Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO YA 03

Unaweza Kuamini Mambo Yenye Biblia Inasema?

Unaweza Kuamini Mambo Yenye Biblia Inasema?

Biblia inazungumuzia mambo mingi yenye Mungu atafanya na iko na mashauri ya mingi. Pengine unapenda kujua mambo yenye Biblia inafundisha, lakini uko na mashaka. Unaweza kuamini mambo yenye Biblia inasema hata kama iliandikwaka zamani? Biblia inaweza kukusaidia kabisa leo? Na unawaza mambo yenye Biblia inasema kama itafanyika mu siku zenye ziko nakuya ni ya kweli? Watu wengi wanajibiaka ndiyo ku ile maulizo yote. Tuone mambo fulani yenye inaweza kukusaidia uamini mambo yenye Biblia inasema.

1. Mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli ao ni ya kuwazia-wazia?

Biblia inasema kama iko na “maneno ya kweli yenye hayana makosa.” (Muhubiri 12:10) Inazungumuzia habari za kweli za watu wenye waliishi kabisa. (Soma Luka 1:3; 3:1, 2.) Watu wengi wenye kujifunza historia na wenye kuchimbula vitu vya zamani, wamepata mambo yenye kuonyesha kama mambo yenye Biblia inasema juu ya tarehe mbalimbali, watu, maeneo, na matukio mbalimbali ni ya kweli.

2. Juu ya nini tunaweza kusema kama Biblia ingali na faida leo?

Mara mingi, Biblia ilisema mambo yenye watu walivumbula kisha miaka mingi. Kwa mufano, inazungumuzia mambo fulani ya sayansi. Wakati Biblia iliandikwa, mawazo yenye watu wengi walikuwa nayo ilikuwa tofauti na mambo yenye Biblia inasema. Lakini, mambo yenye watu wenye kujifunza sayansi wamevumbula inaonyesha kabisa kama Biblia inasemaka kweli. Mambo yenye Biblia inasema “yanategemeka sikuzote, sasa na milele.”​Zaburi 111:8.

3. Juu ya nini tuamini mambo yenye Biblia inasema kuwa itatokea?

Mu Biblia muko maunabii * yenye inazungumuzia “mambo yenye bado hayajafanywa.” (Isaya 46:10) Kuko mambo mingi yenye Biblia ilisemaka kama itafanyika. Na ilifanyikaka vilevile hata kama kulikuwa kulishapita miaka mingi. Tena, Biblia ilizungumuziaka waziwazi hali zenye ziko leo. Mu hii somo, tutachunguza maunabii fulani ya Biblia. Utaona namna ilitimiaka kabisa-kabisa!

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna mambo yenye watu wenye kujifunza sayansi wamevumbula inapatana na Biblia, na tuchunguze maunabii fulani ya Biblia yenye kushangaza.

4. Sayansi inapatana na Biblia

Zamani, watu wengi waliamini kama dunia inaikala juu ya kitu fulani. Muangalie VIDEO.

Ona mambo yenye iliandikwa mu kitabu ya Yobu miaka 3500 hivi yenye imepita. Musome Yobu 26:7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Juu ya nini inashangaza kuona kama Biblia inasema kuwa dunia iko “mahali kwenye hakuna kitu”?

Ni mu miaka ya 1800 njo watu walifikia kuelewa muzuri namna maji inafanyaka muzunguko kati ya dunia na anga. Lakini, ona mambo yenye Biblia ilikuwaka ilishasema zamani. Musome Yobu 36:27, 28, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Nini njo inakushangaza wakati unasoma namna Biblia inazungumuzia kwa njia ya mwepesi namna maji inafanyaka muzunguko kati ya dunia na anga?

  • Maandiko yenye tumetoka kusoma imekusaidia uamini zaidi mambo yenye Biblia inasema?

5. Biblia ilisema mbele ya wakati mambo yenye ingetokea

Musome Isaya 44:27–​45:2, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Biblia ilisemaka nini miaka 200 mbele Babiloni iharibiwe?

Historia inahakikisha kama Koreshi, mufalme wa Uajemi, pamoja na jeshi yake walikamata muji wa Babiloni mu mwaka wa 539 M.K.Y. * Waligeuza njia ya maji ya muto wenye ulikuwa unalinda Babiloni. Walikuta milango ya muji iko wazi. Kwa hiyo, wakaingia na kukamata muji bila kupigana. Leo, miaka zaidi ya 2500 tangu ile mambo itendeke, Babiloni ingali mabomoko. Tuone sasa mambo ingine yenye Biblia ilisemaka itatokea.

Musome Isaya 13:19, 20, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani ile unabii ilitimia?

Mabomoko ya Babiloni mu Iraki ya leo

6. Biblia ilisema mbele ya wakati mambo yenye tuko tunaona leo

Biblia inaita hii wakati yenye tunaishi kuwa “siku za mwisho.” (2 Timoteo 3:1) Ona mambo yenye Biblia ilisemaka kama ingetokea mu hii wakati.

Musome Matayo 24:6, 7, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Biblia ilisema kama ni mambo gani ingetokea mu siku za mwisho?

Musome 2 Timoteo 3:1-5, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Biblia ilisema kama watu wangekuwa na tabia gani mu siku za mwisho?

  • Ni tabia gani zenye weye uko unajionea?

WATU FULANI WANASEMAKA: “Mu Biblia muko tu hadisi za kuwazia-wazia.”

  • Nini njo inakufanya uamini kabisa kama mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli?

KWA KIFUPI

Historia, sayansi, na maunabii, ile yote inaonyesha kama unaweza kuamini mambo yenye Biblia inasema.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Mambo yenye Biblia inasema ni ya kweli ao ni ya kuwazia-wazia?

  • Ni mu mambo gani fulani sayansi inapatana na Biblia?

  • Unawaza kama Biblia inaweza kutuambia mambo yenye itatokea mu siku zenye ziko nakuya? Juu ya nini unawaza vile?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Ni kweli mu Biblia muko makosa vile sayansi inaonyesha?

“Sayansi Inapatana na Biblia?” (Inapatikana ku Enternete)

Ona namna mambo yenye Biblia ilisemaka juu ya Utawala wa Ugiriki ilitimiaka.

‘Maneno ya Manabii’ Yanatutia Nguvu (5:22)

Ona namna maunabii ya Biblia ilibadilisha mawazo yenye mwanaume fulani alikuwa nayo kuhusu Biblia.

“Kwangu Mimi, Hakukuwa Mungu” (Munara wa Mulinzi Na. 5 2017)

^ fu. 9 Unabii ni mambo yenye Mungu anasema, kwa mufano mambo yenye anasema kama itatokea mu siku zenye ziko nakuya.

^ fu. 25 M.K.Y. maana yake “Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu,” na K.K.Y. maana yake “Kisha Kuzaliwa kwa Yesu.”