Hamia kwenye habari

Je, Mtu Anaweza Kujiuzulu Kuwa Shahidi wa Yehova?

Je, Mtu Anaweza Kujiuzulu Kuwa Shahidi wa Yehova?

 Ndiyo. Mtu anaweza kujiuzulu kutoka katika tengenezo letu kwa njia mbili:

  •   Kwa ombi rasmi. Mtu anaweza kutoa ombi kwa mdomo au kwa maandishi kwamba ameamua hataki kuendelea kuwa Shahidi wa Yehova.

  •   Kwa matendo. Mtu anaweza kuchukua hatua inayomfanya asiwe sehemu ya undugu wetu wa ulimwenguni pote. (1 Petro 5:9) Kwa mfano, anaweza kujiunga na dini nyingine na kujulisha wazi nia yake ya kuendelea kushirikiana na dini hiyo.​—1 Yohana 2:​19.

Namna gani ikiwa mtu haendelei kuhubiri au kuhudhuria mikutano? Je, mnamwona mtu huyo kuwa amejiuzulu?

 Hapana, hatumwoni hivyo. Kujiuzulu, au kujitenga, ni tofauti na kuwa dhaifu katika imani. Mara nyingi, wale ambao kwa muda wanapunguza bidii au wanaacha kuabudu pamoja nasi hawajaacha imani badala yake wanakuwa wamevunjika moyo tu. Badala ya kuwapuuza watu kama hao, tunajaribu kuwafariji na kuwategemeza. (1 Wathesalonike 5:​14; Yuda 22) Ikiwa mtu anataka msaada, wazee wa kutaniko huongoza kutoa msaada wa kiroho.​—Wagalatia 6:1; 1 Petro 5:​1-3.

 Hata hivyo, wazee hawajapewa mamlaka ya kumshurutisha au kumshinikiza mtu aendelee kuwa Shahidi wa Yehova. Kila mtu hujichagulia dini atakayofuata. (Yoshua 24:15) Tunaamini kwamba wale wanaomtumikia Mungu wanapaswa kufanya hivyo kwa hiari, kutoka moyoni.​—Zaburi 110:3; Mathayo 22:37.