine, nilitambua kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa na utaratibu, tofauti na makelele na fujo yenye nilikuwa ninaona wakati wa michezo ya besiboli katika kiwanja hicho. Mambo yenye niliona kwenye mukusanyiko huo yalinichochea kuanza kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova na kuenda kwenye mikutano yao.

Nilipendezwa sana na mambo mengi yenye nilijifunza katika Biblia. Kwa mufano, Yesu alitabiri kwamba katika siku za mwisho, wanafunzi wake wangehubiri habari njema ya Ufalme wa Mungu katika dunia yote. (Mathayo 24:14) Nilijifunza pia kwamba, Wakristo wa kweli hawafanye kazi yao ya kuhubiri ili kupata feza. Yesu alisema hivi: ‘Mulipokea bure, mutoe bure.’​—Mathayo 10:8.

Wakati nilikuwa ninajifunza Biblia, nililinganisha mambo yenye Biblia inasema na mambo yenye niliona kati ya Mashahidi wa Yehova. Bidii yao kwa ajili ya kutangaza habari njema ya Ufalme wa Mungu ilinipendeza sana. Niliona kwamba walionyesha roho ya kutoa kama vile Yesu aliambia Wakristo wafanye. Kwa hiyo, wakati nilisoma Marko 10:21 na kuona mualiko huu wa Yesu, ‘Kuja ukuwe mufuasi wangu,’ nilipenda kuwa Shahidi.

Lakini, iliomba wakati murefu ili nimufuate kabisa. Kwa mufano, kwa miaka mingi nilicheza kila juma namba yangu ya “bahati” katika tombola la taifa. Hata hivyo, nilijifunza katika Biblia kwamba Mungu anachukia wale wenye kuabudu “mungu wa Bahati Njema,” na hata wale wenye pupa. (Isaya 65:11; Wakolosai 3:5) Kwa hiyo, nikaamua kuacha michezo ya feza. Siku ya Yenga ya kwanza kisha kuacha kucheza tombola, namba yangu ya “bahati” ilipata ushindi! Watu walinichekelea kwa sababu sikucheza juma hilo, na walinikaza sana ili nicheze tena, lakini sikufanya hivyo. Tangu wakati huo, sijarudilia tena kucheza michezo ya feza.

Nilipambana na jaribu lingine la ‘utu wangu mupya’ siku yenye nilibatizwa kwenye mukusanyiko wa Mashahidi wa Yehova. (Waefeso 4:24) Mangaribi ya siku hiyo, wakati nilirudia kwenye hoteli ambako nilikuwa ninapanga, nilikuta rafiki yangu mwanamuke wa zamani akiningoja kwenye mulango wa chumba changu. Aliniambia hivi: “Sammy, acha tujifurahishe!” Lakini nikamujibia mara moja hivi: “Hapana!” Nilimukumbusha kwamba nilikuwa ninaishi sasa kulingana na kanuni za Biblia. (1 Wakorintho 6:18) Alisema kwa sauti ya juu: “Nini?” Kisha akazarau mawazo ya Biblia kuhusu uasherati na akanikaza turudilie tena uhusiano wetu. Lakini, niliingia tu ndani ya chumba changu na kufunga mulango. Leo, nafurahi kusema kwamba tangu nilikuwa Shahidi katika mwaka wa 1958, nimeshikamana na kanuni za Biblia zenye zimebadilisha maisha yangu.

FAIDA YENYE NIMEPATA

Ah, kama ningeandika kitabu chenye kuonyesha faida zenye nimepata kwa kufuata muongozo wa Biblia! Kati ya faida hizo ni kwamba niko sasa na marafiki wa kweli, maisha yenye kusudi, na furaha ya kweli.

Ningali ninafurahia besiboli, lakini nimebadilisha mawazo yangu. Nilijulikana sana na nilipata feza nyingi katika besiboli, lakini mambo hayo yalikuwa ya muda mufupi tu. Lakini, uhusiano wangu pamoja na Mungu na familia ya ndugu na dada ya duniani pote vitaendelea milele. Biblia inasema hivi: “Ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.” (1 Yohana 2:17) Sasa napenda Yehova Mungu na watu wake kuliko kitu kingine!