Ona video zinazopatikana

Ona habari zilizo ndani

SOMO LA 2

Namna ya Kuwa Munyenyekevu

Namna ya Kuwa Munyenyekevu

UNYENYEKEVU MAANA YAKE NINI?

Mutu munyenyekevu anaonyesha heshima. Hatende kwa kiburi, wala hawaze kama wengine wanapaswa kumutendea kama vile mutu wa maana sana. Lakini, mutu munyenyekevu anahangaikia kabisa wengine na iko tayari kujifunza kupitia watu hao.

Watu fulani wanajidanganya kwa kuwaza kama unyenyekevu ni uzaifu. Lakini kwa kweli, unyenyekevu ni nguvu yenye inamusaidia mutu akubali makosa yake na atambue kama kuko mambo yenye hana uwezo wa kufanya.

JUU YA NINI UNYENYEKEVU NI WA MAANA?

  • Unyenyekevu unasaidia mutu asikilizane na watu wengine. Kitabu The Narcissism Epidemic kinasema hivi: “Kwa ujumla, ni mwepesi zaidi kwa watu wanyenyekevu kupata marafiki.” Kinasema tena kama kwa watu kama hao ni “mwepesi zaidi kuzungumuza na kujiunga na wengine, na wanaweza kufanya vile na watu mingi zaidi.”

  • Unyenyekevu utamusaidia mutoto wako mu maisha yake ya wakati wenye kuja. Kama mutoto wako anajifunza kuwa munyenyekevu leo, itakuwa mwepesi zaidi kwake kupata kazi wakati atakuwa mukubwa. Munganga Leonard Sax anaandika hivi: “Kama kijana anajionaka sana, na anawaza kama anaweza kufanya kila kitu, hawezi kufurahisha mutu mwenye kumuuliza maulizo juu ya kumupatia kazi. Lakini kijana mwenye anapenda kabisa kujua kile chenye mutu mwenye kumuuliza maulizo kwa ajili ya kazi anapenda, anaweza kupata kazi.” *

NAMNA YA KUFUNDISHA MUTOTO UNYENYEKEVU

Umusaidie mutoto wako aepuke kujipandisha.

KANUNI YA BIBLIA: “Kama mutu yeyote anawaza yeye ni kitu wakati yeye haiko kitu, anajidanganya yeye mwenyewe.”​—Wagalatia 6:3.

  • Epuka misemo yenye haiko ya kweli. Misemo kama vile “Ndoto zako zote zinaweza kutimia” na “Unaweza kuwa chochote chenye unataka” inaweza kuonekana kuwa yenye kutia moyo, lakini mara mingi haikuwake ya kweli mu maisha ya kawaida. Watoto wako wanaweza kuwa na maisha ya muzuri kama wanajiwekea mipango yenye wanaweza kufikia na kama wanatumika sana ili kuitimiza.

  • Onyesha wazi mambo yenye inafanya umusifu. Kuambia tu mutoto kama anafanya mambo “muzuri sana” hakumusaidie akuwe munyenyekevu. Ukuwe wazi wakati unamusifu.

  • Usikubali mutoto wako atumie bila mipaka njia za kupashana habari ku Enternete. Mara mingi, ku Enternete, watu wanapenda kujipandisha kwa kuonyesha uwezo wao mbalimbali na mambo yenye wametimiza. Ile ni tofauti sana na unyenyekevu.

  • Umutie moyo mutoto wako kuomba musamaha bila kukawia. Wakati mutoto wako anafanya jambo fulani la mubaya, umusaidie kutambua kosa lake na kulikubali.

Umutie moyo kuonyesha shukrani.

KANUNI YA BIBLIA: “Mujionyeshe kuwa wenye shukrani.” ​—Wakolosai 3:15.

  • Umufundishe kuonyesha shukrani kwa sababu ya uumbaji. Watoto wanapaswa kujifunza kuonyesha shukrani juu ya vitu vyote vyenye viliumbwa na kuelewa kama tuko na lazima sana ya vile vitu ili tuendelee kuishi. Tuko na lazima ya hewa ili kupumua, maji ya kunywa, na chakula. Utumie ile mifano ili kumusaidia mutoto aone kama Muumbaji ni wa ajabu, na ili kumusaidia aonyeshe shukrani kwa vitu vyote vya muzuri sana vyenye kuwa katika uumbaji.

  • Umufundishe kuonyesha watu shukrani. Saidia mutoto wako aepuke kusikilia wengine wivu juu wako wanafanya mambo muzuri zaidi ao wako na uwezo zaidi, lakini umuonyeshe kama anaweza kujifunza kupitia watu hao.

  • Umufundishe namna ya kuonyesha shukrani. Fundisha watoto wako kusema “aksanti,” hapana tu kwa maneno, lakini kwa kuonyesha shukrani ya kweli. Kuwa wenye shukrani kunatusaidia tuendelee kuwa wanyenyekevu.

Umufundishe mutoto wako kama ni muzuri kusaidia wengine.

KANUNI YA BIBLIA: “Kwa unyenyekevu muone wengine kuwa wazuri zaidi kuliko ninyi, mukiendelea kuangalia, hapana faida zenu ninyi wenyewe tu, lakini pia faida za wengine.”​—Wafilipi 2:3, 4.

  • Mutoto wako anapaswa kusaidia kufanya kazi za nyumbani. Kuambia mutoto wako kama hapaswe kusaidia kufanya kazi za nyumbani ni kama vile kumuambia kama ‘Uko wa maana sana, haupaswe kufanya hizi kazi!’ Mutoto anapaswa kutanguliza kwanza kazi za nyumbani mbele ya michezo. Umuonyeshe namna kufanya kazi za nyumbani kunaletea wengine faida, na kuwa wengine watafurahi na kumuheshimia wakati anawasaidia.

  • Ukazie kama ni muzuri kusaidia wengine. Kufanya mambo kwa faida ya wengine kutasaidia watoto wakuwe wakomavu. Kwa hiyo, utie moyo mutoto wako atafute watu wenye kuwa na lazima ya musaada. Umusaidie ajue ni nini anaweza kufanya ili kuwasaidia. Umusifu na umuunge mukono wakati anasaidia wengine.

^ fu. 8 Inatoka mu kitabu The Collapse of Parenting.