Ona video zinazopatikana

Ufufuo Ni Nini?

Ufufuo Ni Nini?

Jibu ya Biblia

 Mu Biblia, neno yenye kutafsiriwa “ufufuo” inatokana na neno ya Kigiriki a·naʹsta·sis, yenye kumaanisha “kuinuka” ao “kusimama tena.” Mutu mwenye anafufuliwa anainuliwa kutoka katika kifo na anarudishiwa uzima. Anakuwa vile alikuwaka mbele akufe.​—1 Wakorinto 15:12, 13.

 Neno “ufufuo” haipatikane mu Maandiko ya Kiebrania, yenye kuitwa pia Agano la Kale. Lakini ahadi ya ufufuo inapatikana ndani. Kwa mufano, kupitia nabii Hosea, Mungu alitoa hii ahadi: “Nitawakomboa kutoka katika nguvu za Kaburi; nitawaokoa kutoka katika kifo.”​—Hosea 13:14; Yobu 14:13-​15; Isaya 26:19; Danieli 12:2, 13.

 Watu watafufuliwa juu waishi wapi? Watu fulani watafufuliwa juu waishi mbinguni. Kule, watatawala na Kristo. (2 Wakorinto 5:1; Ufunuo 5:9, 10) Biblia inaita ufufuo wao kuwa “ufufuo wa kwanza.” Ile inaonyesha kama kutakuwa ufufuo mwingine. (Ufunuo 20:6; Wafilipi 3:11) Ufufuo mwingine ni wa watu wengi sana wenye watafufuliwa juu waishi ku dunia.​—Zaburi 37:29.

 Watu watafufuliwa namna gani? Mungu amepatia Yesu nguvu ya kufufua wafu. (Yohana 11:25) Yesu atafufua “wale wote wenye kuwa katika makaburi ya ukumbusho.” Kila mutu mwenye atafufuliwa atakuwa vile alikuwaka mbele akufe. (Yohana 5:28, 29) Wale wenye wanafufuliwa ili kuenda mbinguni wanapewa mwili wa roho. Wale wenye watafufuliwa ili kuishi ku dunia watapewa mwili wa nyama na damu, lakini wenye hauna kasoro, na watakuwa na afya ya muzuri kabisa.​—Isaya 33:24; 35:5, 6; 1 Wakorinto 15:42-​44, 50.

 Nani njo atafufuliwa? Biblia inasema kama “kutakuwa ufufuo wa wenye haki na wenye hawako wenye haki.” (Matendo 24:15) Wenye haki ni watu waaminifu, sawa vile Noa, Sara, na Abrahamu. (Mwanzo 6:9; Waebrania 11:11; Yakobo 2:21) Wenye hawako wenye haki ni wale wenye hawakutii sheria za Mungu juu hawakupata nafasi ya kujifunza zile sheria na kuzifuata.

 Lakini, kuko watu wenye ni wabaya sana, wenye hawawezi kubadilika. Wale watu hawatafufuliwaka.​—Matayo 23:33; Waebrania 10:26, 27.

 Ufufuo utafanyika wakati gani? Biblia ilisema kama ufufuo wa wale wenye wataenda mbinguni ungeanza wakati wa kuwapo kwa Kristo. Ule ufufuo ulianza mu mwaka wa 1914. (1 Wakorinto 15:21-​23) Ufufuo wa wale wenye wataishi ku dunia utafanyika wakati wa Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo. Ile wakati, dunia itafanywa kuwa paradiso.​—Luka 23:43; Ufunuo 20:6, 12, 13.

 Juu ya nini unaweza kuamini kama kutakuwa ufufuo? Biblia inazungumuzia watu 9 wenye walifufuliwa. Na mu kila hali, kuko watu wenye walishuhudia ile jambo. (1 Wafalme 17:17-​24; 2 Wafalme 4:32-​37; 13:20, 21; Luka 7:11-​17; 8:40-​56; Yohana 11:38-​44; Matendo 9:36-​42; Matendo 20:7-​12; 1 Wakorinto 15:3-6) Kwa mufano, Yesu alimufufua Lazaro, hata kama Lazaro alikuwa amefanya siku ine mu kaburi, na alifanya vile mbele ya watu wengi. (Yohana 11:39, 42) Hata wale wenye walikuwa namupinga Yesu hawakukatala kama Yesu alimufufua Lazaro. Njo maana walifanya mipango ya kuua Yesu na Lazaro.​—Yohana 11:47, 53; 12:9-​11.

 Biblia inaonyesha kama Mungu iko na uwezo na nia ya kufufua wafu. Anakumbuka mambo yote juu ya kila mutu mwenye atafufua kwa kutumia nguvu yake yenye haina mipaka. (Yobu 37:23; Matayo 10:30; Luka 20:37, 38) Mungu iko na uwezo wa kufufua wafu, na anapenda kufanya vile! Wakati Biblia inazungumuzia ufufuo, inasema hivi juu ya Mungu: “Utatamani sana kazi ya mikono yako.”​—Yobu 14:15.

Mawazo ya uongo juu ya ufufuo

 Wazo ya uongo: Ufufuo ni kuunganisha tena nafsi na mwili.

 Kweli njo hii: Biblia inasema kama nafsi njo mutu, hapana kitu fulani yenye inaendelea kuishi kisha mwili kufa. (Mwanzo 2:7, maelezo ya chini; Ezekieli 18:4) Mutu mwenye anafufuliwa haunganishwe tena na nafsi yake; lakini anaumbwa tena na kuwa nafsi yenye uzima.

 Wazo ya uongo: Watu fulani watafufuliwa na kuharibiwa palepale.

 Kweli njo hii: Biblia inasema kama “wale wenye walizoea kutenda mambo maovu” watapata “ufufuo wa hukumu.” (Yohana 5:29) Lakini watahukumiwa juu ya mambo yenye watafanya kisha kufufuliwa, hapana juu ya mambo yenye walifanyaka mbele wakufe. Yesu alisema hivi: “Wafu watasikia sauti ya Mwana wa Mungu, na wale wenye wamesikiliza wataishi.” (Yohana 5:25) Majina ya wale wenye ‘watasikiliza,’ ao kutii, mambo yenye watajifunza kisha kufufuliwa itaandikwa mu “kitabu cha kukunjwa cha uzima.”​—Ufunuo 20:12, 13.

 Wazo ya uongo: Wakati mutu anafufuliwa, anapewa mwili uleule wenye alikuwaka nao mbele akufe.

 Kweli njo hii: Kisha kufa, mwili wa mutu unaharibikaka.​—Muhubiri 3:19, 20.