Ufunuo kwa Yohana 4:1-11

  • Aona maono ya Yehova mbinguni (1-11)

    • Yehova akiwa ameketi kwenye kiti chake cha ufalme (2)

    • Wazee 24 kwenye viti vya ufalme (4)

    • Viumbe hai wanne (6)

4  Baada ya hayo nikaona, na tazama! mlango uliofunguliwa mbinguni, na sauti ya kwanza niliyoisikia ikizungumza nami ilikuwa kama ya tarumbeta, ikisema: “Panda uje huku, nami nitakuonyesha mambo ambayo lazima yatendeke.”  Baada ya hayo mara moja nikawa katika nguvu za roho, na tazama! kiti cha ufalme kilikuwa mahali pake mbinguni, na kulikuwa na mtu aliyeketi kwenye kile kiti.+  Na Yule aliyeketi alionekana kama jiwe la yaspi+ na jiwe jekundu lenye thamani, na kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.+  Kuzunguka kile kiti cha ufalme kulikuwa na viti vya ufalme 24, na kwenye viti hivyo vya ufalme niliona wameketi wazee 24+ waliovaa mavazi meupe, na juu ya vichwa vyao mataji ya dhahabu.  Kwenye kile kiti cha ufalme kulitokea radi+ na sauti na ngurumo;+ na kulikuwa na taa saba za moto zikiwaka mbele ya kile kiti cha ufalme, ambazo zinamaanisha zile roho saba za Mungu.+  Mbele ya kile kiti cha ufalme kulikuwa na kitu kinachofanana na bahari ya kioo,+ kama fuwele. Katikati ya kile kiti cha ufalme* na kuzunguka kile kiti kulikuwa na viumbe hai wanne+ waliojaa macho mbele na nyuma.  Kiumbe hai wa kwanza alikuwa kama simba,+ na kiumbe hai wa pili alikuwa kama ng’ombe dume mchanga,+ na kiumbe hai wa tatu+ alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na kiumbe hai wa nne+ alikuwa kama tai anayeruka.+  Kuhusu wale viumbe hai wanne, kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita; walikuwa na macho kila mahali pande zote na chini yao.+ Na mchana na usiku wanaendelea kusema: “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova*+ Mungu, Mweza-Yote, aliyekuwako na aliyeko na anayekuja.”+  Kila mara wale viumbe hai wanapompa utukufu na heshima na shukrani Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme, Yule anayeishi milele na milele,+ 10  wale wazee 24+ huanguka chini mbele za Yule anayeketi kwenye kile kiti cha ufalme na kumwabudu Yule anayeishi milele na milele, nao hutupa mataji yao mbele ya kile kiti wakisema: 11  “Unastahili, Ee Yehova* Mungu wetu, kupokea utukufu+ na heshima+ na nguvu,+ kwa sababu uliumba vitu vyote,+ na kwa sababu ya mapenzi yako vilitokea navyo vikaumbwa.”

Maelezo ya Chini

Au “Katikati pamoja na kile kiti cha ufalme.”