Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MAWAZO YA BIBLIA

Mateso

Mateso

Watu fulani wanafikiri kuwa ni Mungu ndiye analetea watu mateso na kwamba ikiwa haiko yeye ndiye anayaleta, maana yake hayahangaikie. Lakini ni hivyo Biblia inafundisha? Jibu la Biblia linaweza kukushangaza.

Ni Mungu ndiye anatuletea mateso?

“Kwa kweli, Mungu hatendi kwa uovu.”Ayubu 34:12.

MAMBO WATU WANASEMA

Watu fulani wanasema kuwa kila jambo linalotokea ni mapenzi ya Mungu. Kwa hiyo, wanaamini kama Mungu ndiye anatuletea mateso. Kwa mufano, wakati misiba ya asili inatokea, wanawaza kuwa matukio hayo ni njia ya Mungu ya kuazibu watu waliotenda zambi.

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia inafundisha waziwazi kama Mungu hatuletee mateso. Kwa mufano, Biblia inasema kama wakati tunajaribiwa, ni kosa kusema, “Mungu ananijaribu.” Sababu gani? Kwa sababu ‘Mungu hawezi kujaribiwa na mambo maovu wala yeye mwenyewe hamujaribu yeyote.’ (Yakobo 1:13) Katika maneno mengine, haiko Mungu ndiye anatuletea majaribu yanayotupata ao mateso yanayotokana na majaribu hayo. Kufanya hivyo ingekuwa uovu, lakini “Mungu hatendi kwa uovu.”—Ayubu 34:12.

Ikiwa haiko Mungu ndiye anatuletea mateso, sasa ni nini ao ni nani anayetuletea mateso? Jambo la kuhuzunisha ni hili: watu wanateswa na watu wengine wasio wakamilifu. (Mhubiri 8:9) Tena, tunaweza kupata mateso kwa sababu ya “tukio lisilotazamiwa,” ni kusema, kwa sababu tu ya kuwa mahali pasipofaa wakati usiofaa. (Mhubiri 9:11) Biblia inafundisha kama kwa vyovyote, Shetani Ibilisi, ‘mutawala wa ulimwengu huu’ ndiye analetea watu mateso, kwa sababu ‘ulimwengu muzima unakaa katika nguvu za yule muovu.’ (Yohana 12:31; 1 Yohana 5:19) Ni Shetani ndiye anafanya watu wateseke, lakini haiko Mungu.

Mungu anahangaikia mateso yetu?

‘Wakati wa taabu zao zote hilo lilimutaabisha.’Isaya 63:9.

MAMBO WATU WANASEMA

Watu fulani wanawaza kama Mungu hahangaikie mateso yetu. Kwa mufano, muandikaji mumoja anataja kile anaita kuwa “kukosa rehema ao huruma [kwa Mungu] kuelekea mateso yetu.” Muandikaji huyo anasema kuwa ikiwa Mungu iko, maana yake anawaona watu “bila huruma na bila kuwahangaikia.”

MAMBO BIBLIA INASEMA

Biblia haiseme kuwa Mungu hana huruma na hahangaikie watu, lakini inafundisha kuwa Mungu anahuzunishwa sana na mateso yetu, na kuwa atayamaliza hivi karibuni. Chunguza mafundisho tatu ya Biblia yenye kufariji.

Mungu anajua mateso yetu. Tangu tu mateso ya watu yalipoanza, hakuna hata chozi moja ambalo limeanguka bila Yehova * kuona, kwa kuwa ‘macho yake yanayongaa’ yanaona kila kitu. (Zaburi 11:4; 56:8) Kwa mufano, waabudu wake walipoteswa wakati wa zamani, Mungu alisema hivi: “Pasipo shaka nimeyaona mateso ya watu wangu.” Lakini, alijua mateso yao kijuujuu tu? Hapana, kwa sababu aliongeza hivi: ‘Ninajua vizuri maumivu waliyo nayo.’ (Kutoka 3:7) Watu wengi wamepata faraja kwa kujua tu jambo hilo, ni kusema, kujua kama Mungu anajua mateso yote yanayotupata, hata majaribu yenye pengine watu wengine hawajue ao hawaelewe kabisa.—Zaburi 31:7; Methali 14:10.

Mungu anajisikia mubaya wakati tunateseka. Yehova anajua mateso yetu na yanamuhuzunisha sana. Kwa mufano, Mungu aliumia kabisa moyoni wakati waabudu wake wa zamani waliteseka. Biblia inasema hivi: ‘Wakati wa taabu zao zote hilo lilimutaabisha.’ (Isaya 63:9) Hata ikiwa Mungu ni mukubwa sana kupita watu, anasikilia huruma watu wanaoteseka, ni kama vile maumivu yao yako katika moyo wake! Kwa kweli, Yehova “ni mwenye rehema sana, mwenye huruma.” (Yakobo 5:11, La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo) Tena, Yehova anatusaidia kuvumilia mateso yetu.—Wafilipi 4:12, 13.

Mungu atamaliza mateso yote ya watu. Biblia inaonyesha kuwa Mungu atamaliza mateso ya kila mutu kwenye dunia. Kupitia Ufalme wake wa mbinguni, Yehova atabadilisha kabisa hali ya watu na kuifanya ikuwe ya muzuri. Juu ya wakati huo, Biblia inaahidi kuwa Mungu “atafuta kila chozi kutoka katika macho yao, na kifo hakitakuwapo tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu hayatakuwapo tena. Mambo ya zamani yamepitilia mbali.” (Ufunuo 21:4) Itakuwa namna gani juu ya watu wenye tayari wamekufa? Mungu atawafufua waishi tena hapa duniani ili wao pia wafurahie uzima bila mateso. (Yohana 5:28, 29) Kuna mutu yeyote atakayesumbuliwa kwa kuendelea kukumbuka mateso ya wakati uliopita? Hapana, kwa sababu Yehova anaahidi hivi: “Mambo ya zamani hayatakumbukwa akilini, wala hayataingia moyoni.”—Isaya 65:17. *

^ fu. 13 Yehova ni jina la Mungu kama vile inaonyeshwa katika Biblia.

^ fu. 15 Ili kujua sababu gani Mungu anaacha watu wateseke kwa muda fulani na namna atamaliza mateso, tafazali soma sura ya 8 na ya 11ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova..