Hamia kwenye habari

Hofu ya Kifo​—Unaweza Kuishindaje?

Hofu ya Kifo​—Unaweza Kuishindaje?

Jibu la Biblia

 Tuna sababu nzuri ya kuogopa kifo kama tunavyomwogopa adui na kuchukua hatua zinazofaa ili kujilinda. (1 Wakorintho 15:26) Lakini, kuogopa kifo kwa sababu ya mafundisho ya uwongo au ushirikina husababisha watu ‘watiishwe chini ya utumwa katika maisha yao yote.’ (Waebrania 2:​15) Kujua ukweli kutakuweka huru kutokana na kuogopa kifo​—hofu ambayo inaweza kuharibu shangwe yako.​—Yohana 8:​32.

Ukweli kuhusu kifo

  •   Wafu hawajui lolote. (Zaburi 146:4) Hupaswi kuogopa kwamba baada ya kufa utapata maumivu au utateseka, kwa sababu Biblia inalinganisha kifo na usingizi.​—Zaburi 13:3; Yohana 11:11-​14.

  •   Wafu hawawezi kutuumiza. Hata wale ambao walikuwa adui zetu wanakuwa “wasiojiweza katika kifo.” (Methali 21:16) Biblia inasema kwamba “chuki yao na wivu wao tayari zimepotea.”​—Mhubiri 9:6.

  •   Kifo si mwisho wa kuwepo kwetu. Mungu atawafufua wafu.​—Yohana 5:​28, 29; Matendo 24:15.

  •   Mungu anaahidi wakati “kifo hakitakuwapo tena.” (Ufunuo 21:4) Kuhusu siku hiyo, Biblia inasema: “Waadilifu wenyewe wataimiliki dunia, nao watakaa milele juu yake,” wakiwa huru kabisa na bila hofu ya kifo.​—Zaburi 37:29.