Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 5

Kama Unakuja ku Mikutano Yetu Utapata Faida Gani?

Kama Unakuja ku Mikutano Yetu Utapata Faida Gani?

Argentina

Sierra Leone

Belgique

Malesia

Watu wengi wameacha kuenda ku ibada ya dini zao, juu wakati wanaenda kule hawapate majibu ya maulizo ya maana yenye wanajiulizaka mu maisha na hawapate kitulizo. Basi, juu ya nini unapaswa kuja ku mikutano ya Mashahidi wa Yehova? Kama unakuja ku mikutano hiyo utapata faida gani?

Utapata furaha kwa sababu utakuwa kati ya watu wenye wanakupenda na kukuhangaikia. Wakati wa mitume, Wakristo walipangwa mu makutaniko mbalimbali, na walikuwa wanafanya mikutano ili kumuabudu Mungu, kujifunza Maandiko, na kutiana moyo. (Waebrania 10:24, 25) Kwa sababu walionyeshana upendo ku mikutano, walijisikia kuwa kati ya marafiki wa kweli, ni kusema, ndugu na dada zao Wakristo. (2 Watesalonike 1:3; 3 Yohana 14) Na sisi tunafuata mufano wao, na tunapata furaha kama wao.

Utajifunza namna ya kutumia kanuni za Biblia mu maisha yako. Kama vile ilikuwa wakati wa zamani, wanaume, wanamuke, na watoto wanakusanyika wote pamoja. Walimu wenye kustahili wanatumia Biblia ili kutusaidia kujua namna ya kutumia kanuni za Biblia mu maisha yetu ya kila siku. (Kumbukumbu la Torati 31:12; Nehemia 8:8) Kila mutu anaweza kuimba, na kutoa majibu kama habari inaomba kutoa majibu. Kwa kufanya vile, tunazungumuzia tumaini letu la Kikristo.​—Waebrania 10:23.

Imani yako katika Mungu itatiwa nguvu. Mutume Paulo aliandikia kutaniko moja la wakati wake hivi: “Ninatamani sana kuwaona ninyi, ili . . . tukuwe na ubadilishanaji wa kitia-moyo, kila mumoja kupitia imani ya mwenzake, yenu na yangu pia.” (Waroma 1:11, 12) Kukusanyika pamoja na ndugu na dada zetu kila mara kunafanya imani yetu ikuwe yenye nguvu na kunafanya tujikaze kufuata kanuni za Biblia mu maisha yetu.

Basi, tunakualika ukuje ku mikutano yetu ili ujionee ile mambo. Tutakukaribisha ao kukupokea kwa furaha. Kuingia ni bure na hatuombake watu watoe sadaka.

  • Tunafuata mufano gani juu ya namna tunafanyaka mikutano yetu?

  • Mikutano yetu inatuletea faida gani?