Isaya 43:1-28

  • Yehova awakusanya tena watu wake (1-7)

  • Miungu yashtakiwa (8-13)

    • “Ninyi ni mashahidi wangu” (10, 12)(10, 12)

  • Waachiliwa huru kutoka Babiloni (14-21)

  • “Tukutane ili tufanye kesi” (22-28)

43  Sasa hivi ndivyo anavyosema Yehova,Muumba wako, Ee Yakobo, Yule aliyekuumba, Ee Israeli:+ “Usiogope, kwa maana nimekukomboa.+ Nimekuita kwa jina lako. Wewe ni mali yangu.   Unapopita katika maji, nitakuwa pamoja nawe,+Na unapopita katika mito, haitafurika na kukufunika.+ Unapotembea katika moto, hutateketea,Wala mwali wa moto hautakuunguza.   Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wako,Mtakatifu wa Israeli, Mwokozi wako. Nimeitoa Misri kuwa fidia kwa ajili yako,Ethiopia na Seba badala yako.   Kwa sababu ulikuwa mwenye thamani machoni pangu,+Uliheshimiwa, nami nimekupenda.+ Basi nitawatoa watu badala yakoNa mataifa badala ya uhai wako.*   Usiogope, kwa maana nipo pamoja nawe.+ Nitauleta uzao wako* kutoka masharikiNa kukukusanya kutoka magharibi.+   Nitaiambia kaskazini, ‘Watoe!’+ Na kusini, ‘Usiwazuie. Walete wanangu kutoka mbali, na mabinti wangu kutoka kwenye miisho ya dunia,+   Kila mtu anayeitwa kwa jina langu+Na niliyemuumba kwa ajili ya utukufu wangu,Ambaye nimemuumba na kumtokeza.’+   Waleteni watu walio vipofu, ingawa wana macho,Na walio viziwi, ingawa wana masikio.+   Mataifa yote na yakusanyike mahali pamoja,Na watu wakusanyike pamoja.+ Ni nani kati yao anayeweza kutangaza haya? Au, je, wanaweza kutufanya tusikie mambo ya kwanza?*+ Na watoe mashahidi wao ili kuthibitisha kwamba wanasema ukweli,Au acha wasikie na kusema, ‘Ni ukweli!’”+ 10  “Ninyi ni mashahidi wangu,”+ asema Yehova,“Naam, mtumishi wangu ambaye nimemchagua,+Ili mjue na kuwa na imani kwangu*Na mwelewe kwamba mimi ni yuleyule.+ Kabla yangu hakuna Mungu aliyefanyizwa,Na baada yangu hakutakuwa na mwingine.+ 11  Mimi—mimi ni Yehova,+ na zaidi yangu hakuna mwokozi.”+ 12  “Mimi ndiye niliyetangaza na kuokoa na kujulishaKulipokuwa hakuna mungu wa kigeni miongoni mwenu.+ Basi ninyi ni mashahidi wangu,” asema Yehova, “nami ni Mungu.+ 13  Pia, mimi ni yuleyule sikuzote;+Na hakuna yeyote anayeweza kunyakua chochote kutoka mkononi mwangu.+ Ninapotenda, ni nani anayeweza kunizuia?”+ 14  Yehova, Mkombozi wenu,+ Mtakatifu wa Israeli,+ anasema hivi: “Nitatuma ujumbe huko Babiloni kwa ajili yenu na kuyashusha makomeo yote ya malango,+Na Wakaldayo, katika meli zao, watalia kwa sababu ya mateso.+ 15  Mimi ni Yehova, Mtakatifu wenu,+ Muumba wa Israeli,+ Mfalme wenu.”+ 16  Yehova anasema hivi: Yule anayetengeneza njia bahariniNa mahali pa kupita hata katika maji yenye msukosuko,+ 17  Yule anayelivuta gari la vita na farasi,+Jeshi pamoja na mashujaa hodari: “Watalala chini na hawataamka.+ Watazimwa, watazimwa mara moja kama utambi unaowaka.” 18  “Msikumbuke mambo ya kwanza,Wala msifikirie sana mambo ya zamani. 19  Tazameni! Ninatenda jambo jipya;+Hata sasa linachipuka. Je, hamlitambui? Nitatengeneza njia nyikani+Na mito jangwani.+ 20  Mnyama wa mwituni ataniheshimu,Mbwamwitu na mbuni,Kwa maana ninatokeza maji nyikani,Mito jangwani,+Ili watu wangu wanywe, naam, mchaguliwa wangu,+ 21  Watu niliojiumbiaIli watangaze sifa zangu.+ 22  Lakini hujaniita mimi, Ee Yakobo,+Kwa sababu ulichoshwa nami, Ee Israeli.+ 23  Hujaniletea kondoo kwa ajili ya dhabihu zako nzima za kuteketezwaWala kunitukuza kwa dhabihu zako. Sijakulazimisha uniletee zawadi,Wala sijakuchosha kwa kudai ubani.+ 24  Hukuninunulia utete wenye manukato kwa pesa zako,Wala hukuniridhisha kwa mafuta ya dhabihu zako.+ Badala yake, umenilemea kwa dhambi zakoNa kunichosha kwa maovu yako.+ 25  Mimi, mimi ndiye ninayeyafuta kabisa makosa*+ yako kwa ajili yangu,+Nami sitazikumbuka dhambi zako.+ 26  Nikumbushe; na tukutane ili tufanye kesi;Toa hoja zako ili kuthibitisha kwamba unasema ukweli. 27  Babu yako wa kwanza alitenda dhambi,Na wasemaji* wako mwenyewe wameniasi.+ 28  Kwa hiyo nitawatia unajisi wakuu wa mahali patakatifu,Nami nitamtoa Yakobo aangamizweNa kumfanya Israeli atukanwe.+

Maelezo ya Chini

Au “nafsi yako.”
Tnn., “Nitaileta mbegu yako.”
Labda ni mambo yatakayotokea kwanza wakati ujao.
Au “na kunitumaini.”
Au “matendo yako ya uasi.”
Labda hawa ni walimu wa Sheria.