Ona video zinazopatikana

Bibila Inasema Nini Kuhusu Bikira Maria?

Bibila Inasema Nini Kuhusu Bikira Maria?

 Jibu ya Biblia

 Biblia inasema kama Maria, mama ya Yesu, alikuwa na pendeleo ya pekee sana ya kumuzala Yesu wakati alikuwa angali bikira. Biblia ilitabiri ile jambo mu kitabu ya Isaya na ilionyesha namna ile jambo ilitimia mu Injili ya Matayo na Luka.

 Mu unabii kuhusu kuzaliwa kwa Masiya, Isaya alitabiri hivi: “Kijana mwanamuke atapata mimba na atazaa mwana.” (Isaya 7:14) Chini ya muongozo wa roho takatifu, Matayo muandikaji wa Injili, alionyesha kama unabii wa Isaya ulitimia wakati Maria alibeba mimba ya Yesu. Kisha kusema kama Maria alipata mimba kwa njia ya muujiza, Matayo aliongezea hivi: “Kwa kweli, hayo yote yalitokea ili kutimiza yale yenye yalisemwa na Yehova kupitia nabii wake, wakati alisema: ‘Angalia! Bikira * atapata mimba na atazaa mwana, na watamupatia jina Emanueli,’ lenye wakati linatafsiriwa linamaanisha, ‘Mungu Iko Pamoja na Sisi.’”​—Matayo 1:22, 23.

 Luka mwandikaji wa Injili alisema pia kama Maria alipata mimba kwa njia ya muujiza. Aliandika kama Mungu alimutuma malaika Gabrieli “kwa bikira mumoja mwenye alikuwa anachumbiwa na mwanaume mwenye kuitwa Yosefu wa nyumba ya Daudi, na jina la ule bikira lilikuwa Maria.” (Luka 1:26, 27) Maria alihakikisha kama alikuwa bikira. Kisha kusikia kama angekuwa mama ya Yesu, Masiya, Maria aliuliza hivi: “Hilo litawezekana namna gani, kwa kuwa sijalala na mwanaume?”​—Luka 1:34.

 Iliwezekana namna gani bikira azale mutoto?

 Maria alipata mimba kupitia roho takatifu, ni kusema, nguvu ya utendaji ya Mungu. (Matayo 1:18) Malaika alimuambia Maria hivi: “Roho takatifu itakuja juu yako, na nguvu za Mwenye Kuwa Juu Zaidi zitakufunika kwa kivuli. Na kwa hiyo ule mwenye atazaliwa ataitwa mutakatifu, Mwana wa Mungu.” * (Luka 1:35) Mungu alifanya muujiza: Alihamisha uzima wa Mwana wake na kuutia mu tumbo ya Maria, na ile ilifanya akuwe na mimba.

 Juu ya nini bikira alizala mutoto?

 Mungu alitumia bikira juu azale mutu mukamilifu, ni kusema, Yesu, mwenye angeweza kuokoa wanadamu kutoka katika zambi na kifo. (Yohana 3:16; Waebrania 10:5) Mungu alihamisha uzima wa Yesu na kuutia mu tumbo ya Maria. Kisha pale, inaonekana wazi kuwa roho takatifu ya Mungu ililinda Yesu wakati alikuwa mu tumbo ya Maria juu asiambukizwe na hali yoyote ya kutokamilika.​—Luka 1:35.

 Njo maana Yesu alizaliwa mukamilifu, alikuwa sawa vile Adamu mbele afanye zambi. Biblia inasema hivi kuhusu Yesu: “Yeye hakufanya zambi.” (1 Petro 2:22) Juu Yesu alikuwa mukamilifu, angeweza kulipa bei ya ukombozi ili kukomboa wanadamu katika zambi na kifo.​—1 Wakorinto 15:21, 22; 1 Timoteo 2:5, 6.

 Maria aliendelea kuwa bikira?

 Biblia haifundishe kama Maria aliendelea kuwa bikira maisha yake yote. Lakini, inaonyesha kama Maria alizala watoto wengine.​—Matayo 12:46; Marko 6:3; Luka 2:7; Yohana 7:5.

Biblia inafundisha kama Yesu alikuwa na ndugu wengi

 Yesu alizaliwa mukamilifu, ni kusema, Maria hakukuwa na zambi?

 Hapana. Kulingana na New Catholic Encyclopedia, fundisho ya kama Maria alizaliwa bila zambi “inaonyesha kama Bikira Maria hakukuwa na ZAMBI YA ASILI tangu mwanzo wa maisha yake, ni kusema, tangu mama yake akuwe na mimba yake. Wanadamu wengine wote waliriti zambi . . . Lakini Maria, kwa NEEMA ya pekee, alilindwa juu asiambukizwe hata kidogo na zambi ya asili.” *

 Lakini hakuna fasi kwenye Biblia inafundisha kama Maria hakukuwa na zambi ya asili. (Zaburi 51:5; Waroma 5:12) Na hata Maria alionyesha kama alikuwa mutenda-zambi wakati alitoa zabihu ya zambi yenye Sheria ya Musa iliomba mama watoe. (Mambo ya Walawi 12:2-8; Luka 2:21-​24) Kitabu New Catholic Encyclopedia inasema hivi: “Maandiko haifundishe waziwazi kama Maria alizaliwa bila zambi . . . [Ni] fundisho ya kanisa.”

 Tunapaswa kumuona Maria namna gani?

 Maria alituachia mufano muzuri: Alikuwa na imani, alikuwa mutiifu, alikuwa munyekevu, na alimupenda Mungu sana. Iko kati ya waaminifu wenye tunapaswa kuiga.​—Waebrania 6:12.

 Hata kama Maria alikuwa na daraka ya pekee ya kuwa mama ya Yesu, Biblia haifundishe kama tunapaswa kumuabudu ao kusali kwake. Yesu hakupatia mama yake heshima fulani ya pekee na hakusema kama wanafunzi wake wanapaswa kufanya vile. Maria anazungumuziwa mu vitabu vya Injili na mara moya tu mu kitabu ya Matendo. Lakini hazungumuziwe mu vitabu vingine 22 vya ile yenye kuitwa Agano Jipya.​—Matendo 1:14.

 Biblia haionyeshe kama Maria alipewa heshima fulani ya pekee na Wakristo wa kwanza-kwanza. Lakini Biblia inafundisha kama Wakristo wanapaswa kumuabudu tu Mungu.​—Matayo 4:10.

^ Neno ya Kiebrania yenye kutafsiriwa “kijana mwanamuke” mu unabii wa Isaya ni ʽal·mahʹ, yenye inaweza kumaanisha mwanamuke bikira ao mwanamuke mwenye haiko bikira. Lakini, chini ya muongozo wa roho takatifu, Matayo alitumia neno ya Kigiriki par·theʹnos, yenye inamaanisha tu “bikira.”

^ Watu fulani wanasema kama maneno “Mwana wa Mungu,” haifae juu ni sawa vile Mungu alifanyaka ngono na mwanamuke. Lakini, maandiko haiseme vile. Inamuita tu Yesu kuwa “Mwana wa Mungu” na “muzaliwa wa kwanza wa viumbe vyote” juu Yesu tu njo wa kwanza na wa mwisho kuumbwa moja kwa moja na Mungu. (Wakolosai 1:13-​15) Biblia inamuita pia mwanadamu wa kwanza, Adamu, kuwa “mwana wa Mungu.” (Luka 3:38) Inamuita vile juu aliumbwa na Mungu.

^ Toleo ya Pili, Buku ya 7, ukurasa wa 331.