Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Namna ya Kuzuia Hasira Yako

Namna ya Kuzuia Hasira Yako

TATIZO

“Nilimufokea dada yangu na kugonga mulango kwa nguvu hivi kwamba chuma kilichokuwa nyuma ya mulango huo kikaingia ndani ya ukuta. Tundu lenye chuma hicho kilifanya ndani ya ukuta liliendelea kunikumbusha namna nilitenda kama mutoto kabisa.”—Diane. *

“Nililalamika kwa nguvu, ‘Uko baba mubaya sana!’ na nikagonga mulango sana. Lakini mbele mulango ujifunge, niliona baba akiangalia kwa huzuni, na mara moja nilipenda kurudisha wakati nyuma na kumeza maneno niliyosema.”—Lauren.

Hali yako inafanana na ya Lauren na Diane? Ikiwa ndiyo, habari hii inaweza kukusaidia.

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Milipuko ya hasira inaharibisha sifa yako. Briana, aliye sasa na miaka 21, anasema hivi: “Nilizoea kufikiri kuwa watu wengine wanapaswa tu kukubali hasira yangu. Lakini kisha nilianza kutambua kuwa watu wanaonekana kuwa wapumbavu wakati hawajizuie, na nilitambua kuwa ni vile nilionekana kwa wengine!”

Biblia inasema hivi: “Yule anayekasirika upesi atatenda upumbavu.”—Methali 14:17.

Watu watakimbia ikiwa kuna mulipuko wa volkeno; vilevile, wataepuka mutu mwenye kuwa na mulipuko wa hasira

Hasira yako inaweza kufanya watu wakuepuke. Daniel, aliye na miaka 18, anasema hivi: “Wakati unakasirika, watu wanaokuzunguka hawakuheshimu tena.” Elaine, aliye pia na miaka 18, anakubaliana na jambo hilo. Anasema hivi: “Kuonyesha hasira hakuvutie. Kunafanya tu watu wakuogope.”

Biblia inasema hivi: “Usiwe na urafiki pamoja na mutu mwenye hasira nyingi; Wala usiende pamoja na mutu wa gazabu nyingi.”—Methali 22:24, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo.

Unaweza kubadilika. Sara, aliye na miaka 15, anasema hivi: “Sikuzote, hauwezi kuzuia namna hali fulani inakufanya ujisikie, lakini unaweza kuzuia namna ya kuonyesha jinsi unajisikia katika moyo. Hauna sababu ya kulipuka kwa hasira.”

Biblia inasema hivi: ‘Asiye mwepesi wa hasira ni bora kuliko mwanaume mwenye nguvu, naye anayezuia roho yake ni bora kuliko mutu anayeteka [anayekamata] jiji.’—Methali 16:32.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Jiwekee muradi. Kuliko kusema “Hiyo ndiyo hali yangu,” jikaze kubadilika katika kipindi fulani, labda katika miezi sita. Katika kipindi hicho, andika maendeleo yako nafasi fulani. Kila wakati unapokasirika, andika (1) jambo lenye lilitokea, (2) namna ulitenda, na (3) namna ungetenda kwa njia ya muzuri, na sababu gani ungefanya hivyo. Kisha, ujiwekee muradi wa kutumia namna hiyo ya muzuri ya kutenda wakati utachokozwa tena. Shauri: Andika pia maendeleo yako! Andika juu ya namna unavyojisikia muzuri kisha kuonyesha sifa ya kujizuia.—Kanuni ya Biblia: Wakolosai 3:8.

Usitende haraka. Wakati mutu fulani ao kitu fulani kinakukasirisha, usiseme neno la kwanza linalokuja katika akili yako. Lakini, ungojee. Vuta pumuzi kabisa ikiwa ni lazima. Erik, aliye na miaka 15, anasema hivi: “Wakati ninavuta pumuzi, hilo linanitolea wakati wa kufikiri mbele nifanye ao kusema jambo fulani lenye nitahuzunikia baadaye.”—Kanuni ya Biblia: Methali 21:23.

Panua mawazo yako. Wakati fulani unaweza kukasirika kwa sababu unaona tu sehemu moja ya hali fulani, ni kusema, sehemu inayokukasirisha. Jaribu kufikiria sehemu ingine ya hali hiyo. Kijana mwanamuke anayeitwa Jessica anasema hivi: “Hata wakati watu wananitendea bila adabu kabisa, kwa kawaida kuna maelezo fulani yanayoweza kunisaidia niwaelewe kidogo.”—Kanuni ya Biblia: Methali 19:11.

Ikiwa ni lazima, ondoka hapo. Biblia inasema hivi: ‘Kabla mabishano hayajalipuka, ujiondokee.’ (Methali 17:14) Kama vile andiko hilo linasema, wakati fulani ni muzuri tu kuondoka katika hali inayochochea hasira. Kwa hiyo, kuliko kuendelea kuwaza juu ya tatizo na kuacha hasira yako ipande zaidi, usibakie bila kufanya jambo lolote. Kijana mwanamuke anayeitwa Danielle anasema hivi: “Ninaona kuwa kufanya mazoezi ya mwili kunaweza kupunguza mahangaiko yangu ya akili na kunisaidia nisipandwe na hasira.”

Jifunze kutofuatilia kila jambo. Biblia inasema hivi: ‘Mufazaike, lakini musitende zambi. Museme moyoni mwenu, . . . na kunyamaza.’ (Zaburi 4:4) Ona kama hakuna ubaya wa kujisikia mwenye kufazaika. Ulizo ni, Ni nini kitatokea kisha hapo? Kijana mwanaume anayeitwa Richard anasema hivi: “Ikiwa unaacha wengine wakukasirishe, hilo linawafanya wakuwe na uwezo juu yako. Sababu gani usijikaze kuwa mutu muzima na kuacha jambo hilo lipite?” Ukifanya hivyo, utatawala hasira yako kuliko kuacha hasira ikutawale.

^ fu. 4 Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.