Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Mimi na bibi yangu Tabitha katika mahubiri

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Kwangu Mimi, Hakukuwa Mungu

Kwangu Mimi, Hakukuwa Mungu
  • ALIZALIWA MWAKA WA: 1974

  • INCHI: JAMUHURI YA KIDEMOKRASIA YA UJERUMANI

  • ALIKUWA: ANAAMINI KAMA HAKUNA MUNGU

MAISHA YANGU YA ZAMANI

Nilizaliwa katika muji moja mudogo katika Saxony, Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Ujerumani ya zamani. Hali nyumbani ilikuwa nzuri na yenye upendo, na wazazi wangu walinifundisha kanuni nzuri za mwenendo. Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Ujerumani ilikuwa inchi ya Kikomunisti, kwa hiyo, watu wengi wa Saxony hawakuona dini kuwa ya maana. Na kwangu mimi, hakukuwa Mungu. Miaka 18 ya kwanza ya maisha yangu iliongozwa na mambo mbili: imani ya kwamba hakuna Mungu na Ukomunisti.

Sababu gani Ukomunisti ulinivutia? Kwa sababu nilipenda wazo la kwamba watu wote wako sawa. Zaidi ya hilo, niliamini kwamba mali yote yalipaswa kugawanywa sawasawa, kwa sababu kufanya hivyo kungemaliza tofauti yenye kuwa kati ya matajiri sana na masikini sana. Kwa hiyo, nilijiingiza katika kikundi cha Ukomunisti cha vijana. Wakati nilikuwa na miaka 14, nilitumika katika mupango wa kutunza mazingira kwa kutengeneza upya karatasi zenye zimekwisha kutumikishwa. Wakubwa wa muji wa Aue walipendezwa sana na bidii yenye nilionyesha hivi kwamba walinipatia zawadi. Hata kama nilikuwa kijana, nilifikia kujuana na wakubwa fulani wenye cheo cha juu katika serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Ujerumani. Niliwaza kama nilikuwa mwenye kufuatilia mambo ya maana na kama maisha yangu ya wakati wenye kuja yangekuwa muzuri.

Kisha kulitokea mabadiliko makubwa. Katika mwaka wa 1989, ukuta wa Berlin ulianguka na pia inchi za Kikomunisti za Ulaya ya mashariki. Hali iliendelea kuwa mubaya zaidi. Bila kukawia, nilitambua kwamba ukosefu wa haki ulienea sana katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Ujerumani. Kwa mufano, watu wenye hawakuunga mukono Ukomunisti walitendewa kama raia wa hali ya chini. Namna gani hilo liliwezekana? Haikuwa sisi Wakomunisti ndio tuliamini kwamba watu wote wako sawa? Ukomunisti ulikuwa jambo la kuwazia tu? Nilihangaika sana.

Kwa hiyo, nilibadilisha mambo yenye nilitanguliza katika maisha na kukazia akili muziki na ufundi wa kuchora. Kufanya kazi ya mwanamuziki na muchoraji ilikuwa ndoto yangu kwa sababu nilijifunza kwenye masomo ya muziki nikiwa na matumaini ya kuenda kwenye masomo ya juu. Zaidi ya hilo, niliacha kufuata kanuni za mwenendo muzuri zenye nilijifunza wakati nilikuwa mutoto. Jambo lenye lilikuwa sasa la lazima kwangu lilikuwa kujifurahisha na hilo lilitia ndani kufanya urafiki wa kimapenzi pamoja na wanawake wengi kwa wakati mumoja. Lakini, muziki, mambo ya kuchora, na kuishi bila kujali havikupunguza mahangaiko yangu. Hata picha zenye nilichora zilionyesha woga wenye haufae. Wakati wenye kuja ungekuwa namna gani? Na maisha yalikuwa na kusudi gani?

Wakati nilifikia kupata majibu yenye nilikuwa ninatafuta, nilishangaa sana. Mangaribi moja kwenye masomo, nilikuwa na wanafunzi fulani wenzangu tukizungumuza kuhusu wakati wenye kuja. Mandy * alikuwa mwanafunzi na pia Shahidi wa Yehova. Mangaribi hiyo, alinipatia shauri la muzuri. Aliniambia hivi: “Andreas, kama unapenda kupata majibu ya maulizo yako kuhusu maisha na kuhusu wakati wenye kuja, chunguza Biblia kwa uangalifu.”

Sikuamini kabisa mambo alisema, lakini niliamua kuchunguza Biblia ili kupata majibu. Mandy aliniongoza kwenye Danieli sura ya 2, na mambo yenye nilisoma yaliniacha kinywa wazi. Unabii huo unazungumuzia serikali kubwa za ulimwengu zenye zingefuatana, ambazo zingekuwa na uvutano mukubwa mupaka siku zetu. Mandy alinionyesha unabii mwingine mwingi wa Biblia wenye kuzungumuzia wakati wetu wenye kuja. Nilipata majibu ya maulizo yangu karibu yote! Lakini, ni nani aliandika unabii huo, na ni nani angeweza kutabiri mambo yenye yangetokea wakati wenye kuja bila kukosea? Inawezekana Mungu iko kabisa?

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU

Mandy alifanya nizungumuze na Horst na Angelika, bibi na bwana wenye kuwa Mashahidi, wenye walinisaidia kuelewa muzuri zaidi Neno la Mungu. Nilitambua haraka kwamba ni dini ya Mashahidi wa Yehova tu, ndiyo kila mara inatumia na kukazia uangalifu jina la Mungu la pekee, Yehova. (Zaburi 83:18; Mathayo 6:9) Nilijifunza kwamba Yehova Mungu anatolea wanadamu tumaini la kuishi milele katika dunia paradiso. Andiko la Zaburi 37:9 linasema: ‘Wale wanaomutumaini Yehova ndio watakaoimiliki dunia.’ Nilielewa kwamba tumaini hilo ni la watu wenye kujikaza kuishi kulingana na kanuni za Mungu juu ya mwenendo kama vile inaonyeshwa katika Biblia.

Hata hivyo, nilijikaza sana kubadilisha maisha yangu ili yapatane na Biblia. Kujulikana sana kama mwanamuziki na muchoraji kulifanya nikuwe na kiburi, kwa hiyo iliomba kwanza nijifunze kuwa munyenyekevu. Zaidi ya hilo, haikuwa mwepesi kuacha mwenendo mubaya wenye nilikuwa nao. Niko mwenye shukrani sana kwa Yehova kwa sababu anaonyesha uvumilivu, rehema, na anaelewa watu wenye kufanya nguvu yao yote ili kutumikisha mambo yenye Biblia inafundisha!

Kwa muda wa miaka 18 ya kwanza ya maisha yangu niliongozwa na Ukomunisti na imani ya kwamba hakuna Mungu, lakini kisha hapo na kufikia sasa Biblia imebadilisha maisha yangu. Mambo yenye nilijifunza yalituliza mahangaiko yangu juu ya wakati wenye kuja na kunipatia kusudi katika maisha. Katika mwaka wa 1993, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova, na katika mwaka wa 2000, nilioa Tabitha, Shahidi mwenye kuwa na bidii. Tunapitisha wakati mwingi kulingana na hali yetu ili kusaidia wengine wajue Biblia. Wengi kati ya watu wenye tunakutana nao wameongozwa na Ukomunisti na imani ya kwamba hakuna Mungu, kama vile mimi pia nilikuwa zamani. Najisikia muzuri sana wakati nawaonyesha namna ya kumujua Yehova.

FAIDA YENYE NIMEPATA

Wakati nilianza kushirikiana na Mashahidi wa Yehova, wazazi wangu waliogopa. Lakini sasa, wameona namna maisha yangu yamebadilika kwa sababu ya kushirikiana na Mashahidi. Nafurahi kwamba wanasoma sasa Biblia na wanakusanyika pamoja na Mashahidi wa Yehova.

Mimi na Tabitha tunafurahia ndoa nzuri kwa sababu tunajikaza kufuata sana mashauri ya Biblia kuhusu ndoa. Kwa mufano, kutii shauri la Biblia kuhusu uaminifu wa bibi na bwana kunaendelea kutia nguvu ndoa yetu.​—Waebrania 13:4.

Siogope tena maisha na sihangaike tena kuhusu wakati wenye kuja. Najisikia kuwa kati ya familia ya duniani pote ya waamini wenzangu, familia yenye kufurahia amani na umoja wa kweli. Katika familia hiyo tunaonana kuwa sawa. Hilo ndilo jambo lenye nilitafuta na nilitaka kupata katika maisha yangu yote.

^ fu. 12 Jina limebadilishwa.