Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 02

Biblia Inatupatia Tumaini

Biblia Inatupatia Tumaini

Mu dunia yote watu wako wanapata magumu yenye inafanya wakuwe na huzuni, mahangaiko, na hata maumivu. Na weye ulishakapata magumu ya vile? Pengine uko unateseka juu ya magonjwa ao juu mutu fulani mwenye unapendaka alikufa. Unaweza kujiuliza hivi: ‘Kuko siku maisha itakuwaka muzuri?’ Biblia iko na jibu ya ile ulizo. Na ile jibu inaweza kukupatia tumaini.

1. Namna gani Biblia inatusaidia tukuwe na tumaini?

Biblia inaonyesha juu ya nini mu dunia muko magumu mingi. Zaidi ya ile, inaonyesha kama ile magumu inakaribia kuisha. Mambo yenye Biblia inasema juu ya “wakati wenye kuja” inaweza kutupatia “tumaini.” (Soma Yeremia 29:11, 12.) Tena, inaweza kutusaidia tuvumilie magumu, tukuwe na furaha leo, na tutumainie kama tutakuwa na furaha milele.

2. Biblia inasema kama maisha itakuwa namna gani mu siku zenye ziko nakuya?

Biblia inasema kama mu siku zenye ziko nakuya “kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.” (Soma Ufunuo 21:4.) Leo, kuko mambo mingi yenye inafanyaka watu wakose tumaini. Kwa mufano, umaskini, ukosefu wa haki, magonjwa, na kifo. Lakini, ile magumu yote itaisha. Biblia inasema kama watu wataishi milele mu Paradiso ku dunia.

3. Unaweza kufanya nini juu uamini kama mambo yenye Biblia inasema kuwa itafanyika mu siku zenye ziko nakuya ni ya kweli?

Watu wengi wanatumaini mambo ya muzuri ifanyike. Hata vile, hawawezi kuwa hakika kama ile mambo itafanyikaka. Lakini, haiko vile juu ya Biblia. Mambo yenye inasema itafanyika kabisa. ‘Kuchunguza Maandiko kwa uangalifu’ kunaweza kutusaidia tuamini kama mambo yenye Biblia inasema kuwa itafanyika mu siku zenye ziko nakuya ni ya kweli. (Matendo 17:11) Wakati utaendelea kujifunza Biblia, utajiamulia kama utaamini ao hapana mambo yenye Biblia inasema kuwa itafanyika mu siku zenye ziko nakuya.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone mambo fulani yenye Biblia inasema juu ya namna maisha itakuwa mu siku zenye ziko nakuya. Na tuone namna tumaini yenye Biblia inatoa iko inasaidia watu leo.

4. Biblia inasema kama watu watakuwa na maisha ya muzuri sana na wataishi milele

Hapa chini kuko mambo mbalimbali yenye Biblia inasema kama itafanyika mu siku zenye ziko nakuya. Ni ya wapi njo inakufurahisha sana? Juu ya nini?

Musome maandiko yenye iko pembeni ya ile mambo, na muzungumuzie hii maulizo:

  • Hii maandiko inaonyesha kama maisha itakuwa namna gani? Unawaza mambo yenye ile maandiko inasema inaweza kusaidia watu wa familia yako na marafiki wako wakuwe na tumaini?

Wazia uko unaishi mu dunia yenye

HAKUNA MUTU MWENYE . . .

KILA MUTU . . .

  • atasikia maumivu, atazeeka, ao kufa.​—Isaya 25:8.

  • ataona wapendwa wake wanafufuliwa juu waishi tena ku dunia.​—Yohana 5:28, 29.

  • atakuwa na afya ya muzuri na nguvu mingi.​—Yobu 33:25.

  • atakuwa na mawazo yenye kuhuzunisha.​—Isaya 65:17.

  • ataishi milele na atakuwa na maisha ya muzuri.​—Zaburi 37:29.

5. Kuamini mambo yenye Biblia inasema kuwa itafanyika mu siku zenye ziko nakuya kunaweza kukusaidia

Magumu mingi yenye kuwa mu dunia inafanya watu wengi wavunjike moyo na hata wakasirike. Watu fulani wanajikaza sana juu ya kumaliza magumu. Ona namna kujua kama maisha itakuwa muzuri mu siku zenye ziko nakuya kunasaidia watu leo. Muangalie VIDEO, na kisha muzungumuzie maulizo yenye iko hapa chini.

  • Vile uliona mu video, ni mambo gani ya ukosefu wa haki yenye ilikuwa inahangaisha Rafika?

  • Hata kama mambo ya kukosa haki yenye alikuwa anaona haikuisha, namna gani Biblia ilimusaidia?

Kuamini mambo yenye Biblia inasema kama itafanyika mu siku zenye ziko nakuya kunaweza kutusaidia tupiganishe hali ya kuvunjika moyo na tukuwe na furaha hata kama tuko na magumu. Musome Mezali 17:22 na Waroma 12:12, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Unawaza kama kuamini mambo yenye Biblia inasema kuwa itafanyika mu siku zenye ziko nakuya kunaweza kukusaidia? Juu ya nini unawaza vile?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mambo yenye Biblia inasema kama itafanyika mu siku zenye ziko nakuya ni ndoto tu.”

  • Juu ya nini unawaza kama ni muzuri uchunguze juu ujionee kama ile mambo ni ya kweli?

KWA KIFUPI

Biblia inasema kama maisha itakuwa muzuri mu siku zenye ziko nakuya. Ile inatupatia tumaini na inatusaidia tuvumilie magumu yetu.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Juu ya nini watu wako na lazima ya tumaini?

  • Biblia inasema maisha itakuwa namna gani mu siku zenye ziko nakuya?

  • Kuamini mambo yenye Biblia inasema kama itafanyika mu siku zenye ziko nakuya kunaweza kukusaidia namna gani leo?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ona namna kuwa na tumaini kunaweza kukusaidia wakati wa magumu.

“Unaweza Kupata Wapi Tumaini?” (Amuka!, 22 Mwezi wa 4, 2004)

Ona namna kutumaini kama mambo itakuwa muzuri kunaweza kusaidia wenye kuwa na ugonjwa wa siku mingi.

“Je, Biblia Inaweza Kukusaidia Ikiwa Una Ugonjwa wa Siku Nyingi?” (Inapatikana ku Enternete)

Wakati uko unaangalia hii video ya muziki, wazia weye na familia yako muko munafurahia maisha mu Paradiso yenye Biblia inazungumuzia.

Wazia ile Siku (3:37)

Ona namna kujifunza mambo yenye Biblia inasema kama Mungu atafanya, kulibadilisha maisha ya mutu mwenye alikuwa anapenda sana mu dunia mukuwe mabadiliko.

“Sijisikie Tena Kuwa Ninapaswa Kubadilisha Dunia” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 7, 2013)