Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MASIMULIZI KUHUSU MAISHA YA WATU

Yehova Amenipatia Mambo Mengi Kuliko Yenye Ninastahili

Yehova Amenipatia Mambo Mengi Kuliko Yenye Ninastahili

Wakati nilikuwa na miaka 17 tu, nilikuwa na tamaa na mahangaiko kama ya vijana wengi. Nilipenda kuwa pamoja na marafiki wangu, kuogelea (nager), na kucheza kabumbu. Lakini siku moja mangaribi, maisha yangu yalibadilika kabisa. Nilifanya aksidenti ya mubaya sana ya pikipiki (moto) na ikafanya nipooze kuanzia kwenye shingo mupaka kwenye miguu. Aksidenti hiyo ilinifikia kumepita miaka 30 hivi, na sasa nimekuwa kwenye kitanda kwa muda murefu.

Nilikomalia katika muji wa Alicante, katika sehemu ya mashariki ya Hispania (Espagne) yenye kuwa pembeni ya bahari. Familia yetu ilikuwa na magumu mengi, kwa hiyo, wakati nilikuwa kijana nilipitisha wakati mwingi kuzunguka-zunguka kwenye barabara. Nyumba yetu ilikuwa karibu na duka la kutengeneza magurudumu (pneus) zenye kuharibika. Nilifanya urafiki na José María mwenye alikuwa anatumika katika duka hilo. Alikuwa mutu muchangamufu mwenye alinionyesha upendo; nilikosa jambo hilo katika familia yetu. Wakati nilikuwa na magumu, José alikuwa kama ndugu na rafiki wa kweli, hata kama alinipita miaka 20.

José María alikuwa ameanza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova. Niliona kama alipenda Maandiko, na mara nyingi alikuwa ananiambia mambo alikuwa anajifunza. Nilikuwa ninamusikiliza kwa heshima, lakini sikupendezwa kabisa na mambo alikuwa anasema. Kwa sababu nilikuwa kijana, nilihangaikia mambo mengine. Lakini, hilo lilikuwa karibu kubadilika.

AKSIDENTI YENYE ILIBADILISHA MAISHA YANGU

Sipendake kuzungumuza sana juu ya aksidenti hiyo ya barabarani. Jambo ninaweza kusema ni hili: nilikuwa mupumbavu na sikuhangaika juu ya kitu chochote. Katika siku moja tu, maisha yangu yote yalibadilika kabisa. Nilikuwa kijana mwenye nguvu, lakini mara moja nilijikuta katika hospitali nikiwa mwenye kupooza. Ilikuwa vigumu kabisa kukubali hali yangu. Niliendelea kujiuliza, ‘Maisha iko na maana?’

José María alikuja kuniangalia, na bila kukawia akafanya mipango ili Mashahidi wa Yehova wa kutaniko lao wakuje kunitembelea kwenye hospitali. Kutembelewa na Mashahidi hao kwa ukawaida kulinigusa moyo. Wakati nilitoka katika chumba cha wagonjwa wenye kuwa katika hali mbaya sana, nilianza mara moja kujifunza Biblia. Nilijua kweli juu ya sababu yenye inafanya watu wateseke na kufa, na sababu gani Mungu anaacha mambo mabaya yafanyike. Tena, nilijua ahadi za Mungu juu ya wakati unaokuja, wakati dunia itajaa watu wakamilifu na hakuna mutu atasema: ‘Mimi ni mugonjwa.’ (Isaya 33:24) Kwa mara ya kwanza katika maisha yangu, nilipata tumaini la muzuri juu ya maisha.

Wakati nilitoka katika hospitali, nilifanya maendeleo haraka katika funzo langu la Biblia. Kwa kutumia kinga ya vilema, nilienda hata kwenye mikutano fulani ya Mashahidi wa Yehova na katika kazi yao ya kuhubiri. Tarehe 5 Mwezi 11, 1988, nilibatizwa kwa kuingizwa ndani ya maji katika beseni kubwa ya kunawia mwili wote; nilikuwa na miaka 20. Yehova Mungu amenisaidia kuwa na mawazo ya muzuri juu ya maisha. Lakini ningefanya nini ili kumuonyesha shukrani yangu?

NINAENDELEA MBELE HATA KAMA NIKO KILEMA

Nilikusudia kutoacha hali yangu inizuie kufanya yote ningeweza kutimiza katika utumishi wa Yehova. Nilipenda kufanya maendeleo. (1 Timotheo 4:15) Mwanzoni, haikukuwa vyepesi kufanya hivyo, kwa sababu watu wa familia yangu walipinga imani yangu mupya. Lakini nilikuwa na waamini wenzangu, ndugu na dada Mashahidi wa Yehova. Walinisaidia kwenda kwenye mikutano yote ya kutaniko na kuhubiri kwa ukawaida.

Kadiri wakati uliendelea kupita, ilionekana kuwa nilipaswa kuhangaikiwa sana usiku na muchana. Kisha kutafuta kwa siku nyingi, nikapata nafasi ya muzuri ya kuwatunzia vilema katika muji wa Valencia, kwenye kilometa 160 kaskazini mwa Alicante. Nafasi hiyo ikakuwa nyumba yangu mupaka leo.

Hata kama siwezi kutoka kwenye kitanda, ninakusudia kuambia wengine mambo ninaamini

Hata kama siwezi kutoka kwenye kitanda, nilikusudia kuendelea mbele. Nilitumia feza zenye vilema wanalipwa na misaada mingine ili kuuza ordinatere na ikawekwa pembeni ya kitanda changu. Na nikauza telefone. Kila asubuhi, mutu fulani mwenye kutuchunga, ananifungulia ordinatere na telefone yangu. Ili kutumikisha ordinatere yangu, ninatumia chombo fulani chenye ninasogeza-sogeza na kidevu changu. Tena niko na muti fulani wa pekee wenye ninakamata na kinywa changu.

Ninatumia muti kuandika namba katika telefone yangu ili kuita mutu

Namna gani vyombo hivyo vinanisaidia? Kwanza kabisa, vinanisaidia kufungua adresi ya Internete jw.org na maktaba kwenye Internete (la BIBLIOTHÈQUE EN LIGNE Watchtower). Vyombo hivyo vimenisaidia kabisa! Mara nyingi, ninatumia saa nyingi kila siku ili kujifunza na kutafuta habari katika vichapo vyenye kutegemea Biblia ili niendelee kujifunza juu ya Mungu na juu ya sifa zake za muzuri sana. Na wakati ninajisikia kuwa peke yangu ao mwenye kuvunjika moyo, sikuzote ninapata habari ya kunitia moyo kwenye adresi yetu ya Internete.

Tena, ordinatere yangu inanisaidia kusikiliza na kushiriki katika mikutano ya kutaniko. Ninaweza kutoa maelezo, kusali, kutoa hotuba, na hata kusoma gazeti Munara wa Mulinzi wakati ninaombwa kufanya hivyo. Hata kama siwezi kufika kwenye mikutano hiyo, ninajisikia kabisa kuwa niko mumoja wa watu wa kutaniko letu.

Kuwa na telefone na ordinatere kunanisaidia pia kuhubiri kwa ukawaida. Siwezi kuhubiri nyumba kwa nyumba kama Mashahidi wengine wengi. Lakini jambo hilo halinizuie kuhubiri. Kwa kutumia vyombo hivyo, ninaweza kuambia watu wengine mambo ninaamini. Kwa kweli, ninafurahia sana kuhubiri kupitia telefone, ndiyo sababu wazee wa kutaniko letu wameniomba nisimamie kampanye za kuhubiri kupitia telefone. Kampanye hizo zimesaidia sana ndugu na dada wa kutaniko wenye hawana uwezo wa kutoka nyumbani.

Ninaongoza funzo la Biblia

Lakini siishi tu kwa sababu ya vyombo vya kiteknolojia. Kila siku, marafiki wapendwa wanakuja kuniangalia. Wanakuja na watu wa jamaa zao na watu wengine wenye wanajuana nao ambao wanapenda kujifunza Biblia. Mara nyingi, wananiomba hata niongoze mazungumuzo. Wakati mwengine, familia zinanitembelea ili nishiriki kwenye ibada yao ya familia ya mangaribi. Ninafurahi sana wakati watoto wadogo wanakaa karibu na kitanda changu na kuniambia sababu gani wanamupenda Yehova.

Ninafurahia ibada ya familia ya mangaribi pamoja na marafiki

Ninafurahia kupokea wageni wengi. Mara nyingi, chumba changu kinajaa marafiki wanaokuja kuniona kutoka karibu ao mbali. Na kama vile unaweza kuwazia, upendo huo unashangaza sana watu wenye kututunza. Kila siku, ninamushukuru Yehova kwa sababu amenisaidia kuwa katika familia hiyo ya muzuri ya ndugu na dada.

NINAENDELEA KUPIGANA VITA

Wakati mutu ananisalimia na kuniuliza habari yangu, ninasema tu, “Mimi huyu, ninaendelea kupigana vita!” Kwa kweli, ninajua kuwa siko mimi mwenyewe katika vita hiyo. Hata tuwe na hali gani ao magumu gani, Wakristo wote wanapigana vita, ni kusema, ‘pigano nzuri la imani.’ (1 Timotheo 6:12) Ni nini kimenisaidia kupigana vita kwa miaka mingi? Ninasali kila siku na ninamushukuru Yehova kwa sababu amefanya maisha yangu yakuwe na maana. Tena ninajikaza kuwa na mambo mengi ya kufanya katika kazi ya Mungu na ninaendelea kukazia macho ahadi ya wakati unaokuja.

José María

Mara nyingi ninawaza juu ya dunia mupya na namna nitajisikia wakati nitakimbia na kuruka tena. Wakati fulani, ninafanya muzaa na rafiki yangu mupendwa José María, mwenye iko na ugonjwa wa polio, juu ya muchezo wa kukimbia pamoja. Ninamuuliza, “Ni nani anaweza kutoka wa kwanza?” Ananijibu, “Kutoka wa kwanza haiko jambo la maana. Jambo la maana ni kuwa hapo, katika Paradiso, ili kukimbia.”

Haikukuwa vyepesi kukubali ulemavu wangu. Ninajua kuwa wakati nilikuwa kijana, nilitenda kama mutu mupumbavu, na hilo limeniletea matokeo mabaya sana. Hata hivyo, niko mwenye shukrani sana kuona kuwa Yehova hakuniacha. Amenipatia mambo mengi sana: familia kubwa ya ndugu na dada, nia ya kuishi, furaha ya kusaidia watu wengine, na tumaini la muzuri kwa ajili ya wakati unaokuja. Kama ninasema kwa kifupi namna ninajisikia, ninaweza kusema kama Yehova amenipatia mambo mengi kuliko yenye ninastahili.