Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SEHEMU YA KUULIZA MAULIZO | YAN-DER HSUUW

Mwanasayansi wa Kiini-Tete Anaeleza Imani Yake

Mwanasayansi wa Kiini-Tete Anaeleza Imani Yake

PROFESA Yan-Der Hsuuw anasimamia uchunguzi wa kiini-tete (embryon) kwenye Masomo ya Juu ya Sayansi na Teknolojia katika muji wa Pingtung, inchi ya Taiwan. Wakati fulani aliamini mageuzi, lakini uchunguzi wake wa mambo ya sayansi ulimusaidia kubadilisha mawazo yake. Alielezea gazeti Amuka! sababu zenye zilifanya abadilishe mawazo yake.

Tafazali, tuelezee kidogo maisha yako.

Nilizaliwa katika mwaka wa 1966 na nilikomalia katika inchi ya Taiwan. Wazazi wangu waliabudu kama watu wa dini ya Tao na dini ya Wabuda. Hata kama tuliabudu wazazi wetu wa zamani na kusali mbele ya sanamu, hatukuunga mukono wazo la kwamba kuko Muumbaji.

Sababu gani ulijifunza biolojia?

Wakati nilikuwa mutoto, nilipenda kutunza wanyama, na nilipenda kujifunza namna ya kuwasaidia wanyama na watu kutoka katika mateso. Kwanza, nilijifunza masomo ya kuwa munganga wa wanyama, na kisha nilijifunza masomo ya kiini-tete; nilitumaini kama masomo hayo ya kiini-tete yangenisaidia kujua namna uzima ulianza.

Wakati fulani uliamini mageuzi. Unaweza kutuelezea sababu gani?

Walimu kwenye masomo ya juu walitufundisha mageuzi, na walisema kama kulikuwa ushuhuda wenye kuunga mukono mageuzi. Niliwaamini.

Sababu gani ulianza kusoma Biblia?

Nilichochewa na mambo mbili. Kwanza, nilifikiri kama kati ya miungu mingi yenye watu wanaabudu, kunapaswa kuwa mungu mumoja mwenye kuwa mukubwa zaidi kuliko wengine. Lakini, ni mungu gani? Pili, nilijua kama Biblia ni kitabu chenye kuheshimiwa sana. Kwa hiyo, nilijiunga na masomo mbalimbali za kujifunza Biblia.

Katika mwaka wa 1992, wakati nilianza kusomea kwenye Masomo ya Juu ya Wakatoliki katika muji wa Louvain, inchi ya Ubelgiji (Belgique), nilitembelea kanisa moja la Katoliki na nilimuomba padri anisaidie kuelewa Biblia, lakini alikataa ombi langu.

Namna gani ulipata majibu ya maulizo yako?

Kisha miaka mbili, wakati nilikuwa ninafanya uchunguzi wa mambo ya sayansi katika inchi hiyo, nilikutana na Ruth, mwanamuke mumoja wa inchi ya Polandi mwenye alikuwa Shahidi wa Yehova. Alijifunza luga ya Kichina ili kusaidia wanafunzi wa masomo ya juu wenye walitaka kujua mengi kuhusu Mungu. Nilikuwa nimesali juu ya kupata musaada kama huo, kwa hiyo, nilifurahi sana kukutana naye.

Ruth alinionyesha kama Biblia inapatana na sayansi hata kama haiko kitabu cha sayansi. Kwa mufano, Daudi muandikaji mumoja wa Biblia alisema hivi katika sala yake kwa Mungu: “Macho yako yalikiona kiini-tete changu, na katika kitabu chako sehemu zake zote zilikuwa zimeandikwa, kuhusiana na siku ambazo zilifanyizwa na hakukuwako hata moja kati ya hizo.” (Zaburi 139:16) Hata kama Daudi alikuwa anatumikisha maneno ya mufano, alisema kweli! Hata mbele ya kufanyizwa kwa sehemu mbalimbali za mwili, maagizo kuhusu namna sehemu hizo zitakomaa yanapatikana tayari. Kupatana kwa Biblia kulinihakikishia kama ni Neno la Mungu. Tena, nilianza kuelewa kama kuko Mungu mumoja tu wa kweli, ni kusema, Yehova. 1

Ni nini ilikuhakikishia kama Mungu aliumba uzima?

Kusudi la uchunguzi wa mambo ya sayansi ni kutafuta kujua kweli, haiko kuunga mukono mawazo yenye watu wako nayo. Masomo yangu kuhusu namna kiini-tete kinakomaa yalinisaidia kubadilisha mawazo yangu, na nilifikia kuamini kama uzima uliumbwa. Kwa mufano, mafundi wanatengeneza mashine ndefu ili sehemu zote zieneane katika mupangilio muzuri na kwa njia ya muzuri. Kiini-tete pia kinakomaa kwa njia kama hiyo, lakini yenye kuwa ngumu kueleweka hata zaidi.

Kiini tete kinaanza na chembe moja iliyotungishwa, sivyo?

Ndiyo. Chembe hiyo ndogo sana inajigawanya, na inaendelea kugawanyika katika chembe zingine. Kwa muda fulani, hesabu ya chembe inaongezeka mara mbili kisha kila kipindi cha saa 12 mupaka 24. Katika mwanzo wa hatua hiyo, chembe zenye kuitwa chembe za musingi zinafanyizwa. 2 Chembe hizo za musingi zinaweza kutokeza aina yoyote ya chembe mbalimbali karibu 200 zenye kuwa za lazima juu ya kufanyiza mutoto muzima, kama vile chembe za damu, za mifupa, za neva, na chembe zingine.

Masomo yangu kuhusu namna kiini-tete kinakomaa yalinisaidia kuamini kama uzima uliumbwa

Chembe zenye kufaa zinapaswa kutokezwa kwa utaratibu wenye kufaa na kwenye nafasi zenye kufaa. Kwanza chembe hizo zinajikusanya na kufanyiza chembe zenye kufanana zenye zitajikusanya pia ili kufanyiza viungo mbalimbali na miguu na mikono. Ni fundi gani anaweza kuandika maagizo kwa ajili ya hatua kama hizo? Lakini, maagizo juu ya namna kiini-tete kinakomaa yanaandikwa muzuri sana katika ADN. Wakati ninachunguza uzuri huo, hilo linafanya niamini kuwa uzima uliumbwa na Mungu.

Sababu gani uliamua kuwa Shahidi wa Yehova?

Kwa kifupi, ni upendo. Yesu Kristo alisema hivi: ‘Kwa jambo hili wote watajua kwamba ninyi ni wanafunzi wangu, mukiwa na upendo kati yenu wenyewe.’ (Yohana 13:35) Upendo huo hauna ubaguzi. Hauchague inchi ya mutu, desturi, ao rangi yake ya ngozi. Nilichunguza na kujionea upendo kama huo wakati nilianza kujiunga pamoja na Mashahidi.

^ 2. Kwa sababu ya zamiri yake ya Kikristo, Profesa Yan-Der Hsuuw hatumikishe chembe za musingi za mwanadamu katika kazi yake.