Ona video zinazopatikana

Je, Ninyi Ni Wakristo?

Je, Ninyi Ni Wakristo?

 Ndiyo. Sisi ni Wakristo sababu:

  •   Tunajikaza kufuata kabisa-kabisa mafundisho na mwenendo wa Yesu Kristo.—1 Petro 2:21.

  •   Tunaamini kwamba Yesu ndiye ufunguo wa kupata wokovu, na kwamba “hakuna jina lingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu ambalo kupitia hilo lazima sisi tupate kuokolewa.”—Matendo 4:12.

  •   Watu wanabatizwa katika jina la Yesu ili kuwa Mashahidi wa Yehova.—Mathayo 28:18, 19.

  •   Tunasali kupitia jina la Yesu.—Yohana 15:16.

  •   Tunaamini kwamba Yesu ndiye Kichwa, ao ndiye aliyepewa mamlaka juu ya kila mutu.—1 Wakorintho 11:3.

 Hata hivyo, kuna mambo mengi yanayotutofautisha na dini zingine zinazojiita za Kikristo. Kwa mufano, tunaamini kwamba Biblia inafundisha kama Yesu ni Mwana wa Mungu, yeye si sehemu ya Utatu. (Marko 12:29) Tunaamini kwamba nafsi inakufa, na kwamba hakuna andiko lolote linaonyesha kama Mungu anawatesa watu katika moto wa milele, na hatuamini kwamba wale wanaoongoza katika makanisa wanapaswa kuwa na macheo yanayowainua juu ya wengine.—Mhubiri 9:5; Ezekieli 18:4; Mathayo 23:8-10.