Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

HABARI KUBWA | MUNGU ANAONA VITA NAMNA GANI?

Namna Mungu Anaona Vita Leo

Namna Mungu Anaona Vita Leo

Leo watu wanaonewa. Watu wengi wanamulilia Mungu tena na tena ili awasaidie na wanajiuliza kama watapata musaada siku fulani. Mungu anasikiliza vilio vyao vya kuomba musaada? Tuseme nini juu ya watu wenye wanapigana vita ili wasiendelee kuonewa? Mungu anaunga mukono bidii yao na kuona kama wako na haki ya kupigana vita?

Har-Magedoni ni vita yenye itamaliza vita zote

Kwanza, unaweza kutulizwa kwa kujua jambo hili: Mungu anaona mateso yenye kuwa katika dunia leo, na anakusudia kufanya jambo fulani. (Zaburi 72:13, 14) Katika Neno lake, Biblia, Mungu anaahidi kama watu wenye kuteseka watapata kitulizo. Wakati gani? ‘Wakati wa ufunuo wa Bwana Yesu kutoka mbinguni pamoja na malaika zake wenye nguvu . . . anapoleta kisasi juu ya wale wasiomujua Mungu na wale wasiotii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.’ (2 Wathesalonike 1: 7, 8) Ufunuo huo wa Yesu utatokea wakati unaokuja kwenye vita yenye Biblia inaita ‘vita vya ile siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.’ Vita hiyo inaitwa pia Har-Magedoni.—Ufunuo 16:14, 16.

Katika vita hiyo ya wakati unaokuja, Mungu hatatumia wanadamu ili kupigana vita na watu wabaya, lakini atatumia Mwana wake, Yesu Kristo, pamoja na malaika wenye nguvu. Majeshi hayo ya mbinguni yatamaliza matendo yote ya kuonea wengine.—Isaya 11:4; Ufunuo 19:11-16.

Mupaka leo, mawazo ya Mungu juu ya vita hayajabadilika. Anaendelea kuona vita kuwa njia ya haki ya kumaliza matendo ya kuonea wengine na ya ubaya. Lakini, kama vile ilikuwa tangu zamani, ni Mungu mwenyewe ndiye ana haki ya kuamua ni wakati gani vita kama hiyo inapaswa kupiganwa na ni nani anapaswa kupigana. Kama vile tumekwisha kuona, Mungu ameamua kama vita yenye itamaliza ubaya na kulipizia kisasi watu wenye kuonewa, ni vita yenye itapiganwa wakati unaokuja na itapiganwa na Mwana wake, Yesu Kristo. Hilo linamaanisha kama Mungu hakubali vita zenye watu wanapigana leo, hata kama inaonekana kuwa wako na sababu ya muzuri ya kufanya hivyo.

Kwa mufano: Fikiria ndugu wawili wenye wanaanza kupigana wakati baba yao haiko. Wanaacha kupigana kwa muda kidogo na wanaita baba yao kwenye telefone. Mumoja anasema kama ni ndugu yake ndiye alianza kumupiganisha, na mwengine anasema kama mwenzake alikuwa anamutendea mubaya. Wote wanamuelezea baba yao, na kila mumoja anatumainia kama baba atamuunga mukono. Lakini, kisha kuwasikiliza wote wawili, baba yao anawaambia waache kupigana na wamungojee mupaka wakati atarudia nyumbani ili kumaliza tatizo lao. Ndugu hao wawili wanavumilia kidogo. Bila kukawia, wanaanza kupigana tena. Wakati baba yao anarudia nyumbani, hafurahie namna kila mutoto alitenda na anawapatia malipizi kwa sababu wote wawili hawakumutii.

Leo, mataifa yenye kupigana vita yanamulilia Mungu ili kupata musaada. Lakini Mungu haunge mukono vita yoyote yenye kutokea leo. Katika Neno lake, Biblia, anasema waziwazi hivi: ‘Musimulipe yeyote uovu kwa uovu,’ na ‘Musijilipizie kisasi wenyewe.’ (Waroma 12:17, 19) Zaidi ya hiyo, anajulisha watu kama wanapaswa ‘kumungojea kwa kutamani’ ili achukue hatua wakati wa Har-Magedoni. (Zaburi 37:7) Wakati mataifa yanakosa kumungojea Mungu atende na yanaamua kupigana vita, anaona vita hizo kuwa ni matendo ya kimbelembele ya jeuri yenye kumuchukiza. Kwa hiyo, kwenye vita ya Har-Magedoni, Mungu ataonyesha hasira yake na kumaliza kabisa ugomvi kati ya mataifa kwa ‘kukomesha vita mupaka kwenye mwisho wa dunia.’ (Zaburi 46:9; Isaya 34:2) Kwa kweli, Har-Magedoni ni vita yenye itamaliza vita zote.

Kumalizika kwa vita ni kati ya baraka nyingi za Ufalme wa Mungu. Yesu alizungumuzia serikali hiyo katika sala hii yenye kujulikana sana: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 6:10) Ufalme wa Mungu utamaliza vita na pia jambo lenye kuleta vita, ni kusema, ubaya. * (Zaburi 37:9, 10, 14, 15) Haishangaze kuona kuwa wanafunzi wa Yesu wanangojea kwa hamu baraka za Ufalme wa Mungu.—2 Petro 3:13.

Hata hivyo, ni lazima tungojee mupaka wakati gani ili Ufalme wa Mungu umalize mateso yote, matendo yote ya kuonea wengine, na ubaya wote? Utimizo wa unabii mbalimbali wa Biblia unaonyesha kama tunaishi katika “siku za mwisho” za ulimwengu huu. (2 Timotheo 3:1-5) * Hivi karibuni, Ufalme wa Mungu utamaliza siku hizi za mwisho kupitia vita ya Har-Magedoni.

Kama vile tumekwisha kuona, watu wenye wataharibiwa kwenye vita hiyo ya mwisho ni wale wenye wanakataa ‘kutii habari njema juu ya Bwana wetu Yesu.’ (2 Wathesalonike 1:8) Lakini, usisahau kama Mungu hafurahie kifo cha mutu yeyote, hata kifo cha mutu mubaya. (Ezekieli 33:11) Kwa sababu “hataki yeyote aangamizwe” katika vita hiyo ya mwisho, leo anahakikisha kuwa habari njema juu ya Bwana wetu Yesu ‘inahubiriwa katika dunia yote inayokaliwa ili kuwa ushahidi kwa mataifa yote’ mbele mwisho ufike. (2 Petro 3:8, 9; Mathayo 24:14; 1 Timotheo 2:3, 4) Kwa kweli, kupitia kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova katika dunia yote, watu leo wanapata nafasi ya kumujua Mungu, kutii habari njema juu ya Yesu, na kuokoka ili kuona siku yenye hakutakuwa tena vita.

^ fu. 9 Ufalme wa Mungu utaondoa pia kifo, adui wa wanadamu. Kama vile inaonyeshwa katika habari yenye kuwa kwenye ukurasa wa 16, Mungu atafufua watu wengi sana, hata watu wengi wenye walikufa kwa sababu ya vita.

^ fu. 10 Ili kupata habari zingine juu ya siku za mwisho, soma sura ya 9 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? chenye kilichapishwa na Mashahidi wa Yehova.