Kutoka 6:1-30

  • Ahadi ya kuwekwa huru yarudiwa (1-13)

    • Jina Yehova halikujulikana kikamili (2, 3)

  • Ukoo wa Musa na Haruni (14-27)

  • Musa kufika tena mbele ya Farao (28-30)

6  Basi Yehova akamwambia Musa: “Sasa utaona mambo nitakayomtendea Farao.+ Mkono wenye nguvu utamlazimisha awaruhusu watu wangu waende zao, na mkono wenye nguvu utamlazimisha awafukuze kutoka katika nchi yake.”+  Kisha Mungu akamwambia Musa: “Mimi ni Yehova.  Nami nilikuwa nikimtokea Abrahamu, Isaka, na Yakobo kama Mungu Mweza-Yote,+ lakini kwa jina langu Yehova+ sikujitambulisha kwao.+  Pia, nilifanya agano pamoja nao kwamba nitawapa nchi ya Kanaani, nchi ambamo waliishi kama wageni.+  Sasa mimi mwenyewe nimesikia kilio cha uchungu cha Waisraeli, ambao Wamisri wanawatumikisha kama watumwa, nami ninakumbuka agano langu.+  “Kwa hiyo, waambie Waisraeli: ‘Mimi ni Yehova, nami nitawatoa kutoka chini ya mizigo ya Wamisri na kuwaokoa kutoka katika utumwa wao,+ nami nitawakomboa kwa mkono ulionyooshwa* na kwa hukumu kubwa.+  Nami nitawachukua muwe watu wangu, nami nitakuwa Mungu wenu,+ nanyi hakika mtajua kwamba mimi ni Yehova Mungu wenu anayewatoa kutoka chini ya mizigo ya Misri.  Nami nitawapeleka katika nchi niliyoapa* kwamba nitampa Abrahamu, Isaka, na Yakobo; nitawapa ninyi iwe miliki yenu.+ Mimi ni Yehova.’”+  Baadaye Musa akawapa Waisraeli ujumbe huo, lakini hawakumsikiliza Musa kwa sababu walikuwa wamevunjika moyo na kwa sababu ya utumwa wa kikatili.+ 10  Kisha Yehova akamwambia Musa: 11  “Nenda ukamwambie Farao, mfalme wa Misri, kwamba anapaswa kuwaruhusu Waisraeli waondoke katika nchi yake.” 12  Lakini Musa akamwambia Yehova: “Tazama! Waisraeli hawajanisikiliza,+ Farao atanisikilizaje mimi, mtu asiye na ufasaha?”*+ 13  Lakini Yehova akawaambia tena Musa na Haruni amri wanazopaswa kuwapa Waisraeli na pia Farao, mfalme wa Misri, ili kuwatoa Waisraeli katika nchi ya Misri. 14  Hawa ndio viongozi wa nyumba ya baba zao: Wana wa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli,+ walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi.+ Hizo ndizo koo za Rubeni. 15  Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli, mwana wa mwanamke Mkanaani.+ Hizo ndizo koo za Simeoni. 16  Haya ndiyo majina ya wana wa Lawi,+ kulingana na koo zao: Gershoni, Kohathi, na Merari.+ Lawi aliishi miaka 137. 17  Wana wa Gershoni walikuwa Libni na Shimei, kulingana na koo zao.+ 18  Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli.+ Kohathi aliishi miaka 133. 19  Wana wa Merari walikuwa Mali na Mushi. Hizo ndizo zilizokuwa koo za Walawi, kulingana na nasaba ya koo zao.+ 20  Sasa Amramu alimwoa Yokebedi, dada ya baba yake.+ Akamzalia Amramu wana hawa: Haruni na Musa.+ Amramu aliishi miaka 137. 21  Wana wa Ishari walikuwa Kora,+ Nefegi, na Zikri. 22  Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elsafani,+ na Sithri. 23  Sasa Haruni alimwoa Elisheba, binti ya Aminadabu, dada ya Nashoni.+ Akamzalia Haruni wana hawa: Nadabu, Abihu, Eleazari, na Ithamari.+ 24  Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elkana, na Abiasafu.+ Hizo ndizo zilizokuwa koo za Wakora.+ 25  Eleazari,+ mwana wa Haruni, alimwoa mmoja wa mabinti wa Putieli. Akamzalia mwana aliyeitwa Finehasi.+ Hao ndio viongozi wa koo* za Walawi, kulingana na koo zao.+ 26  Hao ndio Haruni na Musa walioambiwa na Yehova: “Watoeni Waisraeli katika nchi ya Misri, kundi kwa kundi.”*+ 27  Hao ndio waliozungumza na Farao, mfalme wa Misri, ili awaruhusu Waisraeli watoke Misri. Ilikuwa huyu Musa na Haruni.+ 28  Siku hiyo ambayo Yehova alizungumza na Musa katika nchi ya Misri, 29  Yehova alimwambia Musa: “Mimi ni Yehova. Mwambie Farao, mfalme wa Misri, kila jambo ninalokwambia.” 30  Kisha Musa akamwambia Yehova: “Tazama! sina ufasaha,* sasa Farao atanisikilizaje?”+

Maelezo ya Chini

Au “wenye nguvu.”
Tnn., “niliyoinua mkono wangu.”
Tnn., “mtu ambaye hajatahiriwa midomo?”
Yaani, ukoo wa upande wa baba.
Tnn., “kulingana na majeshi yao.”
Tnn., “sijatahiriwa midomo.”