Barua ya Kwanza ya Petro 5:1-14

  • Lichungeni kundi la Mungu (1-4)

  • Muwe wanyenyekevu na mkeshe (5-11)

    • Mtupieni Mungu mahangaiko yenu yote (7)

    • Ibilisi ni kama simba anayenguruma (8)

  • Maneno ya kumalizia (12-14)

5  Kwa hiyo, nikiwa mzee pia, shahidi wa mateso ya Kristo, na mshiriki wa utukufu utakaofunuliwa,+ ninawasihi* wazee miongoni mwenu:  Lichungeni kundi la Mungu+ lililo chini ya utunzaji wenu, mkiwa waangalizi,* si kwa kulazimishwa, bali kwa hiari mbele za Mungu;+ si kwa kupenda pato lisilo la haki,+ bali kwa hamu;  si kupiga ubwana juu ya wale ambao ni urithi wa Mungu,+ bali kuwa vielelezo kwa kundi.+  Na mchungaji mkuu+ atakapofunuliwa, mtapokea taji la utukufu lisilofifia.+  Vivyo hivyo, enyi vijana, jitiisheni kwa wanaume wazee.*+ Lakini ninyi nyote mtendeane kwa* unyenyekevu,* kwa sababu Mungu huwapinga wenye majivuno, lakini huwapa wanyenyekevu fadhili zisizostahiliwa.+  Kwa hiyo, jinyenyekezeni chini ya mkono wenye nguvu wa Mungu, ili awainue kwa wakati unaofaa,+  huku mkitupa mahangaiko* yenu yote juu yake,+ kwa sababu yeye anawajali ninyi.+  Tunzeni akili zenu, iweni waangalifu!+ Adui yenu, Ibilisi, anatembea huku na huku kama simba anayenguruma, akitafuta kummeza mtu.*+  Lakini chukueni msimamo dhidi yake,+ mkiwa imara katika imani, mkijua kwamba mateso yaleyale yanaupata ushirika mzima wa ndugu zenu* ulimwenguni.+ 10  Lakini, baada ya kuteseka kwa muda mfupi, Mungu wa fadhili zote zisizostahiliwa, aliyewaita kwenye utukufu wake wa milele+ katika muungano na Kristo, yeye mwenyewe atamaliza mazoezi yenu. Atawafanya muwe imara,+ atawatia nguvu,+ atawapa msingi imara. 11  Na awe na nguvu milele. Amina. 12  Kupitia Silvano,*+ ambaye ninamwona kuwa ndugu mwaminifu, nimewaandikia kwa maneno machache, ili kuwatia moyo na kutoa ushahidi kwa bidii kwamba hizi ndizo fadhili zisizostahiliwa za Mungu. Simameni imara katika fadhili hizo. 13  Mwanamke aliye Babiloni, aliyechaguliwa kama ninyi, anawatumia salamu zake, na vilevile Marko,+ mwanangu. 14  Salimianeni kwa busu la upendo. Na muwe na amani ninyi nyote mlio katika muungano na Kristo.

Maelezo ya Chini

Au “ninawahimiza.”
Au “mkililinda kwa makini.”
Au “wazee.”
Au “mjifunge; mjivike.”
Au “unyenyekevu wa akili.”
Au “matatizo; wasiwasi wenu wote.”
Au “akimtafuta mtu ili ammeze.”
Tnn., “undugu wenu.”
Pia anaitwa Sila.