Barua ya Kwanza ya Petro 2:1-25

  • Kuzeni hamu kwa ajili ya neno (1-3)

  • Mawe yaliyo hai yaliyojengwa kuwa nyumba ya kiroho (4-10)

  • Kuishi kama wageni katika ulimwengu (11, 12)

  • Ujitiisho unaofaa (13-25)

    • Kristo, kielelezo chetu (21)

2  Basi, acheni ubaya wote+ na udanganyifu na unafiki na wivu na masengenyo.  Kama watoto wachanga waliozaliwa hivi karibuni,+ kuzeni hamu kwa ajili ya maziwa yasiyochanganywa na kitu* ya lile neno, ili kupitia hayo mkue kufikia wokovu,+  mradi tu mmeonja na kuona kwamba Bwana ni mwenye fadhili.  Mkimjia yeye, jiwe lililo hai lililokataliwa na wanadamu+ bali lililochaguliwa na lenye thamani kwa Mungu,+  ninyi wenyewe pia kama mawe yaliyo hai mnajengwa kuwa nyumba ya kiroho+ kusudi muwe ukuhani mtakatifu, ili kutoa dhabihu za kiroho+ zenye kukubalika kwa Mungu kupitia Yesu Kristo.+  Kwa maana Andiko linasema: “Tazama! Ninaweka katika Sayuni jiwe lililochaguliwa, jiwe la pembeni la msingi lenye thamani, na yeyote anayeonyesha imani katika hilo hatakata tamaa kamwe.”*+  Kwa hiyo, yeye ni mwenye thamani kwenu, kwa sababu ninyi ni waamini; lakini kwa wale wasioamini, “jiwe ambalo wajenzi walilikataa+ limekuwa jiwe kuu la pembeni”*+  na “jiwe la kukwaza na mwamba wa kuangusha.”+ Wanajikwaa kwa sababu hawatii lile neno. Waliwekwa rasmi pia kwa kusudi hilo.  Lakini ninyi ni “jamii iliyochaguliwa, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu,+ na watu walio mali ya pekee,+ ili mtangaze kotekote sifa bora”*+ za Yule aliyewaita kutoka katika giza kuingia katika nuru yake ya ajabu.+ 10  Kwa kuwa wakati fulani ninyi hamkuwa watu, lakini sasa ninyi ni watu wa Mungu;+ hamkuwa mmeonyeshwa rehema, lakini sasa mmeonyeshwa rehema.+ 11  Wapendwa, ninawahimiza ninyi kama wageni na wakaaji wa muda+ kwamba mwendelee kujiepusha na tamaa za mwili,+ ambazo hupigana vita nanyi.*+ 12  Dumisheni mwenendo wenu ukiwa mzuri kati ya mataifa,+ ili wanapowashutumu kuwa watenda dhambi, washuhudie kwa macho yao matendo yenu mazuri+ na hivyo wamtukuze Mungu katika siku ya ukaguzi wake. 13  Kwa ajili ya Bwana jitiisheni wenyewe kwa kila kitu kilichofanywa na binadamu,*+ iwe ni kwa mfalme+ akiwa mkubwa 14  au kwa magavana wakiwa kama wametumwa naye kuwaadhibu watenda maovu lakini kuwasifu wanaotenda mema.+ 15  Kwa maana ni mapenzi ya Mungu kwamba kwa kutenda mema mnyamazishe* maneno ya kijinga ya watu wasio na akili.+ 16  Iweni kama watu huru,+ mkitumia uhuru wenu, si kama kifuniko* cha kufanya mabaya,+ bali kama watumwa wa Mungu.+ 17  Waheshimuni watu wa namna zote,+ upendeni ushirika mzima wa akina ndugu,*+ mwogopeni Mungu,+ mheshimuni mfalme.+ 18  Watumishi na wajitiishe kwa mabwana wao kwa woga unaofaa,+ si kwa wale tu walio wema na wapole, bali pia kwa wale ambao ni wagumu kupendeza. 19  Kwa maana inakubalika ikiwa mtu anavumilia taabu* na kuteseka isivyo haki kwa sababu ya dhamiri kwa Mungu.+ 20  Kwa maana kuna faida gani ikiwa mnavumilia mnapopigwa kwa kufanya dhambi?+ Lakini ikiwa mnavumilia mateso kwa sababu ya kufanya mema, jambo hilo linakubalika kwa Mungu.+ 21  Kwa kweli, mliitwa kwenye mwendo huu, kwa sababu hata Kristo aliteseka kwa ajili yenu,+ akiwaachia ninyi kielelezo ili mfuate hatua zake kwa ukaribu.+ 22  Yeye hakufanya dhambi,+ wala udanganyifu haukupatikana kinywani mwake.+ 23  Alipokuwa akitukanwa,*+ hakujibu kwa kutukana.*+ Alipokuwa akiteseka,+ hakutoa vitisho, bali alijikabidhi mkononi mwa Yule anayehukumu+ kwa uadilifu. 24  Yeye mwenyewe alichukua dhambi zetu+ katika mwili wake mwenyewe juu ya mti,+ ili tufe kuhusiana* na dhambi na tuishi kuhusiana na uadilifu. Na “kwa vidonda vyake mliponywa.”+ 25  Kwa maana mlikuwa kama kondoo wanaopotea njia,+ lakini sasa mmerudi kwa mchungaji+ na mwangalizi wa nafsi zenu.*

Maelezo ya Chini

Au “maziwa safi; maziwa halisi.”
Tnn., “hataaibika.”
Tnn., “kichwa cha pembeni.”
Yaani, sifa zake nzuri na matendo mazuri.
Au “na nafsi zenu.”
Au “shirika la kibinadamu.”
Tnn., “mzibe.”
Au “kisingizio.”
Tnn., “undugu.”
Au “ huzuni; maumivu.”
Au “akishutumiwa.”
Au “hakushutumu.”
Au “tuachane.”
Au “wa uhai wenu.”