Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Mahangaiko

Mahangaiko

Kuko mahangaiko ya aina mbili: mahangaiko yenye kufaa na mahangaiko yasiyofaa. Biblia inatusaidia kutambua aina hizo mbili.

Ni jambo la kawaida kuwa na mahangaiko?

UKWELI

Mahangaiko yanaweza kufanya mutu ajisikie kuwa na mashaka, wasiwasi, ao woga. Kwa sababu tunaishi katika dunia yenye hatujue jambo lenye linaweza kutokea kesho, kila mutu anaweza kuwa na mahangaiko.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Mufalme Daudi aliandika hivi: ‘Nitaweka upinzani katika nafsi yangu mupaka wakati gani, huzuni katika moyo wangu wakati wa muchana?’ (Zaburi 13:2) Ni nini ilisaidia Daudi ashindane na hali hiyo? Alimufungulia Mungu moyo wake katika sala, kwa kutumainia kabisa upendo mushikamanifu wa Mungu. (Zaburi 13:5; 62:8) Kwa kweli, Mungu anatuomba tumutupie mizigo yetu. Andiko la 1 Petro 5:7 linasema hivi: ‘Mutupe mahangaiko yenu yote juu [ya Mungu], kwa sababu yeye anawajali [anawahangaikia] ninyi.’

Kufanyia jambo fulani wapendwa wetu kunaweza kutupunguzia mahangaiko juu yao

Mara nyingi, kuko mambo yenye tunaweza kufanya ili kupunguza mahangaiko yetu. Kwa mufano, wakati Paulo, muandikaji mumoja wa Biblia, alikuwa na “hangaiko kwa ajili ya makutaniko yote,” alifanya yake yote ili kufariji na kutia moyo watu wenye alihangaikia. (2 Wakorintho 11:28) Katika njia hiyo, mahangaiko yake yalikuwa yenye kufaa, kwa sababu yalimuchochea kutolea wengine musaada wenye walikuwa nao lazima. Sisi pia tunaweza kufanya vile. Lakini, kama hatufanye vile, hilo linaweza kuonyesha kama hatupendezwe nao.—Methali 17:17.

‘Muendelee kuangalia, si faida za kibinafsi [za kipekee] za mambo yenu wenyewe tu, bali pia faida za kibinafsi za wengine.’Wafilipi 2:4.

Namna gani unaweza kupiganisha hali ya kuhangaika sana?

UKWELI

Watu wanaweza kuhangaika juu ya makosa yao ya zamani, juu ya wakati unaokuja, ao juu ya feza. *

MAMBO BIBLIA INASEMA

Kuhangaika juu ya makosa ya zamani: Mbele ya kuwa Wakristo, watu fulani walikuwa walevi, wanyanganyi, waasherati, na wezi. (1 Wakorintho 6:9-11) Kuliko kukazia akili maisha yao ya zamani, walibadilisha njia zao na kutumainia rehema kubwa ya Mungu, yenye anaonyesha kwa kupenda. Andiko la Zaburi 130:4 linasema hivi: ‘Kwako wewe [Mungu] kuna musamaha wa kweli, ili upate kuogopwa.’

Kuhangaika juu ya mambo ya kesho: Yesu alisema hivi: ‘Musihangaike kamwe juu ya kesho, kwa maana kesho itakuwa na mahangaiko yake yenyewe.’ (Mathayo 6:25, 34) Alipenda kusema nini? Upiganishe mahangaiko ya leo. Usiyafanye yakuwe magumu kwa kufikiria mahangaiko ya kesho, yenye yanaweza kukufanya usione mambo namna yalivyo na kukufanya ukamate maamuzi ya haraka. Tena, ukumbuke kama mahangaiko mengi yanaweza kuonekana mwishowe kuwa hayakukuwa ya lazima.

Kuhangaika juu ya feza: Mwanaume mumoja mwenye hekima alisali hivi: ‘Usinipe umasikini wala utajiri.’ (Methali 30:8) Lakini, alitafuta kuwa na sifa ya kutosheka ao kufurahia tu yenye angeweza kupata; sifa yenye Mungu anakubali. Andiko la Waebrania 13:5 linasema hivi: ‘Namna yenu ya maisha ikuwe bila upendo wa pesa, huku mukirizika na vitu vya sasa. Kwa maana [Mungu] amesema: Sitakuacha wala kukutupa hata kidogo.’ Feza zinaweza kutuvunja moyo, lakini Mungu hawezi hata siku moja kuvunja moyo watu wenye kumutumainia na wenye kuishi maisha mepesi.

‘Sijamuona mutu yeyote muadilifu akiwa ameachwa kabisa, wala uzao wake ukitafuta mukate.’Zaburi 37:25.

Kuko siku tutaishi bila mahangaiko?

MAMBO WATU WANASEMA

Katika habari moja ya mwaka wa 2008 ya gazeti The Guardian, mutangazaji wa habari Harriet Green alisema hivi: “Tunaingia katika kipindi kipya cha mahangaiko.” Katika mwaka wa 2014, Patrick O’Connor aliandika katika gazeti moja kama “Waamerika wanaonekana kuwa wenye kuhangaika sana kuliko zamani.” (The Wall Street Journal)

MAMBO BIBLIA INASEMA

‘Hangaiko katika moyo wa mutu linaufanya uiname, lakini neno njema linafanya ushangilie.’ (Methali 12:25) ‘Neno njema’ linaweza kupatikana katika habari njema ya Ufalme wa Mungu. (Mathayo 24:14) Ufalme huo, ni kusema, serikali ya Mungu, utafanya hivi karibuni mambo yenye sisi wenyewe hatuwezi kufanya; utaondoa mambo yenye kuleta mahangaiko, kama vile ugonjwa na kifo! “[Mungu] atafuta kila chozi kutoka katika macho [yetu], na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena.”—Ufunuo 21:4.

“Mungu anayetoa tumaini na awajaze ninyi shangwe yote na amani kwa kuamini kwenu.”Waroma 15:13.

^ fu. 10 Inaweza kuwa muzuri watu wenye kuteswa na tatizo la kuhangaika sana waonane na munganga. Gazeti Amuka! halipendekeze matunzo yoyote.