Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Kuvumilia Wengine—Biblia Inaweza Kukusaidia

Kuvumilia Wengine—Biblia Inaweza Kukusaidia

 “Kuvumilia wengine kunasiadiaka kukuwe amani.”​—Mambo yenye UNESCO ilisema kuhusu kuvumilia wengine, mu 1995.

 Lakini kukosa kuvumilia wengine kunaweza kufanya watu wasiheshimiane na hata wachukiane. Na ile inaweza kutokeza maneno ya chuki, ubaguzi, na jeuri.

 Lakini watu wako na mawazo tofauti kuhusu maana ya kuvumilia wengine. Watu fulani wanawaza kama mutu mwenye anavumilia wengine anapaswa kukubali matendo yote na tabia zote za wengine. Lakini wengine wako na mawazo ya Biblia juu ya ile jambo, ni kusema, mutu mwenye anavumilia wengine anaheshimia haki ya kila mutu ya kujichagulia kanuni za mwenendo na mambo ya kuamini, hata kama yeye hakubaliane na ile mambo.

 Biblia inaweza kusaidia watu waweze kuvumilia wengine mu njia yenye kufaa mu dunia ya leo?

Mambo yenye Biblia inasema juu ya kuvumilia wengine

 Biblia inatutia moyo tuvumilie wengine. Inasema hivi: “Usawaziko wenu ujulikane kwa watu wote” (Wafilipi 4:5) Biblia inatutia moyo tutendee wengine muzuri na kwa adabu. Watu wenye kufuata ile mashauri ya Biblia, inawezekana hawakubaliane na kanuni za mwenendo za mutu mwingine na hawazifuate, lakini wanaacha ule mutu atende kulingana na mambo yenye amejiamulia.

 Hata vile, Biblia inasema kama Mungu ameonyesha namna wanadamu wanapaswa kujiendesha. Inasema hivi: “Ee mwanadamu, [Mungu] amekuambia mambo mema.” (Mika 6:8) Inaonyesha muongozo wenye Mungu anatoa ili kusaidia watu wakuwe na maisha ya muzuri kadiri inawezekana.​—Isaya 48:17, 18.

 Mungu haturuhusu kuhukumu watu wengine. Biblia inaonyesha kama “kuko mumoja tu mwenye kuwa Mutoaji-sheria na Muamuzi . . . Wewe ni nani ili ukuwe unamuhukumu jirani yako?” (Yakobo 4:12) Mungu anapatia kila mutu uhuru wa kukamata maamuzi, juu kila mutu atatoa hesabu kulingana na maamuzi yake.​—Kumbukumbu la Torati 30:19.

Mambo yenye Biblia inasema juu ya heshima

 Biblia inasema kama tunapaswa “[kuheshimu] watu wote.” (1 Petro 2:17, Biblia Habari Njema) Kwa hiyo, wale wenye wanaamua kufuata kanuni za Biblia wanatendea watu wote kwa heshima, bila kuangalia mambo yenye wanaamini ao namna yao ya kuishi. (Luka 6:31) Lakini, ile haimaanishe kama wale wenye kufuata mashauri ya Biblia wanakubaliana na mambo yote yenye wengine wanaamini, ao mawazo yote yenye wengine wako nayo, ao kama wanaunga mukono maamuzi yote yenye wengine wanakamata. Hata vile kuliko kukosea wengine adabu ao kuwatendea bila heshima, wanajikaza sana kuiga namna Yesu alikuwa anatendea wengine.

 Kwa mufano, Yesu alikutana na mwanamuke fulani mwenye alikuwa mu dini yenye yeye hakukubaliana nayo. Ule mwanamuke alikuwa pia anaishi na mwanaume mwenye hakukuwa bwana yake, namna ya kuishi yenye Yesu hakukubali. Hata vile Yesu alizungumuza na ule mwanamuke kwa heshima.​—Yohana 4:9, 17-24.

 Kama Yesu, Wakristo wako tayari kufasiria mambo yenye wanaamini kwa wale wenye kuwa tayari kusikiliza. Lakini wanafanya vile kwa “heshima kubwa.” (1 Petro 3:15) Biblia inafundisha Wakristo kama hawapaswe kukaza wengine wakubali mawazo yao. Inasema kama mufuasi wa Kristo “hana lazima ya kupigana, lakini anapaswa kuwa mupole kwa wote,” kutia ndani wale wenye wanaamini mambo tofauti.​—2 Timoteo 2:24.

Mambo yenye Biblia inasema kuhusu chuki

 Biblia inatuambia ‘tufuatie amani pamoja na watu wote.’ (Waebrania 12:14) Mutu mwenye anafuatilia amani anaepuka chuki. Bila kuvunja kanuni zake mwenyewe, anajikaza kuishi kwa amani pamoya na wengine. (Matayo 5:9) Biblia inatia pia moyo Wakristo kupenda maadui wao kwa kutendea muzuri wale wenye wanawatendea mambo ya mubaya.​—Matayo 5:44.

 Kwa kweli, Biblia inasema kama Mungu “anachukia,” ao “anachukia sana,” matendo yenye inashushia wengine heshima ao inawaumiza. (Mezali 6:16-19) Biblia inatumia hapa neno kuchukia ili kuonyesha namna matendo ya mubaya inapaswa kuchukiwa sana. Biblia inaonyesha kama Mungu iko tayari kusamehe na kusaidia watu wenye wanabadilisha namna yao ya kuishi na kuanza kuishi kulingana na kanuni zake.​—Isaya 55:7.

Maandiko ya Biblia yenye inazungumuzia kuvumilia wengine na kuwaheshimia

 Tito 3:2: ‘Mukuwe na usawaziko, na mukuwe wapole kuelekea watu wote.’

 Mutu mwenye usawaziko anatendea kwa upole watu wenye kuwa na mawazo yenye kuwa tofauti na yake, na ile inafanya watu watendeane kwa heshima.

 Matayo 7:12: “Mambo yote yenye munataka watu wawatendee, ninyi pia lazima muwatendee wao.”

 Siye wote tunafurahiaka wakati wengine wanatutendea kwa heshima na wanahangaikia mawazo yetu. Ili kujifunza mambo mingi kuhusu hii amri ya mwenendo yenye kujulikana sana yenye Yesu alifundisha, ona habari “Yesu Alisema Tunapaswa Kuwatendeaje Wengine?

 Yoshua 24:15: “Muchague leo ni nani mutatumikia.”

 Wakati tunaheshimia haki ya wengine ya kukamata maamuzi tunasaidia kukuwe amani.

 Matendo 10:34: “Mungu hana ubaguzi.”

 Mungu hakuwake nabagua mutu juu tu ya desturi yake, juu tu ni mwanaume ao mwanamuke, juu ya inchi yake, ao rangi yake ya ngozi. Wale wenye wanapenda kumuiga Mungu, wanaheshimia watu wote.

 Habakuki 1:12, 13: ‘[Mungu] hawezi kuvumilia uovu.’

 Uvumilivu wa Mungu, uko na mipaka. Hataruhusu watu waendelee kufanya mambo ya mubaya milele. Ili kujifunza mambo mingi, angalia video Sababu Gani Mungu Anaacha Mateso?

 Waroma 12:19: “Muachie kasirani kali [ya Mungu] nafasi; kwa maana imeandikwa: ‘Kisasi ni changu; mimi nitalipa,’ ni vile Yehova anasema.” a

 Yehova haruhusu mutu yeyote alipize kisasi. Kwa wakati wenye ameweka atahakikisha kama kila mutu anatendewa kwa haki. Ili kujifunza mambo mingi, ona habari “Je, Kilio cha Haki Kitasikika?

a Yehova ni jina ya pekee ya Mungu. (Zaburi 83:18) Ona habari “Yehova Ni Nani?