Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

UIGE IMANI YAO | DEBORA

‘Nilisimama Kama Mama Katika Israeli’

‘Nilisimama Kama Mama Katika Israeli’

DEBORA aliangalia maaskari wenye walikuwa wamekusanyika juu ya Mulima Tabori. Aliguswa moyo kuwaona kwenye mulima huo. Wakati wa asubuhi, alitambua uhodari wao na imani ya Baraka, kiongozi wao. Hata kama walikuwa maaskari 10000 wenye nguvu, imani yao na uhodari wao vingejaribiwa sana siku hiyo. Wangepigana na adui asiye na huruma, walikuwa kidogo na hawakukuwa na silaha za muzuri. Lakini walikuja tu kupigana, zaidi sana kwa sababu mwanamuke huyo aliwatia moyo.

Umuone Debora katika akili yako, wakati nguo zake zinapeperushwa na upepo; yeye na Baraka wanaangalia eneo kubwa lenye kupendeza. Mulima Tabori ulikuwa wenye kupanuka chini na wenye kugonda juu, lakini sehemu yake ya juu haikukuwa na chongo. Mutu aliyekuwa juu ya mulima huo angeweza kuona Bonde la Esdraeloni kwenye meta 400 hivi chini; bonde hilo lilikuwa linafika sehemu ya kusini-mangaribi. Muto Kishoni ulijikunja-kunja katika eneo kubwa la bonde lenye majani ambalo liliongoza kwenye Bahari Kubwa kupitia Mulima Karmeli. Pengine muto ulikuwa unakauka asubuhi hiyo, lakini kuko jambo lingine lenye lilikuwa linaangara kwenye bonde hilo kubwa. Jeshi la Sisera lilikuwa linakaribia sana, na vyombo vyao vya chuma vilikuwa vinaangara sana. Sisera alichagua vyombo vya muzuri sana katika jeshi lake, ni kusema, magari 900 ya vita yenye labda yalikuwa na panga za chuma kwenye magurudumu (pneus). Alikuwa na kusudi la kufagia kabisa jeshi la Israeli lenye halikukuwa na silaha za muzuri kama zake!

Debora alijua kuwa Baraka na jeshi lake walikuwa wanangojea neno fulani ao alama fulani, kutoka kwake. Yeye tu ndiye alikuwa mwanamuke hapo? Kuwa na madaraka mengi katika hali kama hiyo kulifanya Debora ajisikie namna gani? Alijiuliza ikiwa alikuwa anafanya nini hapo? Kwa kweli, hapana! Yehova, Mungu wake, alikuwa amemuambia aanzishe vita hiyo; tena alikuwa amemuambia kuwa atatumia mwanamuke ili kuimaliza. (Waamuzi 4:9) Debora na wapiganaji hao wenye uhodari wanaweza kutufundisha nini juu ya imani?

‘NENDA, USAMBAE KATIKA MULIMA TABORI’

Wakati Biblia inataja Debora kwa mara ya kwanza, inamuita “nabii.” Jina hilo linaonyesha kuwa Debora hakukuwa mwanamuke wa kawaida, lakini, katika Biblia haiko yeye tu ndiye anaitwa hivyo. * Debora alikuwa na daraka lingine. Ni wazi kuwa alikuwa anahukumu watu kwa kutoa jibu la Yehova juu ya magumu yenye yalikuwa yanatokea.—Waamuzi 4:4, 5.

Debora alikuwa anaishi katika eneo lenye milima la Efraimu, kati ya muji wa Betheli na wa Rama. Hapo alikuwa anakaa chini ya muti wa ngazi ili kuhukumu watu kama vile Yehova alimuomba. Kwa kweli, kazi ya Debora ilikuwa ngumu, lakini hakuruhusu imuogopeshe. Kazi yake ilikuwa ya lazima sana. Baadaye alifikia kutunga wimbo wenye uliongozwa na roho ya Mungu. Katika wimbo huo, kulikuwa na maneno haya juu ya watu wa taifa lake wasio waaminifu: “Wakaanza kuchagua miungu mipya. Ndipo kukawa na vita malangoni.” (Waamuzi 5:8) Kwa sababu Waisraeli walimuacha Yehova ili kutumikia miungu mingine, Yehova aliacha maadui wao wawatawale. Mufalme Mukanaani Yabini, aliwatawala kwa kutumia jenerali mwenye nguvu aliyeitwa Sisera.

Jina Sisera liliwaogopesha na kuwatetemesha sana Waisraeli. Dini ya Wakanaani na desturi yao havikukuwa na huruma, vilikuwa na mambo kama vile ukahaba kwenye hekalu na kuunguza watoto ili kuwatoa kwa miungu yao. Hali ilikuwa namna gani kwa sababu ya kutawaliwa na jenerali Mukanaani na jeshi lake? Wimbo wa Debora unaonyesha kama ilikuwa vigumu kusafiri katika inchi na hakuna mutu aliishi tena katika vijiji. (Waamuzi 5:6, 7) Wazia namna watu walikuwa wanatetemeka katika mapori na vilima, waliogopa kulima ao kuishi katika vijiji vyenye havina ukuta, na kusafiri katika barabara ili wasishambuliwe, watoto wao wasikamatwe, na bibi zao wasilalwe kinguvu. *

Watu waliishi katika woga kwa miaka 20, mupaka wakati Yehova aliona kuwa watu wake wenye vichwa vigumu walikuwa tayari kubadilika. Ao kama vile maneno yaliyoongozwa na roho ya Mungu katika wimbo wa Debora na Baraka yanasema, ‘Mupaka mimi, Debora, niliposimama, mupaka niliposimama kama mama katika Israeli.’ Hatujue ikiwa Debora, bibi ya mwanaume mwenye kuitwa Lapidothi, alikuwa na watoto, lakini neno mama lilitumiwa kwa njia ya mufano. Kwa kweli, Yehova alimupatia Debora kazi ya kulinda watu wake kama mama. Yehova alimuambia Debora aite muamuzi Baraka, mwanaume mwenye nguvu na mwenye imani, ili apigane vita na Sisera.—Waamuzi 4:3, 6, 7; 5:7.

Debora alimutia Baraka moyo apigane ili kuokoa watu wa Mungu

Kupitia Debora, Yehova alimuamuru Baraka hivi: ‘Nenda, usambae katika Mulima Tabori.’ Baraka alipaswa kukusanya wanaume 10000 katika makabila mawili ya Israeli. Debora alimujulisha ahadi ya Mungu kwamba watapata ushindi juu ya Sisera, mwanaume mwenye nguvu, na magari yake 900 ya vita! Kwa kweli, ahadi hiyo ilimushangaza Baraka. Taifa la Israeli halikukuwa na jeshi na silaha nyingi. Hata hivyo, Baraka aliitika kwenda kwenye vita, ikiwa tu Debora angeenda pamoja nao kwenye Mulima Tabori.—Waamuzi 4:6-8; 5:6-8.

Watu fulani wamesema kama Baraka alikosa imani kwa kumuomba Debora aende naye katika vita, lakini huo ni uwongo. Baraka hakuomba Mungu amupatie silaha zingine. Lakini, kwa sababu alikuwa mutu wa imani, aliona kuwa lilikuwa jambo la maana kwenda pamoja na mujumbe wa Yehova ili awatie nguvu, yeye na watu wake. (Waebrania 11:32, 33) Yehova aliitika ombi la Baraka. Alimuruhusu Debora aende. Lakini, Yehova alimuongoza tena Debora atabiri kama utukufu juu ya ushindi wa mwisho wa vita hautapewa mwanaume. (Waamuzi 4:9) Mungu alikuwa ameamua kuwa mwanamuke ndiye angemuua mutu huyo mubaya, Sisera!

Katika dunia leo, wanawake wanatendewa mubaya, bila haki, na kwa jeuri. Mara nyingi, hawapewe heshima yenye Mungu anapenda wapate. Lakini, Mungu anaona wanaume na wanawake kuwa sawa, na wote anawakubali. (Waroma 2:11; Wagalatia 3:28) Mufano wa Debora unatukumbusha kama anabariki pia wanawake kwa kuwapatia mapendeleo na alama zenye kuonyesha kuwa anawatumainia na kuwakubali. Ni jambo la maana tuepuke kabisa kuwa na ubaguzi kama watu wengi katika dunia leo.

“DUNIA ILITIKISIKA, MBINGU PIA ZIKATIRIRIKA MAJI”

Baraka alienda kukusanya jeshi lake. Alikusanya wanaume 10000 wenye walikuwa hodari zaidi ili waende kupigana na jeshi la Sisera lenye kuogopesha. Wakati Baraka alikuwa anaongoza jeshi lake kwenye Mulima Tabori, alifurahi kwa sababu kulikuwa jambo lenye liliwafanya wakuwe hodari zaidi. Biblia inasema hivi: “Na Debora akapanda pamoja naye.” (Waamuzi 4:10) Wazia namna maaskari hao walitiwa moyo kuona kuwa mwanamuke huyo hodari alijiunga nao kwenda kwenye Mulima Tabori; alikuwa tayari kuhatarisha uzima wake kwa sababu alikuwa na imani kwa Yehova!

Wakati Sisera alijua kama Waisraeli walikusanya jeshi ili kumupiganisha, alitenda haraka. Wafalme wengi wa Kanaani walijiunga na Mufalme Yabini, ambaye pengine ndiye alikuwa mwenye nguvu zaidi kati yao. Magari mengi ya vita ya majeshi ya Sisera yalifanya udongo utikisike wakati yalitembea pamoja na kujaza bonde. Wakanaani walikuwa hakika kuwa watafagia haraka jeshi la Israeli lenye waliona kuwa bure.—Waamuzi 4:12, 13; 5:19.

Baraka na Debora wangefanya nini wakati maadui walikaribia? Wangebakia kwenye Mulima Tabori, labda hilo lingewaletea faida ya kupata ushindi juu ya maadui wao waliokuwa wanakaribia, kwa sababu magari yao ya vita yalipaswa kupigana muzuri katika eneo la bonde. Lakini Baraka angepigana kufuatana na maagizo ya Yehova, kwa hiyo alingojea neno kutoka kwa Debora. Mwishowe, wakati ulifika. Debora alimuambia hivi: ‘Simama, kwa maana hii ndiyo siku ambayo Yehova hakika atamutia Sisera mukononi mwako. Je, Yehova siye ambaye ameenda mbele yako?’ Tena Biblia inasema: ‘Baraka akashuka kutoka Mulima Tabori akiwa na wanaume elfu kumi nyuma yake.’—Waamuzi 4:14. *

Jeshi la Israeli lilishuka kutoka kwenye mulima na kwenda katika eneo la bonde lenye kuwa wazi. Wakajielekeza mahali kulikuwa magari hayo ya vita yenye kuogopesha. Yehova alienda mbele yao, kama vile Debora alikuwa ameahidi? Jibu lilipatikana bila kukawia. Biblia inasema hivi: “Dunia ilitikisika, mbingu pia zikatiririka maji.” Yehova alivuruga majeshi ya Sisera yenye kiburi. Na mvua ikanyesha! Ilikuwa mvua kubwa sana, inaonekana kuwa udongo ulijaa maji haraka. Bila kukawia, magari hayo mazito ya chuma hayakuwa tena na faida yoyote. Yalizama katika matope, na hayakuweza tena kuendelea.—Waamuzi 4:14, 15; 5:4.

Baraka na watu wake hawakuvurugika kwa sababu ya mvua hiyo kubwa. Walijua kwenye ilitoka. Walienda haraka mupaka kwenye majeshi ya Wakanaani yalikuwa. Waisraeli walitenda ili kutimiza hukumu ya Mungu, waliua maaskari wote wa Sisera. Muto Kishoni ulijaa maji na ukashusha maiti ya wanajeshi hao katika Bahari Kubwa.—Waamuzi 4:16; 5:21.

Kama vile Debora alitabiri, Yehova alipigania watu wake, kwa kuwapatia ushindi juu ya majeshi ya Sisera

Leo, Yehova hatume tena watumishi wake wapigane vita ya kimwili. Lakini, anawaomba wapigane vita ya kiroho. (Mathayo 26:52; 2 Wakorintho 10:4) Ikiwa tunajikaza kumutii Mungu katika dunia ya leo, tunashiriki katika vita hiyo. Tuko na lazima ya uhodari, kwa sababu watu wenye kujitia upande wa Mungu leo wanaweza kupata upinzani mukali. Lakini Yehova hajabadilika. Anaendelea kusaidia watu wenye kumuamini na kumutumainia kama Debora, Baraka, na maaskari wa Israeli ya zamani waliokuwa hodari.

‘ALIBARIKIWA ZAIDI KATI YA WANAWAKE’

Adui mumoja Mukanaani aliponyoka, huyo ndiye alikuwa adui mubaya sana! Sisera, mutesaji mukubwa wa watu wa Mungu alikimbia kwa muguu kutoka kwenye uwanja wa vita. Sisera aliacha watu wake wakufe katika matope. Aliponyoka maaskari Waisraeli na kukimbilia kwenye udongo wenye kukauka ili kwenda kujificha kwa watu wa karibu wenye walikuwa wamefanya mapatano nao. Kwa sababu aliogopa sana kwamba maaskari Waisraeli wanaweza tena kumuona, alikimbia haraka kilometa nyingi katika bonde na kujielekeza kwenye hema za Heberi. Heberi alikuwa mutu wa kabila la Wakeni mwenye alikuwa amejitenga na watu wake wenye kuhama-hama ambao waliishi upande wa kusini, na kisha akakuja kufanya agano na Mufalme Yabini.—Waamuzi 4:11, 17.

Sisera akiwa mwenye kuchoka sana, akafika kwenye kambi ya Heberi. Hakumukuta Heberi nyumbani kwake. Lakini alikuta Yaeli, bibi ya Heberi. Pengine Sisera aliwaza kama Yaeli angeheshimia mapatano ya bwana yake pamoja na Mufalme Yabini. Labda aliona kuwa haiwezekane mwanamuke atende ao kuwaza tofauti na bwana yake. Ni wazi kwamba Sisera hakukuwa anamujua Yaeli! Kwa kweli, Yaeli alikuwa anaona ubaya wa Wakaanani waliotesa watu katika inchi; na pengine aliona kuwa alikuwa na uamuzi wa kufanya: angeamua kumusaidia mwanaume huyo mubaya ao kuunga Yehova mukono kwa kumushambulia adui huyo wa watu wa Yehova. Lakini angefanya nini? Namna gani mwanamuke angepata ushindi juu ya mupiganaji huyo mwenye nguvu na mwenye kuzoea vita?

Yaeli alipaswa kufikiri haraka. Alimupatia Sisera nafasi ya kupumzikia. Sisera alimuambia Yaeli asiambie mutu yeyote mwenye anakuja kumutafuta kama alikuwa pale. Wakati Sisera alilala, Yaeli alimufunika, na wakati alimuomba maji, alimupatia maziwa mazito. Mara moja, Sisera akalala usingizi muzito. Kisha Yaeli akakamata vyombo viwili vya nyumbani vyenye wanawake wenye kukaa katika mahema walikuwa wanatumia mara nyingi na kwa ufundi. Alitumia nyundo (marteau) na chombo fulani chenye kuwa kama musumari. Yaeli aliinama karibu na kichwa cha Sisera, sasa alikuwa mbele ya jambo ngumu zaidi lenye alipaswa kufanya ili kutimiza hukumu ya Mungu. Kuwa na mashaka ao kusita kidogo kungemuletea hatari. Yaeli aliwaza juu ya watu wa Mungu na namna mutu huyo alikuwa amewatesa kwa miaka mingi? Ao alifikiria pendeleo la kujiunga upande wa Yehova? Habari hiyo haiseme kitu juu ya mambo hayo. Tunajua tu kama alitenda bila kukawia. Aliua Sisera!—Waamuzi 4:18-21; 5:24-27.

Kisha Baraka alikuja kumutafuta Sisera. Wakati Yaeli alimuonyesha maiti ya Sisera iliyotobolewa kwenye sura na chombo fulani chenye kuwa kama musumari, alijua kuwa unabii wa Debora ulikuwa umetimia. Mwanamuke huyo alimuua Sisera, mwanajeshi mwenye nguvu! Leo, watu wenye kuchambua na wenye mashaka wameita Yaeli majina mengi mabaya, lakini Baraka na Debora hawangeitika mawazo hayo. Katika wimbo wao, waliongozwa na roho ya Mungu kumusifu Yaeli kuwa ‘alibarikiwa zaidi kati ya wanawake’ kwa sababu ya tendo lake la uhodari. (Waamuzi 4:22; 5:24) Debora hakutafuta sifa yake mwenyewe. Hakumusikilia Yaeli wivu kwa sababu alisifiwa hivyo; lakini alifurahi kuona kuwa neno la Yehova lilikuwa limetimia

Kwa kuwa Sisera alikuwa amekufa, Mufalme Yabini hakuogopesha tena Waisraeli. Mwishowe, Wakanaani hawakuwatesa tena. Waisraeli wakaishi kwa amani miaka 40. (Waamuzi 4:24; 5:31) Debora, Baraka, na Yaeli walibarikiwa sana kwa sababu waliweka imani yao katika Yehova Mungu! Ikiwa tunaiga imani ya Debora, tunajitia upande wa Yehova kwa uhodari na kuwatia moyo wengine wafanye hivyo, Yehova atatubariki kwa kutupatia ushindi na amani yenye kuendelea.

^ fu. 7 Kulikuwa manabii wengine wanawake, kama vile, Miriamu, Hulda, na bibi ya Isaya.—Kutoka 15:20; 2 Wafalme 22:14; Isaya 8:3.

^ fu. 9 Wimbo wa Debora unaonyesha kuwa, mara nyingi wakati Sisera alikuwa anarudi kutoka kwenye vita, alikuwa analeta vitu vingi na hata vijana wanawake. Wakati fulani, kila askari alikuwa anarudia na mwanamuke zaidi ya mumoja. (Waamuzi 5:30) Maneno “tumbo la uzazi” yenye kutumiwa katika andiko hilo, yanamaanisha “kijana mwanamuke.” Maneno hayo yanatukumbusha kuwa wanawake hao walionwa kuwa wa maana zaidi sana kwa sababu ya viungo vyao vya uzazi. Ilikuwa kawaida kulala wanawake kinguvu.

^ fu. 17 Pigano lenye lilitokea linazungumuziwa mara mbili katika Biblia; linaelezwa katika Waamuzi sura ya 4 na katika wimbo wa Debora na Baraka wenye kuwa katika sura ya 5. Sura hizo mbili zinazungumuzia habari moja, lakini kila sura inatoa maelezo fulani yenye haikutajwa katika sura ingine.