Kwa Waroma 15:1-33

  • Karibishaneni kama Kristo alivyofanya (1-13)

  • Paulo, mtumishi kwa mataifa (14-21)

  • Mipango ya safari za Paulo (22-33)

15  Basi, sisi tulio na nguvu tunapaswa kubeba udhaifu wa wale wasio na nguvu,+ na tusiwe tukijipendeza wenyewe.+  Kila mmoja wetu na ampendeze jirani yake kwa mema, ili kumjenga.+  Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe,+ bali kama ilivyoandikwa: “Shutuma za wale wanaokushutumu zimeniangukia.”+  Kwa maana mambo yote yaliyoandikwa zamani yaliandikwa ili kutufundisha,+ ili kupitia uvumilivu wetu+ na kupitia faraja kutoka kwa Maandiko tuwe na tumaini.+  Basi Mungu anayetoa uvumilivu na faraja na awawezeshe ninyi miongoni mwenu wenyewe kuwa na mtazamo uleule wa akili ambao Kristo Yesu alikuwa nao,  ili kwa umoja+ na kwa sauti moja* mumtukuze Mungu na Baba ya Bwana wetu Yesu Kristo.  Basi mkaribishane,*+ kama vile Kristo pia alivyowakaribisha,+ kwa kusudi la kumtukuza Mungu.  Kwa maana ninawaambia kwamba Kristo alikuwa mhudumu wa wale waliotahiriwa+ kwa ajili ya ukweli wa Mungu, ili kuthibitisha ahadi ambazo Yeye aliwapa mababu zao,+  na kwamba mataifa yamtukuze Mungu kwa sababu ya rehema yake.+ Kama ilivyoandikwa: “Ndiyo sababu nitakukiri wewe waziwazi kati ya mataifa nami nitakwimbia nyimbo za sifa.”+ 10  Tena anasema: “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake.”+ 11  Tena: “Msifuni Yehova,* enyi mataifa yote, na watu wote wamsifu yeye.”+ 12  Na tena Isaya anasema: “Kutakuwa na mzizi wa Yese,+ yule anayesimama ili kutawala mataifa;+ na mataifa yatamtumainia yeye.”+ 13  Mungu anayetoa tumaini na awajaze ninyi shangwe yote na amani kwa kumtegemea, ili tumaini lenu liongezeke* kwa nguvu za roho takatifu.+ 14  Ndugu zangu, sasa mimi mwenyewe nimesadiki kuwahusu, kwamba ninyi pia mmejaa wema, mmejaa ujuzi wote, na kwamba mnaweza kuonyana.* 15  Hata hivyo, nimewaandikia waziwazi zaidi kuhusu mambo fulani, ili kuwakumbusha tena, kwa sababu ya fadhili zisizostahiliwa nilizopewa kutoka kwa Mungu 16  ili niwe mtumishi wa watu wote wa Kristo Yesu kwa mataifa.+ Ninafanya kazi takatifu ya habari njema ya Mungu,+ ili mataifa haya yawe toleo linalokubalika, lililotakaswa kwa roho takatifu. 17  Basi nina sababu ya kufurahi katika Kristo Yesu kuhusu mambo yanayohusiana na Mungu. 18  Kwa maana sitathubutu kusema kuhusu chochote isipokuwa yale ambayo Kristo amefanya kupitia mimi ili mataifa yatii, kwa maneno na matendo yangu, 19  kwa nguvu za ishara na mambo ya ajabu,*+ kwa nguvu za roho ya Mungu, hivi kwamba kutoka Yerusalemu na kuzunguka mpaka Ilirikamu nimehubiri kikamili habari njema kuhusu Kristo.+ 20  Kwa kweli, katika njia hii, nilikusudia kwamba nisitangaze habari njema mahali ambapo jina la Kristo lilikuwa limetangazwa tayari, ili nisijenge juu ya msingi wa mtu mwingine; 21  bali, kama ilivyoandikwa: “Wale ambao hawajapata ujumbe wowote kumhusu wataona, na wale ambao hawajasikia wataelewa.”+ 22  Pia hiyo ndiyo sababu nilizuiwa mara nyingi kuja kwenu. 23  Lakini sasa sina tena eneo ambalo halijaguswa katika maeneo haya, na kwa miaka mingi* nimetamani kuja kwenu. 24  Kwa hiyo, nikisafiri kwenda Uhispania, natumaini kwamba nitawaona na mtanisindikiza umbali fulani, baada ya mimi kufurahia ushirika wenu kwa muda. 25  Lakini sasa ninakaribia kusafiri kwenda Yerusalemu kuwahudumia watakatifu.+ 26  Kwa maana wale walio Makedonia na Akaya wamependezwa kushiriki vitu vyao kwa kuwatolea mchango fulani walio maskini kati ya watakatifu huko Yerusalemu.+ 27  Kweli, wamependezwa kufanya hivyo, na kwa hakika walikuwa wadeni kwao; kwa maana ikiwa mataifa wameshiriki mambo yao ya kiroho, wao pia wana deni la kuwahudumia kwa vitu vyao vya kimwili.+ 28  Basi nikimaliza jambo hili na kuwafikishia mchango huu* salama, nitaondoka na kupitia kwenu nikielekea Uhispania. 29  Isitoshe, najua kwamba nitakapokuja kwenu nitakuja nikiwa na kipimo kamili cha baraka kutoka kwa Kristo. 30  Sasa ninawahimiza ninyi, akina ndugu, kupitia Bwana wetu Yesu Kristo na kupitia upendo wa roho, kwamba mjikaze pamoja nami katika kusali kwa Mungu kwa ajili yangu,+ 31  ili nikombolewe+ kutoka kwa wale wasio waamini huko Yudea na kwamba huduma yangu kwa ajili ya Yerusalemu ikubalike kwa watakatifu,+ 32  ili kwa mapenzi ya Mungu nije kwenu nikiwa na shangwe na kuburudishwa pamoja nanyi. 33  Mungu anayetoa amani na awe pamoja nanyi nyote.+ Amina.

Maelezo ya Chini

Tnn., “kinywa kimoja.”
Au “muwakubali wengine.”
Au “lifurike.”
Au “kufundishana.”
Au “miujiza.”
Au labda, “kadhaa.”
Tnn., “tunda hili.”