Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

E+/taseffski/via Getty Images (Stock photo. Posed by model.)

ENDELEA KUKESHA!

Matatizo ya Afya ya Akili ya Vijana Yameongezeka Sana—Biblia Inasema Nini?

Matatizo ya Afya ya Akili ya Vijana Yameongezeka Sana—Biblia Inasema Nini?

 Jumatatu, Februari 13, 2023, Vituo vya Kuzuia na Kudhibiti Magonjwa ya Kuambukiza (CDC) nchini Marekani vilitoa ripoti kuhusu afya ya akili ya vijana nchini Marekani. Ripoti hiyo ilionyesha kwamba asilimia 40 ya wanafunzi wa shule za sekondari walikuwa na huzuni ya kuendelea au kujihisi hawafai kwa vipindi virefu.

 Dakt. Kathleen Ethier, mkurugenzi wa Kitengo cha CDC cha Afya ya Vijana Wanaobalehe na Walio Shuleni (DASH) alisema hivi: “Ingawa katika miaka 10 iliyopita tumeona mwelekeo wa kuharibika kwa afya ya akili ya vijana, kiwango cha kuzorota kwa afya ya akili ya wasichana wanaobalehe kimeongezeka. Hivi karibuni wasichana wengi zaidi wamefikiria na hata wamepanga kujiua.”

 Ripoti hiyo ilisema hivi:

  •   Zaidi ya msichana 1 kati ya 10 (asilimia 14) wamelazimishwa kufanya ngono licha ya kwamba hawakutaka. Dakt. Ethier anasema: “Hilo ni jambo lenye kuogopesha. Kati ya wasichana 10 wanaobalehe ambao wewe unawafahamu, angalau mmoja kati yao, au hata zaidi, amebakwa.”

  •   Msichana 1 kati ya 3 hivi (asilimia 30) alifikiria sana kuhusu kujiua.

  •   Wasichana 3 kati ya 5 hivi (asilimia 57) alikuwa na huzuni ya kuendelea au kujihisi hafai kwa muda mrefu.

 Takwimu hizo zinasikitisha sana. Kipindi cha ujana kinapaswa kuwa kipindi cha shangwe na furaha. Ni nini kinachoweza kuwasaidia vijana kukabiliana na mikazo wanayokumbana nayo leo? Biblia inasema nini?

Biblia inawapa vijana msaada unaofaa

 Biblia inafafanua kwa njia nzuri kipindi chenye mkazo tunachokabili leo. Inakiita “nyakati za hatari zilizo ngumu kushughulika nazo.” (2 Timotheo 3:1-5) Hata hivyo, Biblia inatoa ushauri usiopitwa na wakati unaowasaidia mamilioni ya vijana ulimwenguni kukabiliana na mikazo kwa njia inayofaa licha ya changamoto wanazokabili. Fikiria makala zifuatazo zinazotegemea Biblia.

 Msaada kwa vijana wanaokabiliana na mawazo ya kujiua

 Msaada kwa vijana wanaokabiliana na kushuka moyo, huzuni, au hisia zisizofaa

 Msaada kwa vijana wanaoonewa kihalisi au kupitia mtandao

 Msaada kwa vijana wanaosumbuliwa au kutendewa vibaya kingono

Biblia inatoa ushauri unaofaa kwa ajili ya wazazi

 Biblia pia inatoa ushauri unaofaa unaoweza kuwasaidia wazazi ili wao waweze kuwasaidia vijana wao kukabiliana na changamoto maishani. Fikiria makala zifuatazo zinazotegemea Biblia.