Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

MUSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | KULEA WATOTO

Kufundisha Watoto Unyenyekevu

Kufundisha Watoto Unyenyekevu

MAGUMU

  • Mutoto wako anajiendesha kwa kiburi, na iko tu na miaka kumi!

  • Anapenda kila mutu amutendee kama mutu wa maana sana.

Pengine unawaza hivi: ‘Sababu gani anajiendesha hivyo? Napenda ajisikie muzuri, lakini sipendi ajione kuwa wa maana kuliko kila mutu!’

Inawezekana kufundisha mutoto unyenyekevu bila kumufanya ajione kuwa wa bure?

MAMBO UNAPASWA KUJUA

Katika miaka ya hivi karibuni, wazazi walitiwa moyo kutimizia watoto kila kitu chenye wanataka; kuwapongeza kila mara, hata kama hawakufanya jambo lenye wanastahili kupongezwa; kujizuia kuwakaripia ao kuwapatia malipizi. Ilizaniwa kwamba kama watoto wanafanywa wajisikie kuwa wa maana, watakomaa wakijiona kuwa wenye kustahili kabisa. Lakini, matokeo yamekuwa namna gani? Kitabu Generation Me (Kizazi cha Mimi Kwanza) kinasema hivi: “Kuliko kutokeza watoto wenye kuwa na usawaziko na wenye kuwa na furaha, mupango wa kufanya watoto wajione kuwa wa maana umetokeza jeshi la watoto wenye kujipenda kupita mipaka.”

Watoto wengi wenye wamekomalishwa kwa kupongezwa kila mara bila sababu yoyote wamekomaa bila kuwa tayari kwa ajili ya hali zenye kuvunja moyo, kuchambuliwa, na kushindwa wakati fulani. Kwa sababu ya kufundishwa kukazia akili tamaa zao, inakuwa nguvu kuwa na uhusiano wenye kudumu na wengine wakati wanakuwa watu wazima. Matokeo ni kwamba wengi kati yao wanapatwa na mahangaiko na kushuka moyo.

Watoto wanajiona kuwa wa maana kwa njia yenye kufaa, hapana kwa kuambiwa kila mara kwamba ni watu wa maana, lakini kupitia mambo yenye wanatimiza kabisa. Kujiamini tu hakutoshe ili kutimiza kusudi hilo. Wanapaswa kujifunza, kufanya mazoezi, na kujua muzuri kufanya ufundi fulani. (Methali 22:29) Wanapaswa pia kuhangaikia mahitaji ya watu wengine. (1 Wakorintho 10:24) Mambo yote hayo yanaomba unyenyekevu.

MAMBO UNAWEZA KUFANYA

Umupongeze wakati anastahili kabisa. Kama mutoto wako mwanamuke anaweza sana kwenye masomo, umupongeze. Kama anapata nukta ndogo, usilaumu mara moja mwalimu. Ukifanya hivyo, itakuwa nguvu kwa mutoto wako kujifunza unyenyekevu. Kuliko kufanya hivyo, umusaidie aone namna anaweza kufanya muzuri zaidi wakati wenye kuja. Umupongeze wakati anafanya tu mambo ya muzuri.

Ukaripie mutoto wakati ni lazima kufanya hivyo. Hilo halimaanishe kwamba unapaswa kuchambua mutoto wako kwa kila kosa lenye anafanya. (Wakolosai 3:21) Lakini, unapaswa kukaripia makosa makubwa. Unapaswa kufanya hivyo pia kuhusu tabia za mubaya. Kama haufanye hivyo, inaweza kuwa nguvu kubadilisha tabia zao baadaye.

Kwa mufano, wazia kwamba mutoto wako anaonyesha muelekeo wa kujivuna. Kama hakaripiwe, anaweza kuwa na kiburi na kuanza kujitenga na wengine. Kwa hiyo, ufasirie mutoto wako kwamba kujivuna kunamufanya aonekane mubaya na kunaweza kumupatisha haya. (Methali 27:2) Umufasirie pia kwamba mutu mwenye kuwa na mawazo yenye kufaa juu yake hana lazima ya kutangazia wengine uwezo wake mbalimbali. Kwa kutoa karipio kama hilo katika roho ya upendo, utamufundisha unyenyekevu bila kumufanya ajione kuwa wa bure.​—Kanuni ya Biblia: Mathayo 23:12.

Tayarisha mutoto wako kwa ajili ya mambo ya maisha. Kutimiza kila jambo lenye mutoto anapenda kunaweza kumufanya ajisikie kama iko na haki ya kupata kila kitu. Kwa mufano, kama mutoto wako anaomba kitu chenye hauna uwezo wa kununua, umufasirie sababu gani ni lazima kuishi kulingana na feza yenye unapata. Kama ni lazima kuvunja mupango wa kufanya matembezi ao mapumuziko, unapaswa kumufasiria kwamba kuvunjika moyo ni sehemu ya maisha na pengine uzungumuze naye kuhusu jambo lenye unafanya wakati unapatwa na hali kama hizo. Kuliko kulinda watoto wako na kila tatizo, uwatayarishe kuhusu magumu yenye watapata wakati watakuwa watu wazima.​—Kanuni ya Biblia: Methali 29:21.

Umufundishe kuwa mutoaji. Onyesha mutoto wako kwamba “kuna furaha zaidi katika kutoa kuliko ilivyo katika kupokea.” (Matendo 20:35) Namna gani? Wewe pamoja naye, munaweza kutayarisha liste ya watu wenye kuwa na lazima ya musaada ili kuwanunulia vitu mbalimbali, kuwabeba, ao kuwatengenezea vitu vyao. Kisha, uende pamoja na mutoto wako wakati unasaidia wamoja kati yao. Uache mutoto wako aone furaha yako wakati unatimizia wengine mambo yenye wako nayo lazima. Kufanya hivyo kutafundisha mutoto wako unyenyekevu katika njia kubwa zaidi, ni kusema, kupitia mufano wako.​—Kanuni ya Biblia: Luka 6:38.