Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

Ulijua?

Ulijua?

Sababu gani Yosefu alikata ndevu mbele ya kuenda kuonana na Farao?

Muchoro wa Zamani wa Wamisri Kwenye Ukuta Unaoonyesha Mutu Anayekata Nywele

Kulingana na kitabu cha Mwanzo, Farao aliamuru kama Yosefu, mufungwa Muebrania, aletwe haraka mbele yake ili aeleze maana ya ndoto zake zenye zilimusumbua. Wakati huo, Yosefu alikuwa amefungwa kwa miaka mingi. Hata kama Farao alimuita haraka, Yosefu alichukua wakati wa kukata ndevu. (Mwanzo 39:20-23; 41:1, 14) Kwa sababu muandikaji alitaja jambo hilo lenye kuonekana kuwa halina maana, hilo linaonyesha kama alijua muzuri desturi za Wamisri.

Kuacha ndevu zikomae lilikuwa jambo la kawaida kwa mataifa mengi ya zamani, na hata kwa Waebrania. Tofauti na hilo, kitabu kimoja cha McClintock na Strong kinasema kama, “Wamisri wa zamani ndio tu taifa la Mashariki lenye lilipinga kukomalisha ndevu.” (Cyclopedia of Biblical, Theological, and Ecclesiastical Literature)

Iliomba mutu akate ndevu tu? Gazeti moja linasema kama, desturi za sherehe za Wamisri ziliomba mwanaume ajitayarishe ili kuingia mbele ya Farao kama vile alipaswa kujitayarisha mbele ya kuingia katika hekalu. (Biblical Archaeology Review) Katika hali hiyo, Yosefu alipaswa kukata nywele zote kwenye kichwa chake na kwenye mwili wake.

Kitabu cha Matendo kinaonyesha kama baba ya Timotheo alikuwa Mugiriki. Hilo linamaanisha kama alitokea Ugiriki?

Haiko lazima. Katika maandishi yake yenye yaliongozwa na roho ya Mungu, wakati fulani mutume Paulo alionyesha tofauti kati ya Wayahudi na Wagiriki, alitumia neno Wagiriki ili kumaanisha watu wote wenye hawakukuwa Wayahudi. (Waroma 1:16; 10:12) Kwa kweli, sababu moja yenye ilimusukuma Paulo kufanya hivyo, ilikuwa kwa sababu luga ya Kigiriki na desturi za Wagiriki zilikuwa zinatumiwa sana katika maeneo yenye alihubiri.

Ni nani watu wa zamani waliona kuwa Mugiriki? Kati ya mwaka wa 301 na 400 mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, Isocrate, musemaji wa Athene, alijivunia juu ya namna desturi za Wagiriki zilikuwa zinaenea katika ulimwengu. Juu ya matokeo ya jambo hilo, alisema hivi: “Watu wenye wamepata faida kupitia elimu yetu wanaitwa Wagiriki hata kama hawako wazaliwa wa Ugiriki.” Hata kama hatuwezi kuhakikisha, inawezekana baba ya Timotheo mwenye hakukuwa Muyahudi na wengine wenye Paulo anaita kuwa Wagiriki, walikuwa Wagiriki kulingana na desturi lakini hawakukuwa Wagiriki wa kizalikio.—Matendo 16:1.