Hamia kwenye habari

Hamia kwenye yaliyomo

Nikabilianaje na Upweke?

Nikabilianaje na Upweke?

 Je, unajihisi ukiwa umetengwa au wewe ni mpweke? Ikiwa ndivyo, basi huenda ukahisi kama mtunga-zaburi alisema: “Mimi ni kama ndege aliye peke yake juu ya paa.” (Zaburi 102:7) Hekima iliyo katika Biblia inaweza kukusaidia kukabiliana na matatizo yanayosababishwa na upweke.

 Sitawisha uhusiano wa karibu na Mungu

 Hata ikiwa uko peke yako, unaweza kupata furaha kwa kutambua uhitaji wako wa kiroho na kujaribu kumjua Mungu. (Mathayo 5:3, 6) Unaweza kupata msaada kutoka katika vyanzo hivi bila malipo.

  •   Biblia inayopatikana kwenye mtandao ambayo ni sahihi na rahisi kusoma

  •   Masomo ya Biblia Kwenye Mtandao yanayojibu maswali muhimu zaidi maishani

  •   Video fupi zinazohusu baadhi ya mafundisho ya msingi ya Biblia

  •  Majibu ya Maswali ya Biblia”—Ni majibu ya moja kwa moja ya maswali ambayo huulizwa mara nyingi

  •  Igeni Imani Yao”—Mfululizo huu unakusaidia kuwazia masimulizi ya maisha ya wanaume na wanawake waaminifu walio katika Biblia

  •  Je, Ni Kazi ya Ubuni?”—Mfululizo huu unakusaidia kujionea jinsi uumbaji unavyovutia na unavyostaajabisha

 Soma masimulizi ya Biblia yanayotia moyo

 Maandiko haya yamewasaidia watu wengi kupata faraja. Badala ya kusoma sehemu kubwa kwa wakati mmoja, jaribu kutumia muda kutafakari kuhusu masimulizi hayo na kusali.—Marko 1:35.

 Jifunze kwa nini mambo mabaya yanatokea ulimwenguni

 Unaweza kupambana na matatizo ikiwa unajua kwa nini mambo mabaya hutokea na hatua ambazo Mungu atachukua ili kuyaondoa.—Isaya 65:17.

 Epuka kuwa na wasiwasi kupita kiasi

 Makala zifuatazo zinaweza kukusaidia kukabiliana na mkazo unaosababishwa na upweke na zitakusaidia ‘kuacha kuhangaika.’—Mathayo 6:25.

 Sitawisha urafiki na watu

 Marafiki wanaweza kukusaidia kuona mambo kwa njia tofauti na kukuletea shangwe, hata katika hali ambazo inakuwa vigumu kuzungumza nao uso kwa uso. Ikiwa huwezi kutoka nyumbani, unaweza kuwasiliana nao kwa njia ya video au kwa kuwapigia simu ili kuimarisha urafiki wenu au kujenga urafiki na watu wapya. Makala zifuatazo zinaweza kukusaidia kupata na kuwa na “rafiki wa kweli.”—Methali 17:17.

 Fanya mazoezi ya kimwili

 Biblia inakubali kwamba “mazoezi ya kimwili ni yenye faida.” (1 Timotheo 4:8) Yanaweza kukusaidia kuwa na afya nzuri ya akili hasa ikiwa wewe ni mpweke. Hata ikiwa huwezi kutoka nyumbani, huenda unaweza kufanya mambo fulani ambayo yatakuchangamsha.