Hamia kwenye habari

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Agano la Kale?

Je, Mashahidi wa Yehova Wanaamini Agano la Kale?

 Ndiyo. Mashahidi wa Yehova wanaamini kwamba Biblia nzima ‘imeongozwa na roho ya Mungu na ni yenye faida.’ (2 Timotheo 3:​16) Biblia nzima inatia ndani maandiko yanayojulikana kama Agano la Kale na Agano Jipya. Kwa kawaida, Mashahidi wa Yehova huita sehemu hizo Maandiko ya Kiebrania na Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo. Tunaziita hivyo ili watu wasiwe na wazo la kwamba sehemu fulani za Biblia zimepitwa na wakati au si muhimu.

Kwa nini Wakristo wanahitaji sehemu zote mbili, yaani, Agano la Kale na pia Agano Jipya?

 Akiongozwa na roho ya Mungu, mtume Mkristo Paulo aliandika hivi: “Mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha sisi.” (Waroma 15:4) Kwa hiyo, kuna habari muhimu kwa ajili yetu katika Maandiko ya Kiebrania. Habari hizo zinatia ndani masimulizi ya kihistoria yenye faida kwetu leo na mashauri yanayofaa.

  •   Masimulizi ya kihistoria. Maandiko ya Kiebrania yana rekodi ndefu ya uumbaji na jinsi mwanadamu alivyotumbukia kwenye dhambi. Ikiwa hatungekuwa na habari hizo, hatungepata majibu yenye kuridhisha kwa maswali haya: Tulitoka wapi? Kwa nini wanadamu hufa? (Mwanzo 2:7, 17) Pia, Maandiko ya Kiebrania yana rekodi ya jinsi Yehova Mungu alivyoshughulika na watu waliopata shangwe na matatizo kama yetu.​—Yakobo 5:​17.

  •   Mashauri yanayofaa. Vitabu vya Biblia vya Methali na Mhubiri, ambavyo ni sehemu ya Maandiko ya Kiebrania, vina hekima yenye kudumu ambayo inaweza kutusaidia maishani. Vitabu hivyo vina mashauri ya jinsi ya kufurahia maisha ya familia (Methali 15:17), jinsi ya kuwa na maoni yaliyosawazika kuhusu kazi (Methali 10:4; Mhubiri 4:6), na jinsi vijana wanaweza kutumia ujana wao kwa njia itakayowaletea furaha maishani (Mhubiri 11:9–12:1).

 Isitoshe, tunaweza kufaidika tukisoma Sheria ya Musa ambayo imeandikwa katika Torati (vitabu vitano vya kwanza vya Biblia). Ingawa Wakristo hawako chini ya Sheria hiyo, ina kanuni muhimu ambazo zinaweza kutusaidia kuwa na maisha yenye furaha.​—Mambo ya Walawi 19:18; Kumbukumbu la Torati 6:​5-7.