Ona video zinazopatikana

Je, Biblia Inaweza Kukusaidia Ikiwa Una Ugonjwa wa Siku Nyingi?

Je, Biblia Inaweza Kukusaidia Ikiwa Una Ugonjwa wa Siku Nyingi?

Jibu la Biblia

 Ndiyo. Mungu anawahangaikia watumishi wake walio wagonjwa. Kuhusu mutumishi mwaminifu wa Mungu, Biblia inasema hivi: ‘Yehova mwenyewe atamutegemeza katika kitanda cha ugonjwa.’ (Zaburi 41:3) Ikiwa una ugonjwa fulani wa siku nyingi, mambo matatu yanayofuata yanaweza kukusaidia:

  1.   Muombe Mungu akupatie nguvu ya kuvumilia. Unaweza kupokea “amani ya Mungu yenye ubora unaozidi fikira zote,” ambayo itapunguza kufazaika kwako na kukusaidia kuvumilia.​—Wafilipi 4:6, 7.

  2.   Tazamia mema. Biblia inasema hivi: “Moyo wa furaha ni dawa nzuri. Lakini roho inayovunjika inakausha mifupa.” (Methali 17:22, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Uwe mutu mwenye kuchekesha wengine wakati fulani, kwa sababu kufanya hivyo kunaweza kukutuliza na kukusaidia uwe na afya nzuri.

  3.   Tumainia wakati ujao. Tumaini nzuri linaweza kukusaidia uwe na furaha ijapokuwa magonjwa ya siku nyingi. (Waroma 12:12) Biblia inazungumuzia wakati ambapo “hakuna mukaaji atakayesema, ‘Mimi ni mugonjwa.’” (Isaya 33:24) Wakati huo Mungu ataponyesha magonjwa yote ya siku nyingi ambayo sayansi ya leo imeshindwa kuponyesha. Kwa mufano, Biblia inaonyesha kwamba watu wenye kuzeeka watakuwa vijana na wenye afya nzuri: “Nyama yake na iwe laini kuliko wakati wa ujana; na arudi kwenye siku za nguvu za ujana wake.”​—Ayubu 33:25.

 Usisahau jambo hili: Mashahidi wa Yehova wanatafuta pia matunzo kwa ajili ya magonjwa ya siku nyingi, hata ikiwa wanajua namna Mungu anavyosaidia watu. (Marko 2:17) Hata hivyo, sisi Mashahidi wa Yehova, hatuwatie watu moyo wakubali matunzo fulani, tunajua kwamba kila mutu anapaswa kujiamulia kuhusu jambo hilo.