Hamia kwenye habari

Kwa Nini Mnaitwa Mashahidi wa Yehova?

Kwa Nini Mnaitwa Mashahidi wa Yehova?

 Yehova ndilo jina la Mungu, linalopatikana katika Biblia. (Kutoka 6:3; Zaburi 83:18) Shahidi ni mtu ambaye hutangaza maoni au kweli ambazo amesadiki.

 Kwa hiyo, jina letu Mashahidi wa Yehova linaonyesha kwamba sisi ni kikundi cha Wakristo wanaotangaza kweli kumhusu Yehova, Muumba wa vitu vyote. (Ufunuo 4:11) Tunawatolea wengine ushahidi kupitia jinsi tunavyoishi na kwa kuwaeleza mambo ambayo tumejifunza kutoka kwa Biblia.—Isaya 43:10-12; 1 Petro 2:12.