Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 25

Juu ya Nini Tunajenga Majumba ya Ufalme na Ni Nini Inatusaidia Kuijenga?

Juu ya Nini Tunajenga Majumba ya Ufalme na Ni Nini Inatusaidia Kuijenga?

Bolivia

Nigeria, mbele ya ujenzi na kisha ujenzi

Tahiti

Kama vile jina Jumba la Ufalme linaonyesha, fundisho kubwa la Biblia lenye kuzungumuziwa sana mule ni Ufalme wa Mungu. Ile njo habari kubwa yenye Yesu alizungumuzia sana mu mahubiri yake.​—Luka 8:1.

Ni nafasi kwenye ibada ya kweli inafanywa mu eneo. Ku Jumba la Ufalme njo kwenye mipango ya kazi ya kuhubiri habari njema inafanywa. (Matayo 24:14) Majumba ya Ufalme haina ukubwa uleule na haijengwe namna moja. Haiko majengo makubwa-makubwa sana na haipambwe kwa namna ya kushangaza. Kutaniko moja ao makutaniko mingi inaweza kuchangia Jumba moja la Ufalme. Mu miaka ya hivi majuzi, tumejenga maelfu ya Majumba ya mupya ya Ufalme (karibu Majumba ya Ufalme tano kila siku) kwa sababu makutaniko inaendelea kuongezeka na wahubiri pia wanaendelea kuongezeka. Feza za kufanya ile kazi yote zinatokaka wapi?​—Matayo 19:26.

Inajengwa kupitia michango ya feza yenye kutolewa juu ya ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Feza hizo zinatumwa ku biro ya tawi ili makutaniko yenye kuwa na lazima ya kujenga ao kutengeneza upya Jumba la Ufalme itumie feza hizo.

Inajengwa na ndugu wa hali zote wenye wanajitolea kufanya kazi bila kulipwa. Mu inchi za mingi kuko Vikundi vya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Vikundi vya wajenzi na ndugu na dada wenye kujitolea wanafanya kazi ya kujenga Majumba ya Ufalme. Wakati wanamaliza Jumba moja wanaenda kujenga Jumba lingine katika inchi ileile ili kusaidia makutaniko kujenga Majumba yao ya Ufalme. Wanaenda hata katika maeneo ya vijiji vya mbali. Mu inchi zingine, Mashahidi wenye kustahili wamewekwa ili kusimamia kazi ya kujenga na kutengeneza upya Majumba ya Ufalme katika eneo fulani. Hata kama ndugu wengi wa eneo hilo wenye kuwa na ufundi wanajitolea kabisa ili kusaidia wakati wa ujenzi, ndugu na dada wa kutaniko njo wanafanya kazi kubwa. Ile kazi yote inawezekana kupitia roho ya Yehova na bidii yenye watu wa Mungu wanaonyesha kwa nafsi yote.​—Zaburi 127:1; Wakolosai 3:23.

  • Juu ya nini nafasi yetu ya ibada inaitwa Jumba la Ufalme?

  • Ni nini inafanya tuweze kujenga Majumba ya Ufalme mu dunia yote?