Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

BIBLIA INABADILISHA MAISHA YA WATU

Niliwaza Nilikuwa Ninafurahia Maisha Yangu Kabisa

Niliwaza Nilikuwa Ninafurahia Maisha Yangu Kabisa
  • ALIZALIWA MWAKA WA: 1982

  • INCHI: POLANDI

  • ALIKUWA : MWENYE KUPENDA JEURI, DAWA ZA KULEWESHA, NA KAZI YA MUZURI

MAISHA YANGU YA ZAMANI:

Nilizaliwa katika muji fulani mudogo wa Polandi, karibu na mupaka wa Ujerumani. Kwa sababu muji wetu ulizungukwa na mashamba na mapori, nilikuwa na maisha ya amani. Wazazi wangu wenye upendo walinitia moyo nikuwe mutu muzuri, nitumike muzuri kwenye masomo, na kutafuta kazi ya muzuri.

Matatizo yangu yalianza wakati nilienda kujifunza sheria kwenye masomo ya juu katika muji wa Wrocław. Kwa sababu nilikuwa mbali na wazazi wangu, nilichagua marafiki wabaya. Sikuzote, nilikuwa ninafurahia muchezo wa kabumbu, lakini kwa kuchochewa na marafiki wangu wapya, nilifikia kupenda sana muchezo huo. Timu yenye nilipenda sana ilitokea Warsaw, na kila Siku ya Posho na Siku ya Yenga niliwafuata mahali popote walikuwa wanacheza. Katika safari hizo, tulikunywa pombe sana, tulitumia dawa za kulewesha, na wakati fulani tulipigana na watu wenye waliunga mukono timu ingine. Niliona mambo hayo kuwa njia ya kuepuka mahangaiko ya akili ya kila siku, hata kama nilijua kwamba kukamatwa na polisi kungeharibisha masomo yangu ya sheria.

Mimi na marafiki wangu tulikuwa tunapenda kutembelea mahali pa kuchezea muziki na kunywa pombe usiku. Wakati tulikuwa huko, mara nyingi tulipigana kwenye barabara. Mara nyingi nilikamatwa na polisi, lakini nilifanya juu chini ili nisipate shida nyingi na sheria, wakati fulani nilipana rushwa (hongo ao kata-midomo). Kwa kweli, niliwaza nilikuwa ninafurahia maisha yangu kabisa. Lakini, katika moyo wangu, nilijua kama mambo nilikuwa ninafanya yalikuwa mabaya. Nilikuwa ninaenda kwenye kanisa kila Siku ya Yenga ili kutuliza zamiri yangu.

BIBLIA ILIBADILISHA MAISHA YANGU:

Katika mwaka wa 2004, Mashahidi wawili wa Yehova walipiga hodi kwenye mulango wangu, na nilikubali kuzungumuza nao juu ya Biblia. Wakati nilijifunza mengi juu ya maana ya kuwa Mukristo wa kweli, zamiri yangu ilianza kunisumbua sana. Nilijua kama nilipaswa kuacha kunywa pombe sana, kutumia dawa za kulewesha, na kuacha kufanya urafiki na watu wenye hawakuishi kulingana na kanuni za Biblia. Tena, nilijua kama nilipaswa kubadilisha hali yangu ya kuwa mukali na mwenye jeuri. Hata kama nilitambua kuwa nilipaswa kufanya mabadiliko, niliendelea tu na tabia zangu mbaya.

Maisha yangu yalibadilika siku moja usiku wakati nilianza kupigana na wanaume munane. Ninakumbuka wakati nilikuwa mwenye kulala kwenye barabara nikiwa mwenye kupigwa sana kwenye kichwa. Nilijisikia kuwa karibu kufa, nilisali hivi: “Yehova unisamehe, kwa sababu sikuchukua kwa uzito Neno lako. Kama ninapona, ninakuahidi kama nitajifunza Biblia na Mashahidi na kubadilisha maisha yangu.” Jambo la kushangaza ni kwamba nilipona. Nilitimiza ahadi yangu ya kujifunza Biblia.

Katika mwaka wa 2006, nilihamia katika inchi ya Uingereza. Kusudi langu lilikuwa kupata feza nyingi za kunisaidia kurudia Polandi na kupata diploma ya juu katika masomo ya sheria. Wakati niliendelea kujifunza Biblia, andiko moja liligusa moyo wangu sana. Mutume Paulo aliandika hivi: ‘Kwa kweli naviona vitu vyote kuwa hasara [upotevu] kwa sababu ya samani bora zaidi ya kumujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa sababu yake nimekubali hasara ya vitu vyote nami naviona kuwa takataka nyingi, ili niweze kumupata Kristo.’ (Wafilipi 3:8) Kama mimi, mutume Paulo alikuwa amejifunza sheria na alikuwa pia mutu mwenye jeuri sana. (Matendo 8:3) Hata hivyo, alielewa kwamba kulikuwa njia ya muzuri ya maisha, ni kusema, kutumikia Mungu na kujikaza sana ili kuiga Yesu. Wakati nilifikiri sana juu ya mufano wa Paulo, niliona kama kazi yenye kuleta feza nyingi na mwenendo wa jeuri haikukuwa siri ya kupata furaha. Nilisadiki kama ningeweza pia kubadilika kwa sababu mutume Paulo alibadilika. Kwa hiyo, niliamua kubakia katika inchi ya Uingereza na kuacha kufuatia diploma ya juu katika masomo ya sheria.

Kuendelea kujifunza juu ya Yehova kulinisaidia niendelee kumukaribia. Niliguswa moyo na ahadi ya Mungu ya kusamehe watu wenye kupenda kabisa kubadilisha maisha yao. (Matendo 2:38) Na wakati nilifikiri sana juu ya andiko la 1 Yohana 4:16, lenye kusema kama “Mungu ni upendo,” nilianza kuelewa sababu gani anachukia jeuri.

Nilipenda kuwa kati ya familia ya Mashahidi wa Yehova ya ndugu na dada wenye furaha

Tena, mwenendo wa Mashahidi ulinivutia sana. Niliona waziwazi kama wanajikaza kushika kanuni za Biblia za juu za mwenendo. Nilipenda kuwa kati ya familia hiyo ya ndugu na dada yenye furaha. Kisha kujikaza sana ili kufanya mabadiliko katika maisha yangu, nilibatizwa na kuwa Shahidi wa Yehova katika mwaka wa 2008.

Mimi na Esther tunapata furaha ya kweli katika kufundisha Biblia watu wenye kusema luga ya Kipolandi

FAIDA YENYE NIMEPATA:

Biblia imenibadilisha: nilikuwa mutu mwenye kupenda mambo makubwa, mwenye jeuri, mwenye kutumia dawa za kulewesha, mwenye kunywa pombe sana na mwenye kupenda sana muchezo wa kabumbu. Sasa nimekuwa mutumishi wa Mungu mwenye kufurahia kufundisha wengine Biblia. Ningali ninafurahia kuangalia muchezo wa kabumbu, lakini sasa ninajikaza kuuweka pa nafasi yake.

Niko mwenye furaha katika ndoa yangu na Esther, mwanamuke mwenye sura ya muzuri anayemuabudu pia Yehova. Tunapata furaha ya kweli katika kufundisha Biblia watu wenye kusema luga ya Kipolandi katika eneo la kaskazini-mangaribi mwa Uingereza. Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, ninajisikia kuwa mwenye furaha ya kweli. Niko na zamiri safi na maisha yenye maana na yenye furaha.