Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 15

Wazee wa Kutaniko Wanafanyaka Kazi Gani?

Wazee wa Kutaniko Wanafanyaka Kazi Gani?

Finlandi

Kazi ya kufundisha

Kazi ya uchungaji

Kazi ya kuhubiri

Katika tengenezo letu hakuna viongozi wa dini wenye wanalipwa mushahara juu ya kazi yenye wanafanya. Lakini, kama vile ilikuwa wakati kutaniko la Kikristo lilianza, wanaume wenye kutimiza sifa zenye kuombwa katika Biblia wanawekwa ili “kuchunga kutaniko la Mungu.” (Matendo 20:28) Wazee hao ni wanaume wenye kukomaa kiroho wenye wanaongoza na kuchunga kutaniko, “hapana kwa kulazimishwa, lakini kwa kupenda mbele ya Mungu; hapana kwa kupenda faida yenye haiko ya haki, lakini kwa hamu.” (1 Petro 5:1-3) Wanafanya kazi gani kwa faida yetu?

Wanatuhangaikia na kutulinda. Wazee wanaongoza kutaniko na wanasaidia watu wote mu kutaniko waendelee kuwa na urafiki muzuri pamoja na Yehova. Juu wanajua kama Mungu njo amewapatia daraka hilo la maana, wazee hawatawale watu wa Mungu, lakini wanatusaidia tukuwe na hali ya muzuri na tukuwe na furaha. (2 Wakorinto 1:24) Kama vile muchungaji anahangaikia kwa bidii kila kondoo wa kundi lake, wazee pia wanajikaza ili kujua kila ndugu na dada mu kutaniko.​—Mezali 27:23.

Wanatufundisha namna ya kufanya mapenzi ya Mungu. Kila juma, wazee wanaongoza mikutano ya kutaniko ili kutia nguvu imani yetu. (Matendo 15:32) Wanaume hao wenye bidii wanaongoza pia kazi ya kuhubiri, wanahubiri pamoja na sisi na wanatuzoeza mu kila sehemu ya mahubiri.

Wanatutia moyo. Ili kutusaidia tukuwe na urafiki muzuri pamoja na Yehova, wazee wanaweza kututembelea ku nyumba ao kuzungumuza na sisi ku Jumba la Ufalme ili kutusaidia na kutufariji kupitia Maandiko.​—Yakobo 5:14, 15.

Zaidi ya kazi yenye wanafanya mu kutaniko, wazee wengi wako na kazi za kimwili na madaraka ya familia, wanapaswa pia kutumia wakati ili kuhangaikia ile mambo. Kwa sababu ndugu hao wanafanya kazi kwa bidii, wanastahili heshima yetu.​—1 Watesalonike 5:12, 13.

  • Wazee wanafanyaka kazi gani mu kutaniko?

  • Namna gani wazee wanahangaikia kila mumoja wetu?