Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Huwaepuka Watu Ambao Zamani Walishirikiana na Dini Yao?

Je, Mashahidi wa Yehova Huwaepuka Watu Ambao Zamani Walishirikiana na Dini Yao?

 Watu waliobatizwa na kuwa Mashahidi wa Yehova lakini sasa wameacha kuwahubiria wengine, labda hata wameacha kushirikiana na waamini wenzao, hawaepukwi. Kwa kweli, sisi hujaribu kuwasaidia waanze kupendezwa tena na mambo ya Mungu.

 Mtu anapofanya dhambi nzito hatengwi na ushirika moja kwa moja. Hata hivyo, Shahidi aliyebatizwa anapokuwa na mazoea ya kuvunja sheria ya maadili ya Biblia bila kutubu, anaepukwa au anatengwa na ushirika. Biblia inasema hivi waziwazi: “Ondoeni yule mtu mwovu kati yenu.”—1 Wakorintho 5:13.

 Lakini vipi mtu anayetengwa lakini mke wake na watoto ni Mashahidi wa Yehova? Uhusiano wa kidini aliokuwa nao na familia yake unabadilika, hata hivyo, uhusiano wa kifamilia unaendelea. Uhusiano wa ndoa na shughuli za kawaida za familia zinaendelea.

 Watu waliotengwa na ushirika wanaweza kuhudhuria mikutano yetu ya kidini. Wakipenda, wanaweza kupata mashauri ya kiroho kutoka kwa wazee wa kutaniko. Kusudi ni kumsaidia kila mmoja astahili tena kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Watu waliotengwa na ushirika wanaokataa mwenendo usiofaa na kuonyesha tamaa ya kweli ya kuishi kupatana na viwango vya Biblia wanakaribishwa kuwa Mashahidi wa Yehova tena.