Ona video zinazopatikana

TUIGE IMANI YAO | MIRIAMU

“Mumuimbie Yehova”!

“Mumuimbie Yehova”!

 Kijana mwanamuke alishajificha fasi yenye hawezi kuonekana, iko naangalia kwa uangalifu sana fasi fulani katikati ya matete. Maji ya Muto Nile iko nateremuka polepole, yeye iko tu pale, hatikisike. Wakati inaendelea kupita, mwili wake unapaswa kuwa unaanza kuluma lakini anaendelea kuchunga, na kuangalia katikati ya ile matete. Makelele ya vidudu yenye iko anasikia pembeni yake haifanye aache kuwa muangalifu. Fasi kwenye iko anaangalia kuko kitunga yenye kufichwa mu muto, na ndani ya ile kitunga muko mudogo yake. Wakati anafikiria vile mutoto wao iko yeye peke bila mutu wa kumusaidia, ile inamuhuzunisha sana. Lakini alijua kama wazazi wake walifanya muzuri kwa kumutia mu kitunga. Ile njo ilikuwa njia moya tu ya kuokoa uzima wake.

 Ule kijana mwanamuke anaonyesha uhodari wa nguvu, lakini alikuwa karibu kuonyesha uhodari wa nguvu tena sana. Hata kama angali na miaka kidogo, tayari alianza kukomalisha sifa moya ya muzuri sana, imani. Mambo yenye itatokea hivi karibuni itahakikisha ile jambo na ile imani itamusaidia mu njia ya ajabu mu maisha yake. Miaka mingi kisha pale, wakati alikuwa mwenye kuzeeka, imani yake ilimusaidia mu kipindi ya maana sana mu historia ya watu wa Mungu. Wakati ingine ileile imani, ilimusaidia pia wakati alifanya kosa nzito. Ule kijana mwanamuke alikuwa nani? Tunaweza kujifunza nini kupitia imani yake?

Miriamu Mutoto wa Utumwa

 Biblia haituambie waziwazi jina ya ule kijana ilikuwa nani, lakini tunamujua. Alikuwa Miriamu, mutoto wa kwanza wa Amramu na Yokebedi, Waebrania wenye walikuwa watumwa mu inchi ya Misri. (Hesabu 26:59) Mudogo yake mwenye alifichwaka mu kitunga alifikiaka kuitwa Musa. Miriamu alikuwaka pia na mudogo mwingine, jina yake Haruni, alikuwa na miaka tatu hivi ile wakati. Hatujue kabisa miaka yenye Miriamu alikuwaka nayo ile wakati, lakini inaonekana pengine alikuwa hayaeneza miaka kumi.

 Miriamu aliishi mu kipindi yenye watu wake walikuwa mu magumu ya nguvu sana. Wamisri waliona Waebrania kuwa hatari sana, njo maana waliwafanya kuwa watumwa na kuanza kuwatesa sana. Wakati watumwa Waebrania waliendelea kuongezeka, Wamisri waliogopa na walikamata mupango mukali tena zaidi. Farao aliamuru kama watoto wote wanaume wa Waebrania wanapaswa kuuawa wakati wanazaliwa. Bila shaka, Miriamu aliona imani yenye wanamuke wawili Waebrania wenye kuitwa Shifra na Pua walionyesha, wenye kazi yao ilikuwa kuzalisha. Wale wanamuke wawili walikatala kutii amri ya Farao.​—Kutoka 1:8-22.

 Miriamu aliona pia imani ya wazazi wake. Kisha kuzala mutoto wa tatu mwenye sura na umbo ya muzuri, Amramu na Yokebedi walimuficha kwa miezi tatu. Hawakuogopa agizo ya Mufalme Farao. Njo maana hawakuacha mutoto yao akufe. (Waebrania 11:23) Haikukuwa mwepesi kwao kuficha mutoto, lakini bila kukawia walilazimika kukamata uamuzi wa nguvu sana. Yokebedi alijua kama juu mutoto yake aendelee kuishi alipaswa kumuficha fasi fulani kwenye mutu fulani angeweza kumuona ili kumulinda na kumuhangaikia. Waza namna ule mama alipaswa kusali sana wakati alikuwa anatengeneza kitunga, na kukipakala kabulimbo na bereu juu maji isiingie ndani na kisha kutia mutoto yake mupendwa ndani ya ile kitunga na kumuacha mu Muto Nile! Bila shaka ni yeye njo alimuambiaka Miriamu abakie pale juu aone mambo yenye itatokea.​—Kutoka 2:1-4

Miriam Muokoaji

 Miriamu aliendelea kungojea. Kisha saa kidogo, akaona watu. Kikundi ya wanamuke wako natembea-tembea pembeni ya Muto Nile. Na hawakukuwa Wamisri wa hivi-hivi tu. Ilikuwa ni mutoto mwanamuke wa Farao pamoya na watumishi wake wanamuke, wenye walikuya kuoga ku Muto Nile. Pengine moyo wa Miriamu ulipiga-piga sana. Unawaza Miriamu angewazia hata kama binti ya Farao mwenyewe angevunja amri ya mufalme na kuchagula kumulinda mutoto Muebrania? Bila shaka mu ile saa Miriamu alisali sana.

 Kisha binti ya Farao akaona ile kitunga katikati ya matete. Akamutuma mutumishi wake mwanamuke amuletee ile kitunga. Habari inasema hivi juu ya binti ya Farao: “Wakati alifungua kile kitunga, akaona ule mutoto, na ule mutoto mwanaume alikuwa analia.” Mara moya akaelewa mambo yenye ilitokea: Mama fulani Muebrania alikuwa anajaribu kuokoa uzima wa mutoto wake. Lakini binti ya Farao akamusikilia huruma ule mutoto mwenye sura na umbo ya muzuri. (Kutoka 2:5, 6) Miriamu alikuwa anaangalia kwa uangalifu na kuona kama binti ya Farao alipenda kulinda mutoto. Miriamu akatambua kama ilikuwa sasa wakati wa kuonyesha imani yake kwa Yehova. Kwa uhodari wote, akamukaribia binti ya Farao na watumishi wake wanamuke.

 Hatujue ni mambo gani ingefikia mutoto wa mutumwa Muebrania mwenye angekuwa na uhodari wa kuzungumuza na mutu wa mu familia ya kifalme. Hata vile, Miriamu alienda na kumuuliza binti ya Farao hivi: “Je, niende kukuitia mwanamuke mwenye kunyonyesha kati ya Waebrania ili akunyonyeshee mutoto huyu?” Iliomba kuwa na akili sana juu ya kuuliza ulizo sawa ile. Binti ya Farao alijua kama hangeweza kunyonyesha ule mutoto. Pengine aliwaza kama ingekuwa muzuri zaidi ikiwa mama Muebrania njo angekuwa ananyonyesha ule mutoto; kisha binti ya Farao yeye mwenyewe angeweza kumupeleka ku nyumba na kumufanya kuwa mutoto wake na kumukomalisha na pia kumusomesha. Miriamu alipaswa kufurahi sana wakati binti ya Farao alimuambia hivi: “Uende!”​—Kutoka 2:7, 8.

Kwa uhodari Miriamu alihakikisha kama mudogo yake alikuwa salama

 Miriamu alirudia ku nyumba yao mbio kuona wazazi wake wenye walikuwa na wasiwasi. Wazia furaha yenye alikuwa nayo wakati alikuwa anamuambia mama yake ile habari. Bila shaka, Yokebedi alikuwa hakika kama ni Yehova njo alikuwa anaongoza mambo, kwa hiyo akaenda pamoya na Miriamu kwa binti ya Farao. Pengine Yokebedi alijikaza kufichika furaha yake wakati binti ya Farao alimuambia hivi: “Chukua mutoto huyu uninyonyeshee yeye, na mimi nitakulipa.”​—Kutoka 2:9.

 Ile siku, Miriamu alijifunza mambo mingi juu ya Mungu wake, Yehova. Alijifunza kama Yehova anahangaikiaka watu wake na kusikiliza sala zao. Alijifunza pia kama haiko tu wanaume ao watu wenye kukomala njo wanaweza kuonyesha imani na uhodari. Yehova anasikilizaka sala za watumishi wake wote waaminifu. (Zaburi 65:2) Leo pia, ikuwe tuko vijana ao watu wakubwa, wanaume ao wanamuke, siye wote tunapaswa kukumbuka ile jambo mu hii wakati ya nguvu.

Miriamu Dada Muvumilivu

 Yokebedi alinyonyesha na kuhangaikia ule mutoto. Wazia vile Miriamu alimupenda tena zaidi mudogo yake wa mwisho mwenye aliokoaka. Pengine alimusaidiaka ajue kusema na alifurahi wakati mudogo yake alitaja kwa mara ya kwanza jina ya Mungu wake, Yehova. Wakati mutoto alikomala, iliomba sasa kumupeleka kwa binti ya Farao. (Kutoka 2:10) Ile jambo ilipaswa kuhuzunisha familia yote. Miriamu alikuwa na hamu ya kuona namna mudogo yake, mwenye binti ya Farao alipatia jina Musa, angekuwa wakati angefikia kuwa mutu muzima. Je, ataendelea kumupenda Yehova wakati atakomalia mu nyumba ya kifalme ya Wamisri?

 Kisha wakati fulani, jibu ikakuwa wazi. Bila shaka Miriamu alipaswa kufurahi sana wakati alijua kama mudogo yake alichagula kumutumikia Mungu wake kuliko kufurahia faida zenye angepata mu nyumba ya kifalme ya Farao! Wakati Musa alikuwa na miaka 40, alipigania watu wake. Siku moya, aliua Mumisri moya juu alimutendea mubaya mutumwa fulani Muebrania. Lakini hakufanya vile mu njia ya muzuri na wakati ilikuwa haiyaenea juu ya kufanya vile. Sasa wakati aliona kama maisha yake ilikuwa mu hatari, alikimbia na kutoka mu inchi ya Misri.​—Kutoka 2:11-15; Matendo 7:23-29; Waebrania 11:24-26.

 Mu miaka makumi ine yenye ilifuata, pengine Miriamu hakupataka tena habari juu ya ndugu yake mudogo wakati alikimbilia mbali mu Midiani, kwenye alikuwa anachunga kondoo. (Kutoka 3:1; Matendo 7:29, 30) Wakati ilipita na Miriamu alizeeka, lakini aliendelea kuona mateso ya watu wake namna ilikuwa tu inaongezeka.

Nabii Miriamu

 Inawezekana Miriamu alikuwa na miaka 80 hivi wakati Musa alirudia, Mungu njo alimutumaka juu akomboe watu wake. Haruni alifikia kuwa musemaji wa Musa, na wote wawili waliendaka kwa Farao juu wamuombe aache watu wa Mungu waende. Bila shaka, Miriamu alifanyaka yake yote juu ya kusaidia na kutia moyo wadogo yake wakati Farao hakuwasikiliza, na wakati walirudia tena na tena kumuona Farao saa yenye Yehova alituma mapigo kumi juu ya Wamisri ili kuwaonya. Kupitia pigo ya mwisho Mungu aliua wazaliwa wote wa kwanza wa Misri, na ile njo ilifanya Waisraeli wote watoke mu Misri! Wazia namna Miriamu alisaidia sana watu wake wakati walitoka Misri chini ya uongozi wa Musa.​—Kutoka 4:14-16, 27-31; 7:1-12:51.

 Kisha, wakati Waisraeli walijikuta katikati ya Bahari Nyekundu na jeshi ya Wamisri, Miriamu aliona wakati ndugu yake Musa alisimama mbele ya Bahari Nyekundu na akainua fimbo yake. Bahari ikagawanyika! Kuona vile Musa aliongoza Waisraeli katikati ya bahari juu ya inchi kavu, bila shaka ile ilifanya imani ya Miriamu ikuwe nguvu zaidi kuliko zamani. Alijua kama Mungu wake iko tayari kufanya jambo yoyote, na kutimiza ahadi yoyote!​—Kutoka 14:1-31.

 Kisha, wakati aliona Waisraeli wanavuka kwa usalama na wakati bahari ilirudia vile ilikuwa na kufunika Farao na jeshi yake, ile jambo ilimusaidia Miriamu aelewe kama Yehova ni Mungu mwenye nguvu zaidi kuliko jeshi yoyote yenye nguvu sana hapa ku dunia. Ile ilifanya watu wamuimbie Yehova. Ili kuitikia wanaume, Miriamu aliongoza wanamuke juu wamuimbie Yehova hii maneno: “Mumuimbie Yehova, kwa maana ametukuzwa sana. Farasi na mupandaji wake, amewatupa katika bahari.”​—Kutoka 15:20, 21; Zaburi 136:15.

Miriamu aliongozwa na roho ya Mungu ili kuongoza wanamuke Waisraeli wamuimbie Yehova wimbo wa ushindi kwenye Bahari Nyekundu

 Ilikuwa wakati ya muzuri sana mu maisha ya Miriamu, hangeweza kuisahau hata siku moya. Ni kupitia hii habari njo Biblia inamuita Miriamu nabii. Yeye njo mwanamuke wa kwanza kuitwa vile. Miriamu iko kati ya hesabu kidogo ya wanamuke wenye walikuwa na pendeleo ya kumutumikia Yehova mu ile njia ya pekee.​—Waamuzi 4:4; 2 Wafalme 22:14; Isaya 8:3; Luka 2:36.

 Biblia inatukumbusha kama Yehova iko anatuangalia na kama iko tayari kutubariki juu ya bidii yetu, uvumilivu wetu, na tamaa yetu ya kumusifu. Njo maana ikuwe uko mutoto ao mukubwa, mwanaume au mwanamuke, na weye unaweza kuonyesha imani yako kwa Yehova. Imani ya vile inamufurahishaka; hawezi kuisahau hata siku moya, na juu ya ile iko tayari kukupatia zawabu. (Waebrania 6:10; 11:6) Hauone kama ile ni sababu ya muzuri ya kuiga imani ya Miriamu?

Miriamu Mwenye Kiburi

 Mapendeleo na kujulikana kunaletaka baraka lakini pia hatari. Wakati Waisraeli walitoka mu utumwa, inawezekana Miriamu njo alikuwa mwanamuke mwenye kujulikana sana mu taifa ya Israeli. Ile itafanya akuwe na kiburi ao na kimbelembele? (Mezali 16:18) Jambo ya kuhuzunisha ni kwamba, aliangukia mu ile mutego.

 Miezi kidogo kisha Waisraeli kutoka Misri, Musa alikaribishaka watu wenye kutoka mbali sana, ilikuwa Yetro baba-mukwe wake, na Sipora bibi ya Musa, pamoya na watoto wao wawili. Musa alimuoa Sipora wakati aliendaka kuishi kule Midiani kwa miaka 40. Pengine Sipora alirudiaka kule Midiani juu ya kutembelea watu wa familia yake, na sasa baba yake anamurudisha mu kambi ya Waisraeli. (Kutoka 18:1-5) Wazia furaha yenye Waisraeli walipaswa kuwa nayo wakati Sipora alirudia! Inawezekana, wengi walikuwa wanapenda kuona bibi ya mutu mwenye Mungu alichagulaka juu ya kuwatosha Misri.

 Miriamu naye alifurahi wakati Sipora alirudia? Pengine ku mwanzo alifurahi. Lakini inaonekana kama kisha wakati fulani Miriamu alifikia kuwa mutu mwenye kiburi. Pengine aliogopa kama Sipora njo atakuwa mwanamuke mwenye kujulikana sana kati ya Waisraeli kuliko yeye. Ikuwe aliogopa ao hapana, Miriamu na Haruni walianza kusema mambo fulani ya mubaya. Na mara mingi mazungumuzo ya vile inafikishaka ku ubaya sana. Kwanza walianza kumusema mubaya Sipora juu hakukuwa Muisraeli lakini alikuwa Mukushi. * Kisha walianza pia kumusema mubaya Musa. Miriamu na Haruni walikuwa wanasema hivi: “Je, Yehova amezungumuza kupitia Musa tu? Je, hajazungumuza kupitia sisi pia?”​—Hesabu 12:1, 2.

Miriamu Mwenye Ukoma

 Ile maneno, ilionyesha kama Miriamu na Haruni walianza kuwa na mawazo ya mubaya sana. Hawakufurahia kuona namna Yehova alikuwa anamutumikisha Musa. Walipenda kupata mamlaka zaidi na kujulikana tena zaidi. Je, walifanya vile juu Musa alikuwa na kiburi na alikuwa anatumikisha mamlaka yake mubaya? Ni kweli Musa naye alikuwa na makosa yake, lakini hakukuwa na kiburi ao kimbelembele. Maandiko yenye iliongozwa na roho ya Mungu inasema hivi: “Sasa mwanaume huyu Musa alikuwa mupole sana kuliko watu wote juu ya uso wa dunia.” Kusema kweli, Miriamu na Haruni walikuwa walishavuka mipaka yao, na walikuwa mu hatari. Kama vile andiko inasema, “Yehova alikuwa anasikiliza.”​—Hesabu 12:2, 3.

 Mara moya Yehova akawaita ndugu hao watatu kwenye hema ya mukutano. Pale nguzo kubwa ya wingu ikashuka na kusimama kwenye muingilio wa hema ya mukutano; ile ni alama ya kuonyesha kama Yehova iko pale. Kisha Yehova akaanza kusema. Akamukemea Miriamu na Haruni, na kuwakumbusha kama iko na urafiki wa pekee sana pamoya na Musa na kama anamutumainiaka sana. Kisha Yehova akawauliza hivi: “Sababu gani, basi, hamukuogopa kusema mubaya juu ya mutumishi wangu, juu ya Musa?” Bila shaka Miriamu na Haruni walitetemeka sana. Yehova aliona kama kumukosea Musa heshima ilikuwa kumukosea Yeye heshima.​—Hesabu 12:4-8.

 Inaonekana kama Miriamu njo alianzisha ile mazungumuzo, na akamuchochea mudogo yake Haruni ili waseme mubaya juu ya Sipora bibi ya mudogo wao Musa. Ile inatusaidia kuelewa juu ya nini Miriamu tu njo mwenye alipata malipizi. Yehova alimupiga ukoma. Ule ugonjwa wenye kuogopesha ulifanya ngozi yake ikuwe “mweupe kama teluji.” Mara moya Haruni akajinyenyekeza mbele ya Musa, na kumuomba amuambie Yehova amusamehe Miriamu. Alisema hivi: “Tumetenda kwa upumbavu katika jambo lenye tumefanya.” Juu Musa alikuwa mutu mupole, alianza kumulilia Yehova na kusema: “Ee Mungu, tafazali umuponyeshe! Tafazali!” (Hesabu 12:9-13) Musa na Haruni walihuzunika sana kuhusu ukoma wa Miriamu na walipenda apone. Ile ilionyesha kama wote wawili walimupenda sana dada yao hata kama alifanya makosa.

Miriamu Anaponyeshwa

 Yehova alimutendea kwa rehema. Juu Miriamu alitubu, Yehova alimuponyesha. Hata vile, aliamuru atengwe na wengine kwa muda wa siku saba, inje ya kambi ya Israeli. Miriamu alipaswa kusikia haya sana, juu watu wangeona kama alipata malipizi. Lakini imani yake ilimuokoa. Alijua kama Baba yake, Yehova, alitenda kwa haki na kama alimupatia malipizi juu alimupenda. Njo maana alifanya sawa vile Yehova alisema. Kambi ya Waisraeli ilikuwa inaongojea ile siku saba yote yenye Miriamu alikuwa peke yake. Kisha Miriamu alionyesha tena imani, mu hii wakati alikubali kwa unyenyekevu “kurudishwa ndani.”​—Hesabu 12:14, 15.

 Yehova anapatiaka nizamu wale wenye anapenda. (Waebrania 12:5, 6) Juu alimupenda sana Miriamu, alimurekebisha. Kusema kweli, ile nizamu ilimuumiza, lakini ilimuokoa pia Miriamu. Juu alijinyenyekeza na kukubali nizamu, Yehova alimukubali tena. Aliendelea kuishi mupaka karibu na mwisho wa safari ya Waisraeli mu jangwa. Alikuwa karibu kueneza miaka 130 wakati alikufa mu jangwa la Zini kule Kadeshi. * (Hesabu 20:1) Mamia ya miaka kisha pale, kwa upendo Yehova alimusifu Miriamu juu alimutumikia kwa uaminifu. Kupitia nabii Mika, Yehova alikumbusha watu wake hivi: “Niliwakomboa kutoka katika nyumba ya utumwa; nilituma Musa, Haruni na Miriamu mbele yenu.”​—Mika 6:4.

Imani ya Miriamu ilimusaidia aendelee kuwa munyenyekevu wakati Yehova alimupatia nizamu

 Tunaweza kujifunza mambo mingi sana kupitia maisha ya Miriamu. Na siye, tunapaswa kulinda wale wenye hawana uwezo wa kujilinda na kutetea mambo ya muzuri kwa uhodari, sawa vile Miriamu alifanyaka wakati alikuwa mutoto. (Yakobo 1:27) Sawa yeye, tunapaswa kutangazia wengine ujumbe wa Mungu kwa furaha. (Waroma 10:15) Pia, tunapaswa kujifunza kuepuka wivu na sifa zingine za mubaya. (Mezali 14:30) Na tena, tunapaswa kuwa tayari kukubali kwa unyenyekevu nizamu kutoka kwa Yehova. (Waebrania 12:5) Kusema kweli, kama tunafanya ile mambo yote, tutakuwa tumeiga kabisa imani ya Miriamu.

^ Kuhusu Sipora, inaonekana kama neno “Mukushi” ilionyesha kama alikuwa Muarabu, sawa Wamidiani wengine, na hapana Muetiopia.

^ Wale watoto wa Yokebedi na Amramu walikufa kufuatana na vile walizaliwa, Miriamu alikufa wa kwanza, kisha Haruni, na Musa alikufa wa mwisho. Na inaonekana kulikuwa napita mwaka moya kati ya kifo ya wote watatu.