Ona video zinazopatikana

Yesu Anatuokoa Namna Gani?

Yesu Anatuokoa Namna Gani?

Jibu ya Biblia

 Yesu aliokoa wanadamu waaminifu wakati alitoa uzima wake kuwa bei ya ukombozi. (Matayo 20:28) Njo maana Biblia inamuita “mwokozi wa ulimwengu.” (1 Yohana 4:14) Biblia inasema tena hivi: “Hakuna wokovu katika mutu mwingine yeyote, kwa maana hakuna jina lingine chini ya mbingu lenye wanadamu walipewa, lenye kupitia hilo tunapaswa kuokolewa.”​—Matendo 4:12.

 Yesu ‘alionja kifo kwa ajili ya kila mutu’ mwenye anamuamini. (Waebrania 2:9; Yohana 3:16) Kisha, “Mungu alimufufua kutoka kwa wafu,” na Yesu akarudia mbinguni akiwa kiumbe wa roho. (Matendo 3:15) Kule mbinguni, Yesu anaweza “kuokoa kwa ukamili wale wenye wanamukaribia Mungu kupitia yeye, kwa sababu sikuzote iko muzima ili kuwaombea.”​—Waebrania 7:25.

Juu ya nini tuko na lazima Yesu atukomboe?

 Siye wote tuko watenda-zambi. (Waroma 3:23) Zambi Inatutenganisha na Mungu, na inatupeleka ku kifo. (Waroma 6:23) Lakini Yesu ni “muteteaji” wa wale ambao wanaamini bei yake ya ukombozi. (1 Yohana 2:1, maelezo ya chini) Anawatetea mbele ya Mungu, kwa kumuomba asikilize sala zao na awasamehe zambi zao kwa musingi wa zabihu yake ya ukombozi. (Matayo 1:21; Waroma 8:34) Mungu anasikilizaka ile maombi ya Yesu juu inapatana na mapenzi yake. Mungu alimutuma Yesu ku dunia “ili ulimwengu uokolewe kupitia yeye.”​—Yohana 3:17.

Kama tu unaamini Yesu ni kusema utaokolewa?

 Hapana. Ni kweli kama tunapaswa kuamini Yesu juu tuokolewe, lakini kuko mambo ingine yenye tunapaswa kufanya. (Matendo 16:30, 31) Biblia inasema hivi: “Kama vile mwili bila roho umekufa, vilevile pia imani bila matendo imekufa.” (Yakobo 2:26) Juu tuokolewe, tunapaswa:

  •   Kujifunza juu ya Yesu na Baba yake, Yehova.​—Yohana 17:3.

  •   Kuwaamini.​—Yohana 12:44; 14:1.

  •   Kuonyesha imani yetu kwa kutii amri zao (Luka 6:46; 1 Yohana 2:17) Yesu alifundisha kama haiko kila mutu mwenye anamuita “Bwana” njo ataokolewa, lakini ni ule tu mwenye “kufanya mapenzi ya Baba [yake] mwenye kuwa mbinguni.”​—Matayo 7:21.

  •   Kuendelea kuonyesha imani hata wakati wa magumu. Yesu alionyesha waziwazi ile jambo wakati alisema hivi: “Lakini ule mwenye atavumilia mupaka mwisho ataokolewa.”​—Matayo 24:13.